Thursday, November 5, 2015

Funguo Tatu (3) Muhimu Za Kukuza Biashara Na Kuwa Yenye Mafanikio.


Kuna njia muhimu za kuikuza biashara yako katika namna ambayo itakupendeza na kukuridhisha, biashara ambayo itawafurahisha wateja wako, na kuweza kukupatia kipato unachokitaka. Zifuatazo ni funguo tatu  zitakazokusaidia kupata mafanikio ya kweli katika biashara na kuweza kuifanya biashara yako kuwa na ukuaji endelevu.

1. Kuwa kiongozi wa biashara yako.
Ili kuweza kujenga biashara yenye mafanikio na yenye ukuaji endelevu unahitaji kuwa kiongozi wa biashara yako, badala kuwa mfanya kazi tu katika biashara hiyo, jione kama kiongozi wa biashara yako. Anza kwa kuwa wazi kuhusu kwa nini umeamua kuanzisha au ulianzisha biashara yako, na vipi kuhusu maono yako, unataka nini kutoka kwenye biashara yako na kwa ajiri ya maisha yako. Waza na ufikiri kama kiongozi wa biashara, na ubakie  mwenye nguvu na mwenye hamasa kubwa ili uweze kuiongoza biashara yako katika mwelekeo ulio sahihi.

2. Weka umakini kwa wateja wako.
Wajue wateja wako, Jitumbukize katika matatizo yao, changamoto zao,  masuala yao na malengo yao ili uweze kujenga, kutoa bidhaa na huduma zenye kiwango kikubwa na zenye ubora kwa wateja wako. Kutoa huduma na bidhaa ambazo zitaweza kupata matokeo makubwa na kuleta majibu chanya kutoka kwao. Na kama mteja wako ataweza kufurahia huduma na bidhaa zako unazotoa, kwa kiasi kikubwa sana atakusaidia katika   kukuongezea wateja, na kipato kwenye biashara yako kitaongezeka ikiwa atawaambia wengine kuhusiana na huduma zako nzuri pamoja na bidhaa unazotoa.

3. Weka umakini katika biashara yako.
Unachopaswa kuzingatia hapa ni kufahamu mambo muhimu katika  biashara yako ( masoko, mauzo n.k.)  ili kuweza kuifanya biashara yako ifanye kile inachosema, kwa kufanya hivi utakuwa unaiweka biashara yako katika njia ya kuelekea kwenye mafanikio na ukuaji. Unahitaji kuwa na ufanisi katika maeneo muhimu ya biashara yako, kuwa na ufanisi katika masoko, uuzaji na utunzaji wa fedha za biashara na hata kwenye mambo ya sheria. inakupasa kujua wajibu wako kama mmiliki wa biashara, unapaswa kujua rasilimali muhimu zinazoitajiwa na biashara yako, ili uweze kuiendesha biashara yako vizuri na kuweza kukupatia faida.
Hizo ni funguo tatu za kujenga biashara yenye mafanikio na ukuaji endelevu, nakutakia kila la kheri katika kuanzisha, kuendeleza na kuboresha biashara yako. Endelea kutembelea mtandao huu kila siku kwa mambo mazuri ya kujifunza na kujihamasisha na pia harika na wenzako ili nao waweze kupata mambo haya mazuri.
Ni mimi rafiki yako.
Geofrey mwakatika.
0767382324/0675555987. 

No comments:

Post a Comment