Tuesday, June 28, 2016

Mambo Matano (5)Muhimu Ya Kukusaidia Katika Kukuza Biashara Yako.


Habari ya wakati huu ndugu msomaji wa makala za mtandao huu, ni matumaini yangu kuwa hu mzima na unaendelea vyema katika kupambana ili kuboresha maisha yako. Karibu tujifunze kwa pamoja mambo matano ya kutusaidia katika kukuza biashara zetu.



Ubora wa huduma yako, hapa tunahusisha kiwango cha utoaji wa huduma yako kama ni katika mgahawa mfano tunazingatia vitu kama vile usafi wa mahali husika na mwonekano kwa ujumla,ikiwa ni pamoja na mpangilio wa vitu. Kama ni duka jambo la kuzingatia ni mpangilio wa bidhaa zako zimekaaje kaaje, kama ni baa je mwonekano ukoje na mpangilio wa viti na namna ya kukaa ukoje, vile vile swala la usalama lazima lizingatiwe hapo. Maswala kama vile ukalimu kwa wateja, mwonekano wa wahudumu au wafanyakazi kama utakuwa nao ni muhimu sana na yote haya yanakuwa katika kipengele cha ubora wa huduma yako. Hivyo hakikisha unazingatia swala hili.

2.       Ubora wa bidhaa zako, hapa tunaangalia licha ya kuwa na huduma nzuri je? Kile unachouza au kutoa kama huduma kwa wateja wako kina ubora gani kwa wateja wako?. Ni muhimu sana kuuza bidhaa zenye ubora kama unataka kuwa mfanyabiashara mkubwa na mwenye kuheshimika na kupendwa na watu. Epuka uuzaji wa bidhaa feki au zilizokwisha muda wake maana hili halitakusaidia daima bali siku ikigundulika ndio kutakuwa kufirisika kwako kwa moja kwa moja na kumbuka muda mwingine unaweza kusababisha madhara makubwa kwa watumiaji, mfano kwa wale wauzaji wa bidhaa ambazo ni chakula au zinatumika moja kwa moja kwa binadamu kama chakula au madawa zaweza kusababisha madhara au hata kifo/vifo hivyo kwa wewe muuzaji zaweza kukusababishia hata kifungo cha kudumu jera.


3.       Matumizi ya lugha, je ni lugha gani unatumia kwa wateja wako?, nakusihi jifunze lugha ya biashara usiwe mtu wa kuongea na wateja kwa kuwafokea au ni kama unawalazimisha badala yake ongea na mteja ni kama unamnyenyekea vile au kumbembeleza. Kuwa na lugha ya maelewano na wateja hii itakusaidia kwa kiasi kikubwa sana. Jifunze kumsikiliza mteja hata pale unapohisi kakukosea au kakudharau wewe jifanye ni kama huelewi hivi swala tu usipoteze wateja kwa jambo dogo ambalo ungeweza kulizuia kwa kukaa kimya tu.

4.       Ogopa kukosa chenji, wafanyabiashara wengi sana sasa wamekuwa na mtindo ambao binafsi nauita ni utaratibu mbovu sana, nao ni ule wa chenji utaijia baadae au muda mwingine anakuambia chenji sina. Naomba niseme hii tabia inakera sana unakuta mtu ni dereva bodaboda kakubeba saa sita za usiku au saa kumi na moja alfajiri unamlipa labda unampatia shilingi elfu kumi anakuambia hana chenji, ukimwambia tunafanyaje unasikia niachie ila yeye ukimwambia sikulipi utasikia aa mafuta gharama sijui hesabu ya bosi maneno mengi sana. Ngoja nikuambie kitu wakati mwingine jifunze kutafuta chenji kabla hujafungua au kuanza biashara yako kama uko karibu na benki nenda hata benki ukatafute chenji hii itakusaidia maana wateja hawapendi mfanyabiashara mbabaishaji. Pia hii itakusaidia katika ushindani maana ambae atakosa chenji siku hiyo kama mteja akikukariri hawezi rudi tena siku nyingine.Wewe mwenye duka acha maswala ya kusema chenji baadae sijui kesho kama mtu anamatumizi mengine?
5.       Usikopeshe ili kuonekana mwema, hii itakusaidia kulinda mtaji wako maana kuna mtu au watu unaweza kuwakopesha bidhaa za pesa nyingi kiasi kwamba inafika wakati sasa hauwezi hata kuongeza bidhaa katika biashara yako hii inakuwa hatari, badala yake kuwa na mipaka ya kukopesha na ili kukusaidia kopesha faida tu ambayo hata ikichelewa kurudi mtaji utakuwepo wa kununua bidhaa za kiwango kile kile. Hii itakusaidia kulinda mtaji wako. Hivyo kamwe usikopeshe ili kuonekana mwema machoni pa watu au ili uonekane mfanyabiashara mwema wakati inakuumiza maana biashara yako hapo haiwezi kuendelea.

Nakutakia kila la kheri katika kuboresha biashara yako au kuanzisha biashara yako.

Kama bado hujajipatie kitabu cha safari ya kuelekea mafanikio basi hakikisha hukikosi. Namna ya kukipata tuma meseji yenye neno kitabu kwenda namba 0754612413 kwa njia ya telegram, au whatsapp(hakikisha whatsapp unayotumia ni new version inayosupport kutuma na kupokea document kama pdf n.k kama sio ingia play store ili kuiupdate) au pia kwa njia ya email ambayo ni Bmaganga22@gmail.com.

Rafiki yako,
Baraka Maganga
Mawasiliano: 0754612413 au 0652612410. Au barua pepe-Bmaganga22@gmail.com.


No comments:

Post a Comment