Wednesday, February 24, 2016

Yatathimini Matumizi Yako Ya Pesa Kwa Umakini Kabla Hujasema Tatizo Mtaji




Habari za wakati huu ndugu mpendwa msomaji wa makala za mtandao huu, ni matumaini yangu kuwa hu mzima na unaendelea vizuri sana katika kutekeleza majukumu yako ya hapa na pale, ni muhimu uendelee kufanya hivyo kwani mapambano yanaendelea kwa kiasi kikubwa sana hivyo jambo la msingi ni kuyaendeleza mapambano hayo kwa kasi ya ajabu ili kuweza kuyatekeleza yale ambayo ni ya msingi na ambayo kwa upande mwingine ndiyo tumekuwa tukiyataka maishani.

Wakati ukiendelea kupambana ndugu mpendwa msomaji wa makala hii hebu kwa dakika moja tu fikiria juu ya matumizi yako. Naposema matumizi najua nakuwa na eleweka kwa kiasi kikubwa tu, matumizi nayo yazungumzia hapa ni matumizi ya pesa. Nilipenda kichwa cha makala ya leo kiwe mtaji sio tatizo lakini nimeamua kukiweka  kama kilivyo kwa kuwa ntakacholenga kukisema kitakuwa na uhusiano tu na mtaji. Tumekuwa ni watu wa kulalamika sana juu ya mitaji, sana tena sana. Lakini leo hii naomba tujadili na tuweze kuelewana kuwa mtaji sio tatizo bali ni vichwa vyetu ndivyo vyenye matatizo. Hapa leo naongea na wafanyakazi uwe mfanyakazi wa serikali au shirika binafsi naongea na wewe hapa leo.

Kwanini nataka niongee na wafanyakazi kwa kiasi kikubwa ni kwa sababu ya vituko vya wafanyakazi, kila mtu leo hii anaamini kuwa wafanyakazi mishahara yao haiwatoshi kwa kuwa wao ni walalamikaji wakubwa kuwa mishahara haiwatoshi. Lakini mimi nataka kusema kuwa mishahara inawatosha. Tutoke huko maana sio lengo la makala. Lengo la makala ni kutaka kuonyesha kuwa mtaji sio tatizo kwa kupitia kuchunguza matumizi yetu ya pesa tunazozipata kama mshahara wa shughuli zetu.

Wakati nikiwa kidato cha sita miaka michache huko nyuma nilijifunza kutoka katika kitabu cha rich dad poor dad cha bw. Kiyosaki tofauti kati ya asset na liabilities.  Kwa mujibu wa kiyosaki anafafanua assets kama kitu ambacho kinachoingiza pesa mfukoni ili hali liabilities ni kitu ambacho kinatoa pesa mfukoni. Hapo hapo rudi katika kichwa cha makala, tathimini matumizi ya pesa zako, wewe pesa zako unazitumia katika nini, je ni asset au liabilities? Jijibu mwenyewe. Kiyosaki aliendelea kusema kama unataka kuwa tajiri nunua assets na kama unataka kuwa masikini nunua liabilities. Hapo hapo turudi kwako huwa unanunua nini?. Rudi nyuma tena jiulize kwanini mpaka leo hauna mtaji wa kuanza biashara au jambo jingine tofauti na kazi yako hiyo. Tatizo mtajii eehe wenzio waliupataje huo mtaji sasa?. Aya nakuambia hivi tatizo sio mtaji tatizo ni akili yako hiyo. Kama unataka kujua kama mshaara wako unaweza kukupatia mtaji chunguza matumizi yako ya pesa. Unatumia pesa nyingi sana kwenye liabilities ndio maana hauna mtaji. Kama unabisha sawa ila huo ndio ukweli na ukweli utabaki kuwa ukweli.

Wafanyakazi wengi wanamtindo wa kununua vikolokolo ndio maana hawapati mitaji, . naposema vikolokolo namaanisha kuwa vitu visivyo na tija wala umuhimu bali katika hali ya kutaka kuuridhisha moyo, mwili au wenzio. wewe huyo kila aina ya simu unataka uwe nayo, baba/mama utaweza kushindana wa wachina kila siku wako na matoleo mapya. Kila uzinduzi wa albamu unataka uende, kila tamasha la muziki wewe humo, kila fashioni mpya ya nguo humo, kila mkopo unataka ukope alafu mkopo huo unataka ukanunue pikipiki ya kuendea kazini. Pikipiki itakudai mafuta alafu utajikuta huna pesa. Kwa matuzimi ya namna hii kweli mshahara haukutoshi na hauwezi kupata mtaji. Lakini ukipunguza mfano ukawa na simu hata teckno p5 inatosha mbona nayo utaingia fb, whatsapp na instrgram, pia makala zangu utasoma sasa yanini bwebwe nyingi za masimu kibao.

