Habari za wakati huu ndugu msomaji wa makala za mtandao
huu ni matumaini yangu kuwa hu mzima na unaendelea vyema mimi pia naendelea
vyema katika mapambano. Turudi katika mada yetu ya leo ambapo nataka kukushirikisha
juu ya jambo muhimu ambalo unatakiwa kuwa nalo kama kweli unataka kufanikiwa.
Jambo lenyewe ni kuhusu Kuendelea
kujifunza. Kama kweli unataka kufanikiwa hakikisha unajijengea tabia hii
kuanzia sasa.
Ipo nguvu kubwa sana katika kujifunza kama kweli unataka kuwa mwenye mafanikio basi
hakikisha kuwa unajifunza kila siku. Yaani usikae bila kujifunza katika kila
jambo ambalo unalifanya. Uwe mkulima, uwe daktari, uwe mwanafunzi, uwe hakimu
uwe nani wewe endelea kujifunza tu. Nakuambia hivyo kwa kuwa takwimu
zinaonyesha kuwa asilimia 40% ya watu wengi duniani huacha kujifunza pindi tu
wanapomaliza elimu zao yaa iwe sekondari au chuo, huo ndio huwa mwisho wa
kujifunza kwao. Sasa kwa wewe unayetaka kufanikiwa hakikisha kuwa haufanyi
makosa katika kujifunza.
1. Kupitia kusafiri,
unaweza kujifunza kupitia kusafiri, hii ni kutokana na sababu kuwa wanadamu
tunatofautiana kiutamaduni kwa kiasi kikubwa sana, hivyo katika kusafiri kutoka
sehemu moja kwenda kwingine kunaweza kukusaidia wewe kubadili maisha yako kwa kuwa utaweza kujifunza namna watu wanavyoishi na wanavyofanya vitu
tofauti tofauti, hivyo hii inaweza kukusaidia wewe katika kujifunza na hivyo
kubadili maisha yako. Unaweza kujifunza namna mpya ya kuendesha shughuli Fulani
kutokana na safari uliyosafiri, hii ni kutokana na sababu kuwa umebadilisha
mazingira ulikuwapo awali.
2. Kusoma vitabu,
unaweza kutafuta kitabu cha mada ambayo unaitaka vitabu vipo vingi sana swala
ni kwako wewe kuamua ni kitabu gani na kinachohusu nini unachotaka kusoma. Kuna
vitabu vya kusoma online, kuna vya kununua ambapo kampuni kama vile amazoni
zinauza vitabu vya kila namna, pia waweza kuingia google na ukasearch kitabu
unachotaka kuhusiana na mada unayotaka na hivyo basi ukapata kujifunza mengi
zaidi na zaidi.
Kusoma magazeti,
nakuona unasema magazeti dah, mbona yamejaa habari hasi, habari za kusikitisha,
habari za majonzi na simanzi na mengine mengi. Ni kweli kwa hayo unayoyasema
lakini sio kweli kuwa magazeti yamejaa mada hasi tu bali hata mada chanya zipo.
Kwenye magazeti kuna makala juu ya mambo
kama vile, afya, kilimo n.k. hivyo jambo la kufanya ni kuwa katika gazeti wewe
nunua gazeti na fuata taarifa chanya tu. Yaani fata kile ambacho unahisi
kimekufanya ununue gazeti, kama umenunua gazetiu kwa ajiri ya kusoma makala za
kilimo basi zitafute mahali zilipo kisha soma na achana na mengine.
4. Kusoma katika blog mbalimbali, hii
pia ni njia moja wapo na mabayo inakuwa kwa kasi sana ambayo wewe unayetaka
kufanikiwa unaweza kuitumia kwa kiasi kikubwa sana. Leo hii kuna blog nyingi
sana ambazo zinatoa mafunzo ya namna mbalimbali, sasa kazi ni kwako wewe kuamua
blog gani inakufaa kutokana na mada zake. Blog ni nyingi mno na zinatoa elimu
tofauti tofauti hivyo basi hakikisha kuwa unatafuta blog ya kukuwezesha wewe
kupata elimu unayota.
Maisha yanabadilika badilika kila siku
na pia utaratibu wa uzalishaji, usafirishaji na hata mawasiliano unabadilika
kila wakati hivyo ni bora uwe katika
hali ya kujifunza ili tu uwe katika nafasi nzuri ya kujifunza na hivyo kukabiliana na mabadiliko haya.
Mwandishi: Baraka Maganga.
Mawasiliano:-simu-0754612413/0652612410.
KARIBU KATIKA DARASA HURU.
Je?
unataka kujifunza na kuwa bora zaidi?,Je? unataka usihangamie kwa kukosa
maarifa?,Je? unataka kujua namna ya kutatua matatizo na changamoto mbalimbali
zinazokukabili?,Je? unakumbana na hali ya kukata tama mara kwa mara?,Je? unashindwa
kujiwekea malengo n.k.Kama
jibu ndio basi karibu katika darasa huru. Namna ya kujiunga na darasa huru
tuma kiasi cha pesa cha shilingi 5000/=
kwa namba 0754612413 kwa mpesa (jina.
Baraka magama) au 0652612410 kwa tigo pesa. (jina: Baraka maganga). Kiasi hiki
ni kwa mwezi mmoja ambapo ukiisha utatakiwa kuchangia tena kiasi hicho hicho. Kisha,
tuma namba yako ya simu kwenda namba moja kati ya hizo huku ukiwa
umeambatanisha na jina lako kamili kama linavyojitokeza katika m-pesa au tigo
pesa. Kumbuka kufanya hivyo huku ukiwa na uhakika kuwa pesa yako imepokelewa na
hapo utaunganishwa kwenye kundi la whatsapp ambalo litakuwa na jina la DARASA HURU.
N.B, huduma hii itatolewa kwa njia ya whatsapp, hivyo
hakikisha simu yako ina uwezo wa whatsapp ndipo ujiunge ili kuepuka usumbufu.Masomo yataanza tarehe 1/4/2016. Saa tatu
kamili usiku.
Barikiwa.
Karibu sana.