Habari za wakati huu ndugu mpendwa msomaji wa makala za mtandao
huu, ni matumaini yangu kuwa hu mzima na unaendelea vizuri sana katika
kutekeleza majukumu yako ya hapa na pale, ni muhimu uendelee kufanya hivyo kwani
mapambano yanaendelea kwa kiasi kikubwa sana hivyo jambo la msingi ni
kuyaendeleza mapambano hayo kwa kasi ya ajabu ili kuweza kuyatekeleza yale
ambayo ni ya msingi na ambayo kwa upande mwingine ndiyo tumekuwa tukiyataka
maishani.
Wakati ukiendelea kupambana ndugu mpendwa msomaji wa
makala hii hebu kwa dakika moja tu fikiria juu ya matumizi yako. Naposema
matumizi najua nakuwa na eleweka kwa kiasi kikubwa tu, matumizi nayo
yazungumzia hapa ni matumizi ya pesa. Nilipenda kichwa cha makala ya leo kiwe
mtaji sio tatizo lakini nimeamua kukiweka
kama kilivyo kwa kuwa ntakacholenga kukisema kitakuwa na uhusiano tu na
mtaji. Tumekuwa ni watu wa kulalamika sana juu ya mitaji, sana tena sana.
Lakini leo hii naomba tujadili na tuweze kuelewana kuwa mtaji sio tatizo bali
ni vichwa vyetu ndivyo vyenye matatizo. Hapa leo naongea na wafanyakazi uwe
mfanyakazi wa serikali au shirika binafsi naongea na wewe hapa leo.
Kwanini nataka niongee na wafanyakazi kwa kiasi kikubwa
ni kwa sababu ya vituko vya wafanyakazi, kila mtu leo hii anaamini kuwa
wafanyakazi mishahara yao haiwatoshi kwa kuwa wao ni walalamikaji wakubwa kuwa
mishahara haiwatoshi. Lakini mimi nataka kusema kuwa mishahara inawatosha.
Tutoke huko maana sio lengo la makala. Lengo la makala ni kutaka kuonyesha kuwa
mtaji sio tatizo kwa kupitia kuchunguza matumizi yetu ya pesa tunazozipata kama
mshahara wa shughuli zetu.
Wakati nikiwa kidato cha sita miaka michache huko nyuma
nilijifunza kutoka katika kitabu cha
rich dad poor dad cha bw. Kiyosaki tofauti kati ya asset na
liabilities. Kwa mujibu wa kiyosaki
anafafanua assets kama kitu ambacho kinachoingiza pesa mfukoni ili hali
liabilities ni kitu ambacho kinatoa pesa mfukoni. Hapo hapo rudi katika kichwa
cha makala, tathimini matumizi ya pesa zako, wewe pesa zako unazitumia katika
nini, je ni asset au liabilities? Jijibu mwenyewe. Kiyosaki aliendelea kusema
kama unataka kuwa tajiri nunua assets na kama unataka kuwa masikini nunua
liabilities. Hapo hapo turudi kwako huwa unanunua nini?. Rudi nyuma tena
jiulize kwanini mpaka leo hauna mtaji wa kuanza biashara au jambo jingine
tofauti na kazi yako hiyo. Tatizo mtajii eehe wenzio waliupataje huo mtaji sasa?.
Aya nakuambia hivi tatizo sio mtaji tatizo ni akili yako hiyo. Kama unataka
kujua kama mshaara wako unaweza kukupatia mtaji chunguza matumizi yako ya pesa.
Unatumia pesa nyingi sana kwenye liabilities ndio maana hauna mtaji. Kama
unabisha sawa ila huo ndio ukweli na ukweli utabaki kuwa ukweli.
Wafanyakazi wengi wanamtindo wa kununua vikolokolo ndio
maana hawapati mitaji, . naposema vikolokolo namaanisha kuwa vitu visivyo na
tija wala umuhimu bali katika hali ya kutaka kuuridhisha moyo, mwili au wenzio.
wewe huyo kila aina ya simu unataka uwe nayo, baba/mama utaweza kushindana wa
wachina kila siku wako na matoleo mapya. Kila uzinduzi wa albamu unataka uende,
kila tamasha la muziki wewe humo, kila fashioni mpya ya nguo humo, kila mkopo
unataka ukope alafu mkopo huo unataka ukanunue pikipiki ya kuendea kazini.
Pikipiki itakudai mafuta alafu utajikuta huna pesa. Kwa matuzimi ya namna hii
kweli mshahara haukutoshi na hauwezi kupata mtaji. Lakini ukipunguza mfano
ukawa na simu hata teckno p5 inatosha mbona nayo utaingia fb, whatsapp na
instrgram, pia makala zangu utasoma sasa yanini bwebwe nyingi za masimu kibao.
Ni muhimu kupendeza kimavazi lakini sio muhimu kuwa na
kila aina ya vazi. Ni muhimu kuwa na pikipiki lakini ujue ni assets au
liabilites. Ni muhimu kuuzulia matamasha na uzinduzi wa albamu za wasanii
uwapendao lakini sio wote. Jiulize kama kwa mwezi unatumia shilingi laki mbili
kutoka katika mshahara wako katika liabilities, ukiachana nazo mara mwaka
utakuwa hujapata mtaji wewe au unaleta habari gani hapa. Chemsha kichwa sio
kulalama tu. Think beyond.
Uwezo wa kupata mtaji kupitia mishahara yetu tunayo sema
shida ni akili zetu na vichwa vyetu. Unakopa mkopo unanunua jiko la gesi, sijui
sofa, sijui sabufa usiposikiliza mziki utakufa simu yako haina mziki? Kuwa na
nidhamu na pesa vinginevyo utaishia kulalamika mpaka siku yesu anarudi.
“If you want to be rich buy
assets” ROBERT KIYOSAKI.
“Mtaji sio tatizo tatizo ni
vichwa vyetu”.
Je unataka kujipatia kitabu
cha Robert kiyosaki ili kujifunza zaidi na zaidi usiwe na shaka.nitumie email
kupitia email yangu ya hapo chini na neno, “nataka kitabu cha rich
dad poor
dad” nami ntakutumia.
Ni mimi rafiki yako,
Baraka Maganga.
Wasiliana nami kwa nambari za simu 0754612413/0654612410 au kwa barua pepe:- Bmaganga22@gmail.com.