Thursday, November 5, 2015

Sababu nne (4) zitakazokufanya ukate tamaa


.
Mara nyingi sana tukekuwa tukifanya shughuli zetu tukiwa na matumaini kuwa shughuli zetu zitafanikiwa lakini wakati mwingine mambo hutuendea kombo ambapo badala ya kufanikiwa katika zile shughuli zetu hujikuta tukiwa tumeshindwa. Pindi tunaposhindwa hapo ndipo ile hali ya kukata tamaa hujitokeza ambapo huwa tunakata tamaa. Sababu zinazotufanya tukate tamaa baada ya kushindwa ni pamoja na zifuatazo:-
1.woga, binadamu ni kiumbe ambaye amejawa na woga sana, kila binadamu ni mwoga lakini kinachowafanya wengine waonekane sio waoga wakati wengine wakionekana kuwa waoga sana no ule  uwezo wa kuukabili woga wao. Yule mwenye uwezo wa kukabiliana na hali ya woga huonekana kuwa sio mwoga ili hali yule asiye na uwezo wa kuukabili woga wake huonekana mwoga. Woga hutufanya tukate tamaa na tusijaribu tena pindi tunaposhindwa, hivyo ni vyema tujifunze  kukabiliana na woga.
2. Kutokuwa na malengo, tunakata tamaa kwasababu tunakuwa hatuna malengo, maisha bila malengo kwa binadamu hayana maana. Hii ni kwa kuwa binadamu asiye na malengo ni sawa na mnyama wa kufugwa ambaye kila siku hutegemea kupelekwa malishoni au kupelekewa chakula/malisho. Hivyo basi jiwekee malengo pia amua na kujitoa katika kuyatekeleza malengo uliyojiwekea, ukifanya hivyo hutoweza kukata tamaa tena.
3. Kutojiamini, pindi unaposhindwa unatawaliwa na hali ya kuto kujiamini ambapo muda mwingine hali ya kuto kujiamini huletwa na ile tabia ya kuanza kujilinganisha na wengine. Pindi unapojilinganisha na wengine hasa wale unaoamini wako juu yako kiuwezo hufanya ushindwe kujiamini katika shughuli zako na hivyo kukata tamaa yako. Ili ufanikishe jambo Fulani yapaswa ujiamini kuwa unauwezo wa kulifanya jambo hilo.
4. Kukosa uvumilivu, watu wengi tumekuwa tukikata tamaa pengine mapema zaidi hii ni kutokana na kukosa uvumilivu. Wengi wetu tumekuwa tukiamini mafanikio ni rahisi hivyo pindi tunapokumbana na vikwazo tunakuwa sio wavumilivu na matokeo yake tunakata tamaa mapema sana. Kukosa uvumilivu imekuwa sababu kubwa sana ambayo hutufanya tukate tamaa mapema bila hata kufikiri kujaribu kwa mara ya pili au hata ya tatu. Tujifunze kuwa wavumilivu katika safari ya mafanikio.
   Hauwezi kukipata kile unachokitaka ikiwa unakata tamaa, Leo hii watu wengi wamekuwa wakilalamika sana juu ya kutokufanikiwa kwao na wakati mwingine huwatupia lawama wengine lakini sababu ya kutokufanikiwa kwao hutokana na kukata tamaa kwao. Nimekueleza juu ya sababu zinazokufanya ukate tamaa ili uziepuke na hatimae ufanikiwe.

No comments:

Post a Comment