Habari za wakati huu ndugu msomaji wa mtandao huu wa
kona ya maarifa. Kama ilivyokawaida kila tunapokutana hapa huwa tunakutana kwa
lengo la kupeana maarifa mapya ambayo yatatusaidia na baadae kutuletea
mafanikio.
Baadhi tumekuwa
tukiamini kuwa njia bora ya kujifunza ni ya
sisi kwenda shuleni kisha mwalimu anakuja anasimama mbele yetu na kuanza
kutufundisha mambo mbalimbali. Wengi tunaamini kujifunza kupo shuleni tu.
Kujifunza kwa njia ya shule ni njia ya hasili na njia hii hutufanya wakati
mwingine tukose uelewa wa mambo ya msingi kuhusu maisha. Chukulia mfano wewe
unaetegemea elimu ya kutoka shuleni utajifunzaje elimu kuhusu pesa maana
shuleni hakuna somo la pesa. Sasa kama jibu ni huwezi kujifunza elimu ya pesa
kutoka shuleni basi zijue njia nyingine zifuatazo ambazo zitakusaidi kujifunza
mambo mengi sana tofauti na yale ya shuleni.
1. Kutazama, hii ni njia mojawapo ya
kujifunza mambo mengi sana na jambo la kushangaza ni kwamba njia hii ni rahisi
na haina gharama kubwa sana lakini ndio njia ambayo haitumiki na wengi.Njia hii
ni nzuri sana maana inahusisha kutazama shughuli aifanyayo mtu Fulani kisha
ukajifunza jambo. Mfano unaweza kumtazama fundi selemala jinsi anavyounganisha
mbao mpaka kupata mlango hivyo ukawa umejifunza jambo Fulani na taratibu
ukilifanyia kazi utajikuta nawe unauwezo wa kuunganisha mbao na kupata mlango
kama alivyokuwa akifanya selemala uliyekuwa unamtazama. Hivyo basi jifunze
kupitia njia ya kutazama.
2. Kusoma vitabu, vitabu vinasiri nyingi
sana kuliko wengi wetu tunavyofikiri. Vitabu hivi daima huwa vinaandikwa na
wataalamu na watu waliofanikiwa kimaisha ambapo huandika kwa lengo ya kufunza
kuhamasisha, na kutia motisha maishani. Lakini kitabu cha kwanza katika
kuhamasisha ni biblia kwa wakristo na kwa waislamu ni kuruani. Vitabu vimejaa
mambo mengi ambayo huwezi kuyapata shuleni kama unavyotegemea, vitabu vimejaaa
historia za watu waliofanikiwa, changamoto zao, maisha yao mpaka kufanikiwa na
baada ya kufanikiwa. Pia kuna vitabu ambavyo vimejaaa elimu kuhusu pesa mfano
wa kitabu hicho ni kitabu cha rich dad poor dad cha bwana Robert
kiyosaki. Hivyo basi jenga utamaduni wa kujisomea angalau kitabu kimoja
kwa wiki.
3. Video, Leo hii unaweza kujifunza mambo
mbalimbali kupitia video za wataalamu mbalimbali. Leo hii kutokana na maendeleo
ya sayansi na teknolojia wataalamu wamekuwa wakifundisha mambo mbalimbali
ambayo hurekodiwa na kuwekwa katika mitando kama vile YouTube ambapo unaweza
kuzitazama video hizo na kujifunza. kama unahisi unaelewa zaidi kwa njia ya
video kuliko zingine basi tumia njia hii ya video katika kujifunza kwako. Leo
hii kuna baadhi ya mambo mfano kuhusu komputa unaweza kujifunza kwa kupitia
kuangalia video fupi za YouTube.
4. Semina, hii ni njia nyingine
ambayo kwa hapa kwetu Tanzania imeibuka hivi karibuni. Njia hii imeshika kasi
sana na kuonekana ni bora sana na ni rahisi kwa kiasi Fulani. Semina
zimegawanyika ambapo zipo semina za bure na za kulipia. Usiogope kutoa pesa na
kwenda kwenye semina mbalimbali, Bali nakushauri tumia pesa yako katika semina
na hautokuja jutia hilo. Nakuambia hivyo kwa kuwa Nina uhakika semina
zinafundisha mambo mengi mazuri ambayo usingeweza kuyapata shuleni na
kwingineko.
5. Kanda za kunasia sauti/ tepu
rekoda, hii
ni njia nyingine sawa na njia ya video ila tofauti ni kuwa video huhusisha
sauti na picha ila njia hii haihusishi sauti na picha. Hivyo basi kama unahisi
hauwezi kujifunza kwa kupitia njia ya video au kusoma vitabu maana kuna vitabu
ambavyo huwekwa katika mfumo wa sauti(audibook) ambapo unaweza kuyapata Yale
yaliyomo kwenye kitabu kwa njia ya kusikiliza.
6. Kuwauliza wataalamu. Kila unachotaka kujifunza
kuna watu wanakijua na watu hawa ndio hufahamika kama wataalamu. Wataalamu hawa
hawapo kwa ajili ya kujisifia au kusifiwa juu ya utaalamu wao Bali wapo ili
kuwasaidia watu ambao wanashida na vitu ambavyo wao ndio wanautaalamu navyo.
Unapotaka kujifunza jambo na ukahisi unahitaji ushauri wa kitaalamu basi fanya
hivyo ili uweze kujifunza kupitia wataalamu hao.
Nimekuorodhoshea njia hizo sita za kujifunza
tofauti na shuleni. Simaanishi kuwa watu wasiende shuleni kujifunza Bali maana
yangu ni kuwa watu wasitegemee shule pekee maana shule pekee haitoshi, hivyo
watumie na njia hizi katika kujifunza Yale ambayo Nina uhakika shuleni hayapo
mfano elimu juu ya pesa.
Ni Mimi rafiki yako
Baraka maganga.
Bmaganga22@ gmail.com.
0754612413/0652612410.

No comments:
Post a Comment