Thursday, December 31, 2015
Hii Ni Silaha Mojawapo Ya Watu Waliofanikiwa.
Wednesday, December 30, 2015
Jifunze Kupitia Vitu Hivi Viwili.
Tuesday, December 29, 2015
Acha Kuangalia Matawi Pekee Kama Kweli Unataka Kufanikiwa.
Monday, December 28, 2015
Jiulize Swali Hili Kwa Kila Unalolifanya.
Monday, December 21, 2015
Hakuna Uhusiano Wa Moja Kwa Moja Kati Ya Vitu Hivi Viwili.
Friday, December 18, 2015
Kitu Hiki Kimoja Kinakufanya Usifanikiwe Maishani.
Thursday, December 17, 2015
Zifahamu Sumu Nne (4) Za Mafanikio Yako.
Monday, December 14, 2015
Anza Na Kitu Hiki Kimoja Kama Kweli Unataka Kufanikiwa.
Monday, December 7, 2015
Lini Basi Itakuwa Zamu Yako?
Saturday, December 5, 2015
Hiki Ni Kitu Muhimu Sana Kuliko Unavyodhani.
Leo tena nakupa kitu kipya na kitu hicho ni umuhimu wa hatua moja. Je ulishawahi kufikiria umuhimu wa hatua moja? Basi endelea kusoma makala hii ili uweze kuufahamu umuhimu wa hatua moja.
Chukulia mfano ulikuwa unatembea kuelekea mahali usipo kujua katika kutembea huko ukafika sehemu ambapo kuna korongo kubwa sana ambapo ukitumbukia huko hakuna kupona na katika safari yako ilikuwa imebaki hatua moja tu ambayo ungeimalizia tu basi ulikuwa unatumbukia kwenye korongo hilo hivyo basi unamua kutokupiga ile hatua ya mwisho na hapo unakuwa umeokoa maisha yako.
Mfano mwingine, chukulia upo katika mashindano fulani ya mbio ambapo mshindi anapewa zawadi ya gari na nyumba. Ukaingia katika mashindano hayo huku ukiwa na uhakika na shauku ya kushinda hivyo ukaanza mbio hizo kwa kasi sana ukawaacha wapinzani mbali sana,lakini ghafla kabla ya kufika kwenye mstari wa mwisho ambapo ni hatua moja tu ili kufika mwisho ukaanguka vibaya sana na ikawa ngumu sana kwa wewe kuinuka, lakini kumbuka ni hatua moja tu ndio ilikuwa imebakia basi kwa kutambua hilo unajikakamua pamoja na maumivu yako unainuka na kumaliza mbio wa kwanza na hivyo kutangazwa mshindi na kujishindia zawadi. Jiulize ingekuwaje kama usinge jikakamua na kumalizia ile hatua moja.
Nimekuwekea mifano miwili ambapo mfano wa kwanza unaonesha umuhimu wa kupunguza hatua ili kuokoa maisha yetu. Inawezekana umekuwa ukifanya mambo mengi sana, sasa chagua jambo moja kati ya mambo mengi unayofanya na ulishikilie hilo mpaka ulikamilishe. Pia mfano huo unatuonesha na kutufunza kuwa ni muhimu tuyachunguze maisha yetu ili tuweze kubaini vikwazo vya ndoto zetu na tuvitoe.
Mfano wa pili unatuonesha kuwa tunaweza kukutana na vikwazo mbalimbali maishani ambavyo vinaweza kusababisha tusiyafikirie malengo yetu na hivyo kushindwa kabisa kuyatekeleza malengo yetu. Vikwazo hivyo ni kama kushindwa, kukata tamaa, hasara katika biashara, uvivu n.k. hivyo basi mfano huu unatuonesha kuwa pamoja na vikwazo vyote sisi tusonge mbele tu tusirudi nyuma kamwe.
Hatua moja ni muhimu iwe kwa kuiongeza au kuipunguza, hivyo jifunze wapi pa kuongeza hatua na ni wapi pa kupunguza. Maana hatua moja kati ya nyingi ndio huamua maisha yetu.
Ni Mimi rafiki yako,
Baraka Maganga.
Bmaganga22@gmail.com.
