Monday, May 2, 2016

Njia Za Kukufanya Ubaki Mwenye Hamasa Muda Wote.

Habari za wakati huu ndugu msomaji wa Makala za mtandao huu, ni matumaini yangu kuwa hu mzima na unaendelea vizuri katika kuhakikisha kuwa unapambana na hatimae kujiletea matokeo bora ambayo ndiyo umekuwa ukiyapigania kila siku, kila wakati na kila dakika. Nami nikusihi pambana bila kuchoka hata siku maana maisha ni mapambano na wale wanaovumilia ndio hupata mema.


Wakati ukiwa unapambana nataka nikusisitize na nikuelekeze juu ya jambo moja nalo ni jambo ambalo limekuwa likitukumba na kutusumbua sana tulio wengi hapa duniani. Jambo lenyewe ni kuwa na hamasa ya muda mfupi, tumekuwa tukikumbwa na hali hii ya kuwa na hamasa ya muda mfupi. Yaani ni watu ambao tumekuwa tukihamasika kwa muda mchache alafu baadae tunajikuta tumerudi kule kule tulikotoka mwanzo yaani ile hamasa haipo tena. Pengine jambo hili limekuwa likitufanya tushindwe kufanikiwa kwa muda mrefu na laweza kuwa likisababishwa na mambo kadha wa kadha.
Ni mara ngapi umekuwa ukitamani sana kufanya jambo fulani baada ya kutoka katika semina fulani, baada ya kusoma kitabu fulani au baada ya kusikiliza historia ya mtu fulani mwenye mafanikio, au pengine ni mara ngapi umekuwa ukipata hamasa baada ya kusikiliza mahubiri au mafunzo ya dini lakini baada ya muda mfupi unakuta hamasa ile imetoweka kama unakumbwa na tatizo hilo basi karibu nikupe njia nne za kukufanya ubaki na hamasa muda wote.
1.    Jifunze kitu kipya kila siku, njia ya kwanza ya kukufanya ubaki na hamsa kila siku, kila wakati na kila dakika ni kwa wewe kuhakikisha kuwa kila siku unajifunza kitu kipya. Hakikisha toka unaanza siku mpaka umeimaliza umejifunza kitu fulani, iwe katika biashara, mapishi, kilimo, ufugaji n.k swala wewe hakikisha umejifunza kitu ambacho mwisho wa siku kitakufanya uweze kutimiza ndoto zako.

2.    Fanyia kazi yale unayojifunza, njia ya pili ya kukufanya ubaki kuwa na hamasa ni kuhakikisha kuwa unayafanyia kazi yale unayojifunza maana yale mambo kwa namna moja au nyingine ndiyo yaletayo hamsa kwako hivyo basi hakikisha unayafanyia kazi. Wengi wetu tumekuwa tukikabiliwa na hali ya kuwa na hamasa ya muda mfupi kwa sababu hatutaki kuyafanyia kazi yale ambayo tumejifunza. Hakikisha unafanyia kazi yale uliyojifunza achana na habari za nitaanza kesho.


3.    Epuka visingizio, visingizio ni njia ambayo watu wengi sana huwa tunaitumia kama sababu za kutufanya tusiweze kufanikisha jambo fulani. Naomba nikionye kuwa epuka visingizio maana havina msaada wowote kwako. Kama unataka kubaki na hamasa muda wote epuka zile kauli za sijui nina umri mkubwa au mdogo, nitafanya kesho, sijasoma, mimi ni mtoto wa kijijini/town n.k. hakikisha unaviepuka kwa kiasi kikubwa ili ubakie na hamasa yako.

4.    Kuwa mvumilivu, usiwe mtu wa kutaka mambo yafanyike hapo hapo na yatokee hapo hapo, bali jua kuwa utokeaji wa mambo huwa unatofautiana kwa kiasi kikubwa sana. Yaani kuna mambo yanahitaji muda mrefu ili yaweze kutokea na kuna mambo yanhitaji muda mfupi ili yaweze kutokea. Sasa msisistizo wangu upo katika yale mambo ambayo yanahitaji muda ili kutokea maana haya ndio huondoa hamasa, hivyo basi kwa yale mambo ambayo yanahitaji muda ili kutokea hakikisha unakuwa mvumilivu. Hiindio njia pekee itakayokufanya ubakie na hamasa katika mambo ya aina hiyo.

Rafiki yako
Baraka Maganga
Mawasiliano: 0754612413/0652612410.
Barua pepe: Bmaganga22@gmail.com.


JE? Unataka kujifunza Zaidi na Zaidi ili kuwa bora katika maisha yako? Basi hakikisha haukosi kitabu cha SAFARI YA KUELEKEA MAFANIKIO. Hiki ni kitabu ambacho kinapatikana bure kabisa yaani bila gharama yoyote ile. JINSI YA KUKIPATA, tuma ujumbe wenye neno kitabu katika whatsapp katika moja ya namba hizo hapo juu. Au tuma ujumbe katika TELEGRAM kwenda namba 0754612413. Au tuma barua pepe(email) yenye jina kitabu kwenda email niliyoionyesha hapo juu, kisha utatumiwa kitabu bure kabisa.

No comments:

Post a Comment