Friday, January 8, 2016

Mambo(7)Saba Muhimu Ya Kuepuka Ili Uweze Kufanikiwa.


Habari ndugu msomaji wa mtandao huu wa kona ya maarifa, ni matumaini yangu kuwa unaendelea vizuri katika kuhakikisha kuwa unashughulikia ipasavyo yale unayo yahangaikia ili tu kujiletea mafanikio ambayo ndio kila mtu anayoyahangaikia. Nami nikusihi kwa moyo mmoja kuwa endelea kupambana mpaka uyatimize yale unayoyaamini kama mafanikio kwako. Pambana pambana bila kuchoka na mafanikio utayaona tu.
Wakati unaendelea kupigana ili kuyasaka mafanikio yafuatayo ni mambo saba muhimu ambayo nataka uyaepuke kwa hali na mali kama kweli unataka kufanikiwa, ni muhimu ukayasoma mambo haya na kuyaweka akilini mwako ili yakusaidia katika safari yako ya kuelekea mafanikio, mambo hayo ni kama ifuatavyo:-


Epuka woga, ndugu mpendwa msomaji wa mtandao huu wa kona ya maarifa ni muhimu ukatambua kuwa woga ni adui wa mafanikio, woga utakukwamisha sana tena sana hivyo basi kama kweli unataka kufanikiwa acha kabisa kujenga woga juu ya yale mambo ambayo unayataka au unataka kuyafanya. Njia moja wapo ya kuepuka woga juu ya kitu fulani ni kwa wewe kufanya kile unachokiogopa zaidi na zaidi. Fanya kile unachokiogopa na woga utaushinda kwa hakika.

2.    Epuka wivu, wivu hauwezi kukupeleka popote, na kwa mtu anaetaka kufanikiwa wivu hatakiwi kuwa nao, kama kweli unataka kufanikiwa achana na habari zile za sijui wivu wa maendeleo sijui nini. Kitu ambacho unatakiwa ukijue ndugu msomaji ni kuwa wivu ni wivu tu achana na habari ya wivu wa maendeleo. Wivu utakuzuia kujifunza kutoka kwa wale waliofanikiwa hivyo basi pingana na habari hizi za wivu na badala yake acha kuwaonea wivu waliofanikiwa na nenda kajifunze kwao.


3.    Epuka chuki, mtu mwenye chuki hatofautiani sana na mtu mwenye chuki. Acha kujenga chuki na watu, usitegemee kufanikiwa ikiwa una chuki moyoni mwako. Chuki juu ya wenzio itakukwamisha maana chuki haina msingi wowote bali ni tabia ambayo ni maalumu na mashuhuri kwa watu ambao hawaelewi ni nini haswa wanakitaka maishani. Hivyo basi kama wewe unataka kufanikiwa basi achana na habari hizi za chuki.

4.    Epuka kisasi, je umekumbwa au unakumbwa na hali ya kisasi yaani unajisikia kulipiza kitu fulani yaani kwamba ukiona mtu fulanii kakufanyia kitu fulani nawe unataka uje ulipize hivyo hivyo. Haimaanishi kuwa mtu akikutendea mambo mabaya basi nawe uweze kumlipizia mabaya hayo hayo. Usipoteze muda wako katika kufikiria juu ya ni vipi ulipize kisasi kwa mwenzio bali tumia muda wako mwingi kuwaza utafanya nini ili uweze kufanikiwa.


5.    Epuka tamaa, achana na habari ya tamaa, tamaa haina msingi wowote kwako kama kweli unataka kufanikiwa. Tamaa ni kitu kibaya sana na ambacho hakiwezi kukufanya usonge mbele, usipende kutamani tamani vitu ovyo badala yake jua jinsi ya kujizuia juu ya matamanio yako. Usiwe mtu wa tamaa ambaye unataka kuwa ma kila kitu badala yake kuwa na vitu vya msingi sio lazima uwe navyo vyote. Hivyo basi achana na habari za tamaa.

6.    Epuka hasira, ikiwa unataka kufanikiwa ni vyema ukatambua kuwa hasira ni kitu kibaya sana. Ni kweli kuwa kila mtu anahasira na viwango vya hasira vinatofautiana kutoka mtu mmoja kwenda mtu mwingine. Nachotaka kukushauri ni kuwa jifunze kuzizuia hasira zako. Ikiwa unataka kufanikiwa jifunze kuanzia sasa kuweza kuzizuia hasira zako, hii itakusaidi wewe kuweza kufanya maamuzi yaliyo bora maana mara nyingi sana watu tumekuwa tukifanya maamuzi kutokana na hasira alafu baadae tunakuja kuanza kujuta, hii ni baada ya hasira yetu kuisha. Hivyo basi jifuze kuzizuia hasira zako.


7.    Epuka ushirikina, wapo watu ambao huamini kuwa mafanikio huja kwa kuwa mshirikina, naomba nikuambie kuwa haya ni mawazo ya kijinga na yasiyofaa katika ulimwengu wa sasa. Kama kweli unataka kufanikiwa acha kabisa kutegemea habari za ushirikina.

Hayo ni mambo saba muhimu ambayo inabidi uyaepuke ili uweze kufanikiwa. Epuka mambo haya kwa kuwa hayana msingi wowote na wala hayawezi kukufikisha popote. Hivyo ndugu msomaji pigana uwezavyo kuyaepuka mambo haya.


Ni mimi rafiki yako,
Baraka Maganga
Wasiliana nami kwa.
 Simu: 0754612413 au 0652612410.
Barua pepe: Bmaganga22@gmail.com


No comments:

Post a Comment