0754612413/0652612410.
posted from Bloggeroid
Ijue Silaha Muhimu Ya Kutumia Kupambana Katika Safari Yako Ya Mafanikio
Friday, December 4, 2015
Vitu vine (4) Muhimu Katika Safari Yako Ya Kuelekea Mafanikio.
Habari za wakati huu ndugu msomaji wa mtandao huu wa kona ya maarifa ni matumaini yangu kuwa hu mzima wa afya na unaendeleza mapambano ya kuzisaka fursa na kuzitumia na kwa zile ambapo zimekwisha patikana unahakikisha hazikuponyoki kizembe nami nasema kazana kwani mapambano yanaendelea hakuna kuchoka mpaka tutimize malengo yetu.
Leo nataka kukushirkisha mambo manne muhimu ambayo unahitaji kuwa nayo ili kuweza kufanikisha safari yako ya mafanikio. Kama ilivyo katika safari za kawaida ambazo tumekuwa tukisafiri mara kwa mara aidha kwa usafiri wa magari, ndege au meli. Huwa kuna kuwa na vitu ambavyo ndio kama mahitaji ya safari zetu, yaani bila vitu hivyo safari zetu zinaweza kuwa za kusuasua na zenye kukosa mwelekeo. Chukulia mfano leo hii unataka kwenda sehemu alafu huna tiketi ya kukuwezesha kufika huko, nina uhakika safari yako itakuwa ya kusuasua na unaweza usisafiri sidhani kama leo hii unaweza kusafiri kwa basi au ndege pasipo kuwa na nauli. Mambo haya yafuatayo ni muhimu sana katika safari yako ya mafaniko yaani ni kama tiketi katika safari yako. Endelea……..
1. Njozi, ili ufanikiwe unahitaji kuwa na njozi tena si njozi bora njozi bali njozi kubwa njozi itakayokunyima usingizi wakati mwingine . njozi kwa lugha nyingine huitwa ndoto(dream). Njozi ni namna au kadiri unavyoyaona maisha yako na yatakavyokuwa baada ya kipindi Fulani cha maisha mfano,unayaonaje maisha yako baada ya miaka miwili,mitano, kumi au ishirini ijayo mbele. Unajiona kuwa utakuwa unamiliki nini haswa je unaliona gari la ndoto yako ukiwa ndani yake, nyumba, shamba ama viwanja?. Uwezo huo ndio hujulikana kama ndoto na ni muhimu sana katika maisha yako kama kweli unataka kufanikiwa.
2. Elimu, elimu ni kitu cha muhimu sana tena sana, iwe ile ya darasani au ile ya kujiendeleza baada ya ile ya darasani kwa wakati huu ambapo kuna ushindani mkubwa sana katika soko ni bora ukawa na hata degree moja. Elimu ya darasani ni muhimu kwa kuwa itakufungua na kukupa mwanga wa maisha, lakini pia katika dunia ya sasa elimu ya darasani pekee haitoshi kukufanya wewe mwenye mafanikio. Bali elimu hii nyingine ya tofauti na ile ya darasani ina umuhimu mkubwa sana katika ndunia ya sasa ambayo imejaa changamoto nyingi. Kuna semina mbalimbali ambazo zimekuwa zikiendeshwa kuhusu mambo mbalimbali kama vile ujasiriamali na biashara, kuna vitabu mbalimbali vya uhamasishaji,ujasiriamali, uwekezaji, biashara n.k.vile vile kuna video ambazo unaweza kuzipata youtube ama kununua dvd. yote haya ni katika kuhakikisha unapata elimu ya kile unachokitaka.
3. Afya, hiki ni kitu cha muhimu pengine kuliko vyote kati ya vile ambavyo ntavitaja hapa. Hii nikwa kuwa afya inahusisha uzima wa mwili ambapo uzima wa mwili utakufanya ufanye kazi zako kwa ufanisi mkubwa sana sidhani kama ipo siku ambayo utaweza kufanya shughuli zako kwa kiwango kile ambacho huwa unafanya siku zote ikiwa unaumwa. Hivyo kwa kutambua umuhimu wa afya ya mwili wako basi hakikisha unafuata kanuni za kiafya kama vile kuhakikisha unafanya mazoezi, punguza kula vitu vyenye mafuta mengi, chumvi, sukari n.k. tunza afya ya mwili wako.
