Saturday, November 7, 2015

Jifunze Kusema Hapana Kwa Makundi Haya Manne (4) Ya Watu.


 Kihistoria tumejenga utamaduni Fulani ambao binafsi naomba niuite utamaduni mbovu sana, utamaduni huo ni ule wa kukubali kila tunaloambiwa na watu ambao wapo juu yetu kiuwezo, kiumri hata kielimu. Utamaduni huu binafsi nauona kuwa muda mwingine huwa kikwazo kikubwa sana katika maisha yetu na hata kuua ndoto na malengo yetu. Leo ndungu msomaji nataka nikushauri haswa kwa wewe ambaye unataka mafanikio kuwa jifunze kusema hapana kwa watu wafuatao:-

 1. Wazazi, tumeaminishwa kuwa kuwakubalia wazazi kwa kila jambo ambalo wanatuambia na hicho ndio kipimo cha heshima na adabu ya mtoto kwa wazazi wake. Tumeaminishwa kuwa mtoto anayekubali kila analoambiwa na wazazi wake huyo ndio mtoto mtiifu. Lakini leo nakushauri jifunze kusema hapana kwa wazazi wako, hii haitakufanya uonekane mtoto asiye na heshima wala adabu na unaposema hapana sema hapana ukiwa na lengo la kutaka kutetea ndoto na malengo yako. Chukulia leo wazazi wanataka usome masomo ya sayansi ili uje kuwa daktari lakini wewe ukiangalia huyawezi hayo masomo, kwa kuogopa kusema hapana unakubali ili hali ulitaka kusoma masomo ya biashara matokeo yake unakuja kufeli na udakitari haupati. Wazazi wale wale wanaanza kukulaumu kwa kushindwa kuwaambia ukweli mwanzo na matokeo yake umefeli. Angalia ulivyojialibia leo hii lakini yote haya yametokana na wewe kushindwa kutamka neno hapana.

2. Rafiki, tumekuwa ni watu wa kukubaliana na marafiki zetu hata kwa mambo tusiyoyataka. Pengine tumekuwa tukifanya hivyo ili tu tuonekane marafiki wema na watii na wenyekujari ama tumekuwa tukifanya hivyo kwa lengo la kuogopa kuvunja urafiki wetu. Lakini kushindwa kusema hapana kwa marafiki zetu kumetuponza wengi sana  leo hii wengine wapo jera kwa kesi za kuiba, wengine ni vibaka, wengine wavuta madawa ya kulevya na wengine wamepoteza maisha yote haya ni kwasababu tulishindwa kusema hapana kwa marafiki zetu. Mwambie rafiki yako hapana pindi unapohisi anakushawishi ufanye mambo ambayo huyataki.

3. Ndugu,jiulize ni Mara ngapi unekuwa ukifanya mambo usiyoyapenda wala kuyataka kisa alikuambia kaka, dada, babu, bibi, mjomba, shangazi n.k. bila shaka jibu ni Mara nyingi. Jiulize tena kwanini nilifanya hayo mambo nisiyoyapenda ili hali nilijua siyapendi? Jibu ni kwasababu ulishindwa kusema hapana kwa kuwa uliogopa watakuona sio mtiifu tena mwenye kukosa adabu. Jiulize tena kama unataka kuendelea na tabia hiyo ya kushindwa kusema hapana. Natumaini jibu ni hautaki tena kuendelea maana umegundua kufanya hivyo kunakuweka mbali na malengo yako.

4. Viongozi wako wa dini, hawa ni watu ambao wamekuwa na mchango mkubwa sana katika maisha yetu. Lakini tunachokosea ni kuwa tumewaamini sana hawa watu kiasi kwamba tumewafanya kuwa wao hawakoseagi hivyo badala ya kuwaheshimu tunawaogopa sana tukiamini woga wetu kwao ndio heshima kwao. Ndio maana hata ikitokea wanatuambia kitu ambacho hatukiitaji sisi hujikuta tumekikubali tu ili tuonekane watiifu kwao. Jifunze kusema hapana kwa watu hawa pia futa woga kabisa sema hapana kama kiongozi wako wa dini atakuambia vitu usivyovipenda.


 Kusema hapana kwa mtu aliye juu yako kiumri, uwezo, elimu, kiongozi wa dini au waalimu wako sio utovu wa nidhamu na tafadhari unaposema hapana hakikisha unatamka neno hili ukiwa na uhakika kuwa unasimamia ndoto na malengo yako usiseme hapana kisa umesoma hapa. Kabla hujasema hapana tafakari kwa kina sana ndipo useme hapana.
E

ndelea kutembelea mtandao huu kwa mambo mengi mazuri ya kujifunza na kujijenga. TWENDE SOTE.

No comments:

Post a Comment