Friday, April 15, 2016
Zifahamu Sumu Kumi(10) Zinazowatesa Vijana Kwa Sasa.
Thursday, April 14, 2016
Sababu Za Kwanini Kila Siku Wewe Hauna Muda.
Habari za wakati huu ndugu msomaji wa
makala za mtandao huu, ni matumaini yangu kuwa hu mzima na unaendelea vyema
katika kubambana ili kuhakikisha kuwa unajiboresha zaidi na zaidi na baadae
unaweza kukamilisha yale ambayo umekwisha kujiwekea kama malengo katika maisha
yako. Nami nikusihi kuwa endelea kupambana pasipo kuchoka kwani harakati na
mapambano yanaendelea kila siku.
Wednesday, April 13, 2016
Zama Zimebadilika Sasa
.
Dunia inabadilika sasa, dunia inabadilika kila siku, kila
saa kila dakika, kila sekunde, kila mwaka dunia inabadilika. Je wewe
unabaadilika kulingana na dunia au unaendelea kuwa vile vile. Yaani wewe
unabaki kuwa vile vile kila siku, kila wiki, kila mwaka na kila mara au
unabadilika kulingana na wakati? Ni muhimu ukajijibu maswali haya bila
kigugumizi hata siku.
Tuesday, April 12, 2016
Tusihishie Kushabikia Tu.
Leo hii tanzania kimeibuka kitu ambacho kimeibuliwa na
serikali ya awamu ya tano. Ambacho kinatufanya wengi wetu tuwe mashabiki sana
wa hiki kitu. Wengi wetu leo hii tumekuwa tukishabikia sana sera ya mheshimiwa
raisi ya kutumbua majibu, kweli wengi sana tunashangiulia lakini leo nataka
kukusisitiza na kukuonya kuwa usiishie kuwa shabiki tu wa hii sera ya kutumbua
majipu.
Saturday, April 9, 2016
Mfahamu Mtu Huyu Vizuri.
Habari za wakati huu ndugu mpenzi msomaji wa makala za mtandao
huu, ni matumaini yangu kuwa hu mzima na unaendelea vyema katika kuhakikisha
kuwa unapambana ilivyo ili kuweza kujiletea mafanikio, nami nasema mapambano
yanaendelea kamwe usikate tamaa hata siku moja. Maana mpambanaji huwa hakubali
kukata tamaa kirahisi.
Wakati unaendelea kupambana ili kuhakikisha kuwa
unajiletea mafanikio ni vyema ukatambua jambo hili,kwa kuwaa ninaaini kuwa wewe
hiki kitu unakifanya ndio maana nikakuuliza je? Mtu huyu unamfahamu vizuri? Najua
kila mtu anasehemu au ana mtu ambaye huwa anakuwa anamwomba ushauri sasa
kutokana na kitendo hiki ndio maana kichwa cha makala hii kinauliza mtu huyu
unamfahamu vizuri?
Wednesday, April 6, 2016
Njia Hizi Zitakusaidia Kupambana Pindi Unapokabiliwa Na Changamoto.
Maisha yamejaa changamoto za namna mbalimbali, wakati
unapambana ili kujihakikishia kuwa unapata mafanikio au matokeo mazuri juu ya
mambo fulani swala la changamoto huwa linakuwa ni jambo ambalo halihepukiki
wakati mwingine. Ni muhimu tupitie katika changamoto kwani changamoto hizi huwa
zinatujenga na kutufanya tuwe imara zaidi na zaidi maishani,
Ni muhimu kusimama imara pindi tunapokuwa tunakabiliwa na
changamoto hizo. Hii ni kutokana na sababu kuwa uwezo wa kupambana na
changamoto hizi huwa upo mikononi mwetu. Ni muhimu kutambua kuwa kwa kila
changamoto inayokukabili ni muhimu uanze kujihoji kwanza na kujiuliza wewe
mwenyewe ufanye nini juu ya changamoto husika. Kwa kufanya hivyo utajikuta
unapata majibu ambayo yanakuwa msaada mkubwa sana kwako. Pamoja na hayo
zifuatazo ni baadhi ya njia ambazo zaweza kukusaidia wewe katika utatuzi wa
changamoto inayokukabili:-
Tuesday, April 5, 2016
Fahamu Kuwa Kila Jambo Linatawaliwa Na Kitu Hiki
Duniani kuna vitu vingi sana ambavyo binadamu huwa
tunakuwa tunavifanya au tunataka kuvifanya, vitu hivi vinaweza kuwa vizuri au
vibaya kutoka kwa mtu mmoja mpaka mtu mwingine hii ni kutokana na tofauti za kimtazamo
miongoni mwetu binadamu. Lakini pamoja na tofauti hizi za kimtazamo huwa
tunakuwa na kitu kimoja ambacho kinaweza kutuunganisha na kutuweka pamoja na
kitu hiki ndicho ambacho wapaswa kujua na kwenda nacho kama unataka kupata
matokeo makubwa. Kitu hicho sio kingine bali ni kanuni.
Monday, April 4, 2016
Usikubali Kutawaliwa Na Vitu Hivi Viwili.
Usikubali Kutawaliwa Na Vitu Hivi Viwili.
Habari za wakati huu ndugu mpendwa msomaji wa makala za
mtandao huu, ni matumaini yangu kuwa hu mzima na unaendelea vizuri katika
kupambana na hatimaye kuhakikisha kuwa unajiletea mafanikio binafsi. Nami
nakusihi endelea kupambana mpaka kieleweke.
Wakati unaendelea kupambana ili kujiletea mafanikio basi
ni vyema ukatambua kuwa vitu hivi viwili ni hatari sana kwako endapo
utaviruhusu vikutawale maishani. Maandiko ya biblia yanatueleza kuwa “kuweni na
kiasi”. Maneno haya yana maana kubwa sana na ninaomba uyashike wewe ambae
unataka kufanikiwa. Hapa nakwenda kukushirikisha vitu viwili ambavyo kamwe
usiruhusu vikutawale maishani mwako.
Subscribe to:
Posts (Atom)