Friday, April 15, 2016

Zifahamu Sumu Kumi(10) Zinazowatesa Vijana Kwa Sasa.

Habari za wakati huu ndugu msomaji wa makala za mtandao huu, ni matumaini yangu kuwa hu mzima na unaendelea vizuri. Mimi pia naendelea vizuri katika harakati za kupambana kimaisha. Leo nakuletea mambo kumi ambayo kwangu nimeyaita sumu ambazo zinatukumba vijana wengi sana kwa sasa.

Thursday, April 14, 2016

Sababu Za Kwanini Kila Siku Wewe Hauna Muda.

Habari za wakati huu ndugu msomaji wa makala za mtandao huu, ni matumaini yangu kuwa hu mzima na unaendelea vyema katika kubambana ili kuhakikisha kuwa unajiboresha zaidi na zaidi na baadae unaweza kukamilisha yale ambayo umekwisha kujiwekea kama malengo katika maisha yako. Nami nikusihi kuwa endelea kupambana pasipo kuchoka kwani harakati na mapambano yanaendelea kila siku.

Wednesday, April 13, 2016

Zama Zimebadilika Sasa

.
Dunia inabadilika sasa, dunia inabadilika kila siku, kila saa kila dakika, kila sekunde, kila mwaka dunia inabadilika. Je wewe unabaadilika kulingana na dunia au unaendelea kuwa vile vile. Yaani wewe unabaki kuwa vile vile kila siku, kila wiki, kila mwaka na kila mara au unabadilika kulingana na wakati? Ni muhimu ukajijibu maswali haya bila kigugumizi hata siku.

Tuesday, April 12, 2016

Tusihishie Kushabikia Tu.

Leo hii tanzania kimeibuka kitu ambacho kimeibuliwa na serikali ya awamu ya tano. Ambacho kinatufanya wengi wetu tuwe mashabiki sana wa hiki kitu. Wengi wetu leo hii tumekuwa tukishabikia sana sera ya mheshimiwa raisi ya kutumbua majibu, kweli wengi sana tunashangiulia lakini leo nataka kukusisitiza na kukuonya kuwa usiishie kuwa shabiki tu wa hii sera ya kutumbua majipu.

Saturday, April 9, 2016

Mfahamu Mtu Huyu Vizuri.


Habari za wakati huu ndugu mpenzi msomaji wa makala za mtandao huu, ni matumaini yangu kuwa hu mzima na unaendelea vyema katika kuhakikisha kuwa unapambana ilivyo ili kuweza kujiletea mafanikio, nami nasema mapambano yanaendelea kamwe usikate tamaa hata siku moja. Maana mpambanaji huwa hakubali kukata tamaa kirahisi.
Wakati unaendelea kupambana ili kuhakikisha kuwa unajiletea mafanikio ni vyema ukatambua jambo hili,kwa kuwaa ninaaini kuwa wewe hiki kitu unakifanya ndio maana nikakuuliza je? Mtu huyu unamfahamu vizuri? Najua kila mtu anasehemu au ana mtu ambaye huwa anakuwa anamwomba ushauri sasa kutokana na kitendo hiki ndio maana kichwa cha makala hii kinauliza mtu huyu unamfahamu vizuri?

Wednesday, April 6, 2016

Njia Hizi Zitakusaidia Kupambana Pindi Unapokabiliwa Na Changamoto.


Maisha yamejaa changamoto za namna mbalimbali, wakati unapambana ili kujihakikishia kuwa unapata mafanikio au matokeo mazuri juu ya mambo fulani swala la changamoto huwa linakuwa ni jambo ambalo halihepukiki wakati mwingine. Ni muhimu tupitie katika changamoto kwani changamoto hizi huwa zinatujenga na kutufanya tuwe imara zaidi na zaidi maishani,
Ni muhimu kusimama imara pindi tunapokuwa tunakabiliwa na changamoto hizo. Hii ni kutokana na sababu kuwa uwezo wa kupambana na changamoto hizi huwa upo mikononi mwetu. Ni muhimu kutambua kuwa kwa kila changamoto inayokukabili ni muhimu uanze kujihoji kwanza na kujiuliza wewe mwenyewe ufanye nini juu ya changamoto husika. Kwa kufanya hivyo utajikuta unapata majibu ambayo yanakuwa msaada mkubwa sana kwako. Pamoja na hayo zifuatazo ni baadhi ya njia ambazo zaweza kukusaidia wewe katika utatuzi wa changamoto inayokukabili:-

Tuesday, April 5, 2016

Fahamu Kuwa Kila Jambo Linatawaliwa Na Kitu Hiki


Duniani kuna vitu vingi sana ambavyo binadamu huwa tunakuwa tunavifanya au tunataka kuvifanya, vitu hivi vinaweza kuwa vizuri au vibaya kutoka kwa mtu mmoja mpaka mtu mwingine hii ni kutokana na tofauti za kimtazamo miongoni mwetu binadamu. Lakini pamoja na tofauti hizi za kimtazamo huwa tunakuwa na kitu kimoja ambacho kinaweza kutuunganisha na kutuweka pamoja na kitu hiki ndicho ambacho wapaswa kujua na kwenda nacho kama unataka kupata matokeo makubwa. Kitu hicho sio kingine bali ni kanuni.

Monday, April 4, 2016

Usikubali Kutawaliwa Na Vitu Hivi Viwili.

Usikubali Kutawaliwa Na Vitu Hivi Viwili.
Habari za wakati huu ndugu mpendwa msomaji wa makala za mtandao huu, ni matumaini yangu kuwa hu mzima na unaendelea vizuri katika kupambana na hatimaye kuhakikisha kuwa unajiletea mafanikio binafsi. Nami nakusihi endelea kupambana mpaka kieleweke.
Wakati unaendelea kupambana ili kujiletea mafanikio basi ni vyema ukatambua kuwa vitu hivi viwili ni hatari sana kwako endapo utaviruhusu vikutawale maishani. Maandiko ya biblia yanatueleza kuwa “kuweni na kiasi”. Maneno haya yana maana kubwa sana na ninaomba uyashike wewe ambae unataka kufanikiwa. Hapa nakwenda kukushirikisha vitu viwili ambavyo kamwe usiruhusu vikutawale maishani mwako.