4. Muda, hapa ndio penye tatizo maana tumekuwa wapoteza muda wakubwa yaani ni watu ambao hatujui ni namna gani tutautumia muda wetu vizuri na kutufanya tuuone muda huo unatutosha sana lakini cha ajabu sasa matumizi mabovu ya muda yametufanya tuwe mabingwa wa kulalamika kuwa muda haututoshi, lakini wewe unaelalamika kumbuka kuwa mungu hana upendeleo katika jambo lolote lile maana kila mtu tajiri kwa masikini,kipofu kwa kiwete, mvuvi kwa mlinzi wote wanamasaa sawa ambayo ni ishirini na nne (24), sasa katika,masaa haya haya wapo wanaozitimiza ndoto zao na wanaoendelea kulalamika hivyo basi jambo la msingi kwako ni kupangilia mambo yako kwa muda uliopewa na sio kulalamika kuwa muda haukutoshi.
Hayo ni mambo muhimu manne ambayo ukiyafuatilia vyema utapata mafanikio makubwa kuliko unavyodhani.
Ni mimi rafiki yako,
Baraka Maganga.
Bmaganga22@gmail.com.
0754612413/0652612410.
Thursday, December 3, 2015
Hili Ndilo Kosa Ambalo Wengi Hulifanya.
Wednesday, December 2, 2015
Hii Sio Sababu Sahihi Ya Kutokufanikiwa Kwako.
Tuesday, December 1, 2015
Wafahamu Maadui Watano (5) Wa Mafanikio Yako.
Habari ya siku ndugu msomaji wa mtandao huu wa kona ya maarifa. Ni matumaini yangu kuwa hu mzima wa afya huku ukiwa mwenye hamasa na uliyejithatiti katika kuhakikisha kuwa unasonga mbele katika kuyatekeleza yale ambayo umekwisha kujiwekea kama malengo yako.
Leo tena tumekutana katika kuendelea kupeana mbinu na maarifa ambayo yatatufanya tuweze kuyafikia malengo yetu. Mara nyingi tumekuwa tukishindwa kutekeleza mipango yetu na pindi inapojitokeza hali hii huwa ni wepesi sana wa kuanza kutafuta sababu za kutokufanikiwa kwetu. Jambo baya ambalo tumekuwa tukilifanya ni kuangalia sababu za nje na kusahau sababu za ndani ambazo zimekuwa zikitupelekea kushindwa. Si ajabu kumkuta mtu kashindwa kwa ajili ya uvivu, uzembe, ukosefu wa hamasa kwake lakini anawageukia watu wengine na kuanza kuwashutumu kwa kushindwa kwake. Mara nyingi tabia hii ndio inayotufanya tusifanikiwe maana tunashindwa kugundua chanzo cha matatizo yetu ili tujirekebishe. Hapa nakuletea maadui watano wa mafanikio yako kama ifuatavyo:-
1) Kuiga watu, kuna watu wanapenda sana kuwaiga wenzao. Kuiga au kumwiga mtu ni ile hali ya kuchukua au kufanya jambo kwa namna ambayo mtu mwingine anaifanya aidha kwa ruhusa(ridhaa) yake au kwa kuiba.Najua wapo watakao ona kuwa nikama nawadaganya hivi naposema kuiga ni adui wa mafaniko yao. Nasema kuiga ni adui wa mafanikio kwa kuzingatia msingi mmoja tu wa uigaji au aina moja ya uigaji ambayo ni ule uigaji wa kuiba. Huu ndio umekuwa ukifanywa na watu wengi yaani ukiona mtu fulani anafanya jambo fulani basi nawe unaanza kulifanya. Mfano umemwona mtu fulani anafanya biashara fulani basi nawe unaanza kuifanya biashara hiyo pengine kichwani mwako umemwiga biashara hiyo ili tu uweze kumwaribia yeye. Nitoe sababu iliyonifanya niseme kuiga ni adui wa mafanikio yako, kuiga kutakuwa adui wa mafanikio yako kwa sababu uigaji unaoufanya unakupunguzia wewe ubunifu na kukufanya usiwe mbunifu bali mtu ambaye anasubiri kutafuniwa alafu yeye ameze kiulaini. Chunguza leo hii, biashara, kazi za maofisini zinasuasua kwa kuwa zimejaa waigaji ambao ubunifu wamekosa kabisa. Chakufanya sasa kama umeyapenda mafanikio ya mtu kajifunze kutoka kwake mwombe akuelekeze hapo utapata vitu Vingi tofauti na pale ambapo wewe unataka uwe unamvizia tu nakufanya mambo yako kama yeye.
