Tuesday, November 10, 2015

Tegemea Kukutana Na Watu (5) Wa Namna Hii Katika Safari Yako Ya Mafanikio

.
Habari za wakati huu ndugu mpenzi msomaji wa mtandao huu. Ni matumaini yangu kuwa hu mzima na mwenye nguvu nyingi za kupambana ,hii yote ni katika kuhakikisha unajiletea mafanikio. Nami nakusihi endelea kupambana pasipo kuchoka. Leo nataka kukuletea aina zifuatazo za watu ambao utegemee kukutana nao. Katika safari yako ya kuelekea mafanikio


1. Wakatisha tamaa, tegemea kukutana na watu ambao watakukatisha tamaa sana kwenye safari yako ya mafanikio, watakuambia huwezi kwa kuwa elimu yako ndogo, watatumia umri wako, watatumia kabila lako, mkoa unaotoka n.k. watu hawa wapo tu na kama wakikushinda watakufanya usiende mbele na matokeo yake ukate tamaa na kushindwa. Hivyo basi pindi wanapokuja watu hawa hakikisha hawakushindi na kuwa sababu ya wewe kutokufanikiwa.

2. Watakao kucheka, kuna muda utakapoanzisha jambo Fulani kuna watu watakucheka sana na kukuona mjinga au mwendawazimu lakini jambo hili lisikufanye ukarudi nyuma katika safari yako ya kuelekea mafanikio. Lakini jambo moja ambalo nataka kukushauri ili uepukane na hali ya kuchekwa ni kuwa usipende kumwambia kila mtu malengo yako Bali mwambie mtu unaemwamini ili akushauri na sio kukuvunja moyo.

3. Watakao kupinga, wapo watu watakaokupinga sana na kukuwekea vizuizi mbalimbali katika safari yako ya mafanikio. Watu hawa sio kuwa hawajui kuwa unaweza kufanikiwa Bali wanajua kuwa unauwezo wa kufanikiwa tena sana, muda mwingine wanakuwa wanajua kuwa unaweza kufanikiwa mpaka ukawazidi wao na ndio maana wanakupinga kwa kuwa wanakuogopa. Mara nyingi anae kupinga anakuwa na sababu kuu mbili za kufanya hivyo aidha anaogopa utamzidi baada ya wewe kufanikiwa au ana wivu.

4. Watakao kuunga mkono, sio wote watakaokupinga wapo watu watakao kuunga mkono tena sana. Mara nyingi watu hawa ni watu wetu wa karibu kama vile wazazi, walezi, marafiki na wakati mwingine huwa watu ambao huwa tunakuwa hatuwajui ila tunakutana nao tu katika shughuli zetu na wanaungana na sisi ili tu kuhakikisha tunakuwa pamoja katika kujiletea mafanikio.

5. Watakao kushauri, utapokea ushauri kutoka sehemu mbalimbali lakini nakuomba kitu kimoja kuwa makini sana katika ushauri ambao utakuwa unaupokea maana ushauri mwingine utapewa kwa lengo la kutaka kukubomoa hivyo kabla haujaukubali ushauri huo ufanyie tathimini na ujiridhishe ndipo uuchukue.

 Katika Safari ya kuelekea mafanikio hautakuwa peke yako Bali utakuwa na watu wengine na moja ya watu ambao utakuwa nao ni kama hao niliokutajia hapo juu. Lengo la kukubainishia makundi haya ni kukufanya uyajue makundi hayo ya watu na uchukue taadhari ya ni jinsi gani ya kukabiliana nayo.

Ni mimi rafiki yako
Baraka maganga

0754612413/0652612410.

No comments:

Post a Comment