Ni muhimu kupendeza kimavazi lakini sio muhimu kuwa na kila aina ya vazi. Ni muhimu kuwa na pikipiki lakini ujue ni assets au liabilites. Ni muhimu kuuzulia matamasha na uzinduzi wa albamu za wasanii uwapendao lakini sio wote. Jiulize kama kwa mwezi unatumia shilingi laki mbili kutoka katika mshahara wako katika liabilities, ukiachana nazo mara mwaka utakuwa hujapata mtaji wewe au unaleta habari gani hapa. Chemsha kichwa sio kulalama tu. Think beyond.

Uwezo wa kupata mtaji kupitia mishahara yetu tunayo sema shida ni akili zetu na vichwa vyetu. Unakopa mkopo unanunua jiko la gesi, sijui sofa, sijui sabufa usiposikiliza mziki utakufa simu yako haina mziki? Kuwa na nidhamu na pesa vinginevyo utaishia kulalamika mpaka siku yesu anarudi.

“If you want to be rich buy assets” ROBERT KIYOSAKI.
“Mtaji sio tatizo tatizo ni vichwa vyetu”.
Je unataka kujipatia kitabu cha Robert kiyosaki ili kujifunza zaidi na zaidi usiwe na shaka.nitumie email kupitia email yangu ya hapo chini na neno, “nataka kitabu cha rich 
dad poor dad” nami ntakutumia.

Ni mimi rafiki yako,
Baraka Maganga.
Wasiliana nami kwa nambari za simu 0754612413/0654612410 au kwa barua pepe:- Bmaganga22@gmail.com.



Tuesday, February 23, 2016

Utavuna Ulichopanda Na Huto Vuna Usichopanda.




Habari za wakati huu ndugu mpenzi msomaji wa makala za mtandao huu, mtandao ambao umelenga kukupatia maarifa ambayo ukiyatumia huta kaa ujute kwanini uliamua kujiunga na mtandao huu ili uwe unasoma makala zake. Ni matumaini yangu kuwa unaendelea vizuri sana katika mapambano nami nasema mapambano yanaendelea na yataendelea.

Ukipanda mahindi utavuna mahindi.
Ukipanda mtama utavuna mtama
Ukipanda matikiti utavuna matikiti.
Usipopanda maharage hutovuna vuna maharage.
Usipopanda mti hutovuna  mti.
Usipopanda alizeti hutovuna alizeti.

Nimeweka kauli hizo hapo juu lengo sio kukuchosha au kukutaka uzisome tu na kuishia kuzishangaa hapana lengo la kuziweka kauli hizo hapo juu ni kutaka uweze kunielewa toka mwako ambacho nakimaanisha maana hapa nataka tuelewane kiurahisi zaidi pengine kuliko siku zote ndugu msomaji wa makala hii. Kama kichwa kisemavyo kuwa utavuna ulichopanda na hutovuna usichokipanda. Hivi nikikuuliza ndugu msomaji wa makala hii kuwa uonapo kauli hii unajifikiria nini juu ya maisha yako. Yaani unaonaje juu ya matokeo uyapatayo kutokana na shughuli zako?. Na uionapo kauli hii unahusianisha vipi na ulalamishi au ulalamikaji wa watanzania wa leo. Binafsi naamini kuwa kama watanzania tungekuwa wenye kuielewa kauli hii vizuri basi leo hii kusingalikuwa na mtanzania anayekaa na kuanza kuilaumu serikali, wazazi, ndugu au walezi wake kuwa wao ndio chanzo cha yeye kuto kufanikiwa. Kwanini nasema hivyo mimi nasema hivyo kutokana na kauli ilivyo.

Kauli inasema utavuna ulichopanda. Kwahiyo ukipanda ulalamishi utavuna ulalamishi kwahiyo ni kuwa ukimlaumu mtu nae atakulaumu au nawewe utalaumiwa na wengine. Kauli inasema utavuna ulichopanda na hautovuna usichopanda hakuna sehemu ambayo imesema utavuna ulichopandiwa na hautovuna ulichopandiwa hapa naweza kusema kauli hii haitambui jambo linaloitwa utegemezi hivyo basi kama vijana wangekuwa wanaielewa vyema kauli hii wangeacha maswala ya kuwategemea wazazi wao kwa kila kitu badala yake wangeanza kupanda mbegu Fulani ambazo zingeweza kuwazalia matunda Fulani ambayo kwa siku za baadae zingewaletea matokeo mazuri.

Kauli hii pia inatukumbusha juu ya uwajibikaji nikiisoma kauli hii nakumbuka juu ya uwajibikaji kuwa kila mtu anapaswa kuwajibika kwa mafanikio yake na sio kumtegemea mtu akuletee mafanikio. Huwa tunakwepa majukumu yetu kwa kiasi kikubwa sana, sasa kauli hii inatukumbusha juu ya uwajibikaji juu ya maisha yetu. Utavuna ulichopanda maana yake unahusikia moja kwa moja juu ya matokeo uyapatayo maishani. Kama wewe ni masikini mpaka sasa tambua kuwa umepanda mbegu za umasikini na ndio maana uko masikini mpaka leo. Hakuna mtu anayehusika na umasikini wako bali ni wewe mwenyewe ndiye unayehusika nao maana ni mbegu ambazo umepanda wewe mwenyewe bila kumhusisha mtu mwingine hivyo basi unawajibika kwa umasikini wako na sio vinginevyo.