2) Kukosa uvumilivu,kabla hujafanikiwa utakumbana na changamoto kadha wa kadha. Safari ya mafanikio imejaa mabonde, mito, milima na vikwazo vya namna mbalimbali atakaye weza kupambana na vikwazo hivi ndiye atakaye yafikia mafanikio. Mafanikio yanahitaji mipango ya muda mrefu je? Upo tayari kuandaa mpango wa miaka kumi mpaka ishirini na kuhakikisha kuwa unakaa nao kwa miaka yote hiyo. Hapa sizungumzii uvumilivu wa muda mchache nazungumzia uvumilivu wa muda mrefu. Uvumilivu ni jambo gumu sana miongoni mwetu, wachache sana ambao wanaweza kuvumilia ndio maana leo hii wengi wamekuwa wakijidanganya kuwa mafanikio yana njia ya mkato jambo ambalo ni gumu sana tena sana. Katika mafanikio hakuna njia ya mkato bali uvumilivu unatakiwa sana tena sana ili kuweza kuyafikia mafanikio husika.
3) Kuambatana na makundi mabovu, makundi kila mtu anayo lakini wangapi tunauhakika kuwa makundi yetu sio mabovu. Kama unataka kujua kundi lako ni bovu au la angalia nini unapata kutoka katika kundi hilo. Je kundi linakusaidia wewe katika kutimiza ndoto yako au malengo yako. Kama jibu ni hapana kwa swali hilo basi jua kuwa kundi hilo ni bovu na halikufai lakini kama jibu ni ndio basi kundi hilo ni bora kwako na endelea nalo. Naposema kundi namaanisha watu ambao umekuwa ukishirikiana nao katika mambo yenu mbalimbali. Watu hawa waweza kuwa marafiki, ndugu au wanajamii wenzako wengine tu.
4) Kukosa mipango, maisha sio kuishi tu bali maisha ni kuishi kwa mipango, usiishi tu kwa kuwa kila ukiamka unaliona jua likichomoza basi unaridhika tu na hali hiyo pia ukiona giza limeanza kutanda unaona ni wakati wa kulala sasa. Hayo sio maisha, maisha ni pale utakapo jihoji na kupata majibu kuwa pale jua litakapo chomoza utafanya nini maana kila tulionapo jua ndipo tunajua kuwa ni siku nyingine sasa weka mipango kuwa kwa kila uitwao leo utafanya nini. Usiishi tu kwasababu kuishi kupo bali ishi kwa sababu unataka kuishi.
5) kukosa midhamu, nidhamu ni ule uwezo au Hali ya kuweza kupanga mambo yako na kuweza kuyasimamia pasipo kushindwa kuyasimamia. Yaani kama ulipanga kufanya jambo fulani alafu ukashindwa kwa sababu zako za uongo na kweli jua dhahiri hauna nidhamu. Mafanikio yanahitaji nidhamu katika kuyatekeleza Yale ambayo umekwisha kujiwekea usiweke tu mipango alafu ukashindwa kuitekeleza. Pindi utakapoweka mipango alafu ukashondwa kuitekeleza huo ni ukosefu wa nidhamu. Ukosefu wa nidhamu utakurudisha nyuma sana katika kuyaelekea mafanikio. Na wengi wetu hatufanikiwi kwa kuwa tumekosa nidhamu yaani hatuwezi kuisimamia mipango yetu ipasavyo.
Mafanikio hayana njia ya mkato na usipende kutafuta sababu za nje za kutokufanikiwa kwako bali chunguza sana mambo yako ya ndani ambayo ndio kikwazo cha mafanikio.
Ni Mimi rafiki yako.
Baraka Maganga.
Bmaganga22@gmail.com
0754612413/0652612410.