Sunday, November 8, 2015

Tabia Hii Itakuweka Mbali Na Malengo Yako Na Kukufanya Usifanikiwe.


Kila mtu anataka kufanikiwa, hakika hakuna mtu asiyependa kufanikiwa. Lakini mafanikio hayaji hivi hivi mafanikio yanapitia mambo mengi sana yenye kufurahisha na yanayovunja  moyo. Lakini yote hayo hayatoshwi kukufanya usifanikiwe jambo jingine ambalo nalo litakufanya usifanikiwe katika safari yako ya kuyaelekea mafanikio ni ile tabia ya  kuwaendekeza marafiki.


 Kila mtu ana marafiki hilo halipingiki na sikatazi watu kuwa na marafiki lakini jambo ambalo nataka kukutaadharisha Leo hii ni kuwa tabia ya kuwaendekeza marafiki itakufanya usifanikiwe kabisa. Namaanisha nini kusema kuwaendekeza marafiki?. Kuwaendekeza marafiki ni pale ambapo unajikuta ukishindwa kufanya mambo yako na shughuli zako ulizojiwekea kisa marafiki wamekuja na kukushawishi ufanye jambo jingine ambalo ni kinyume na ratiba yako binafsi.

 Jiulize ndugu msomaji ni mara ngapi rafiki yako amekuwa akija na kukuomba mwende sehemu mkatembee, mkaangalie Mpira kwenye vibanda vya mpira, mwende kwenye kumbi za sinema au hata kwenda kubalizi ufukweni. Na ukamkubalia ili hali ulikuwa na shughuli zako ambazo ulipanga kuzitekeleza. Chukulia mfano umejiwekea malengo ya kupunguza uzito hivyo ukaweka ratiba ya kufanya mazoezi ili kutimiza lengo lako la kupunguza uzito, unapoanza tu kufanya zoezi anakuja rafiki yako na kukuomba mkaangalie mpira, nawe kwa kuwa umemwendekeza rafiki yako unaamua kuhairisha mazoezi na kuambatana nae kwenye kibanda cha mpira ili mkaangalie mpira. Sasa jiulize kwa kufanya hivyo utayatekeleza malengo yako kweli?.

 Jifunze kumkatalia rafiki yako kwa baadhi ya mambo Fulani Fulani ili tu uweze kutekeleza ratiba zako ulizojipangia. Hiyo haitapunguza urafiki wenu kama kweli mnapendana na nimarafiki haswa kwani nachoamini Mimi rafiki yako lazima awe mwelewa na mwenye kuzijua na kuziheshimu ratiba zako, pia asiyeweza kuzivunja ratiba zako ovyoovyo. Nawe inatakiwa uwe na uwezo wa kuitetea ratiba yako ambayo itakufanya utekeleze malengo yako. Usipende kumfurahisha rafiki yako wakati wewe unajiumiza Mara kwa Mara. Kuwa na rafiki haimaanishi umnyenyekee maana kufanya hivyo unaweza kujikuta umekuwa mtumwa na sio rafiki.

 Marafiki ni watu muhimu sana tena sana lakini ni watu wa kuwa nao makini kwa kuwa rafiki anaweza kuwa mtu wa kwanza kukuulia ndoto zako bila wewe kujua kuwa ni rafiki yako ndiye chanzo cha wewe kushindwa kutekeleza malengo yako jambo la msingi na kubwa la kufanya chunguza sana ratiba anazokuletea rafiki yako.

Ni mimi rafiki yako
Baraka maganga
Bmaganga22@gmail.com

0754612413/0652612410.

No comments:

Post a Comment