Kauli hii inanikumbusha juu ya ubora wa mbegu zetu yaani kama unataka kupata matokeo bora  ni wakati sasa wa kupanda mbegu bora, maana si utavuna ulichopanda maana yake ni kuwa mbegu bora huzaa mbegu bora  na mbaya huzaa mbaya nyenziye. Hivyo basi panda mbegu bora maana ndiyo ikufahayo.

Maishani tumekuwa tukikumbwa na mambo mengi sana na tumekuwa watu wa kuwasakizia wengine kuwa ndio wahusika wa mambo hayo yanayotutokea hata kama ni kwa kuwasingizia lakini huwa tunataka kuuaminisha umma kuwa hali zetu mbaya ni matokeo ya watu au vitu fulani kumbe tunakuwa tunajidanganya sasa jambo la msingi hapa ni kuwa kwa kuwa umegundua kuwa utavuna ulichopanda hata ikitokea watu wanakushawishi uanze kulalamika juu ya jambo fulani we achana nao maana ukweli wa mambo ushaujua.
Uvivu huzaa uvivu.
Lawama huzaa lawama.
Visingizio huzaa vizingizio.
Tamaa huzaa tamaa.n.k

Ni mimi rafiki yako,
Baraka Maganga.
Wasiliana nami kwa nambari za simu 0754612413/0654612410 au kwa barua pepe:- Bmaganga22@gmail.com.


Monday, February 22, 2016

Fanya Kitu Hiki Na Utafanikiwa Tu




Habari za wakati huu ndugu msomaji wa makala za mtandao huu, ni matumaini yangu kuwa hu mzima na unaendelea vizuri katika kupambana

Tuesday, February 16, 2016

Usifanye Kwa Kuwa Umeona Wanafanya.







Umekuwa ukitaka kufanya jambo au mambo mbalimbali maishani au umekuwa ukitaka kufanya mambo mbalimbali. Lakini wakati

Monday, February 15, 2016

Jifunze Na Jua Kwamba Kuna Muda Unatakiwa Kusema Hapana.


Habari za wakati huu ndugu mpendwa msomaji wa makala za mtandao huu, ni matumaini yangu kuwa hu mzima wa afya na unaendelea vizuri

Saturday, February 13, 2016

Mambo Sita (6) Ambayo Sio Msaada Katika Kutatua Changamoto Zetu Lakini Tunayafanya.


Maisha ni mapambano, ni mapambano dhidi ya changamoto ambazo huibuka kila leo na hatuna budi kuweza kukabiliana na changamoto husika

Friday, February 12, 2016

Watu Sahihi, Taarifa Sahihi Tunaenda Mbele.


Kumekuwa na tatizo moja kwa sasa ambalo limekuwa likitusumbua kwa kiasi kikubwa sana na tatizo hili limekuwa likitugharimu wengi sana na kujikuta

Thursday, February 11, 2016

Usiishi Ni Kama Hakuna Maisha Tena.


Katika maisha yetu sisi wanadamu tumekuwa tukiishi na watu wa aina tofauti tofauti kitabia, kimaumbile na kihali mbalimbali. Yote haya ni maisha tu

Wednesday, February 10, 2016

Fahamu Kuwa Kila Kitu Huanza Na Wewe.

Habari za wakati huu ndugu mpendwa msomaji wa makala za mtandao huu. Ni matumaini yangu kuwa hu mzima na unaednelea vizuri katika

Thursday, February 4, 2016

Sababu Za Kwanini Unapaswa Kuwa Mwaminifu.

Habari za wakati huu ndugu msomaji wa mtandao huu wa kona ya maarifa, ni matuimaini yangu kuwa hu mzima wa afya na unaendelea

Wednesday, February 3, 2016

Njia Tano Za Kukuwezesha Kuwa Na Hali Ya Kuendelea Kutenda.

Mara nyingi sana tumekuwa watu wenye kukosa hali ya kuendelea kutaka kufanya mambo ambayo tumekuwa tukitaka kuyafanya. Ukosefu wa hali hii ndiyo ambayo

Tuesday, February 2, 2016

Sababu Tisa (9) Zinazofanya Watu Wengi Kushindwa Maishani.

Mara nyingi sana tumekuwa ni watu wa kujaribu hili na lile katika ile hali ya kutaka pengine kujikwamua kutoka katika hali ngumu za kimaisha tulizokuwa nazo,

Monday, February 1, 2016

Usitishike Na Watakao Kupinga Kwa Kigezo Hiki.

Habari za wakati huu ndugu msomaji wa mtandao huu wa kona ya maarifa ni matumani yangu kuwa hu mzima na unaendelea vizuri katika kupambana