Usikubali Kutawaliwa Na Vitu Hivi Viwili.
Habari za wakati huu ndugu mpendwa msomaji wa makala za
mtandao huu, ni matumaini yangu kuwa hu mzima na unaendelea vizuri katika
kupambana na hatimaye kuhakikisha kuwa unajiletea mafanikio binafsi. Nami
nakusihi endelea kupambana mpaka kieleweke.
Wakati unaendelea kupambana ili kujiletea mafanikio basi
ni vyema ukatambua kuwa vitu hivi viwili ni hatari sana kwako endapo
utaviruhusu vikutawale maishani. Maandiko ya biblia yanatueleza kuwa “kuweni na
kiasi”. Maneno haya yana maana kubwa sana na ninaomba uyashike wewe ambae
unataka kufanikiwa. Hapa nakwenda kukushirikisha vitu viwili ambavyo kamwe
usiruhusu vikutawale maishani mwako.
Tamaa ya pesa,
ndugu msomaji wa makala hii ni vyema ukatambua kuwa pesa ni kitu muhimu sana
tena sana kwa ajili ya maisha yetu ya kila siku. Natambua kuwa pesa ni kitu
muhimu kwa kuwa ndio inayotupatia mahitaji yetu muhimu kama vile chakula,
maradhi, nguo na huduma za kiafya. Natambua kuwa bila pesa huwezi kupata hivi
vitu. Lakini naomba nikuonye sasa kuwa tamaa ya pesa aikufanyi wewe kuwa na
pesa, na kubwa zaidi tamaa ya pesa inaweza kukupelekea wewe kutaka kupata pesa
kwa njia zisizo halali. Na hili ndilo jambo ambalo limekuwa likitukumba wengi
wetu kwa sasa. Kwamba kutokana na tamaa ya pesa tunajikuta tunaanza kufanya
mambo hata ambayo ni kinyume na maadili na miiko ya jamii kisa tu tupate pesa.
Ni vizuri kutamani kuwa na pesa lakini
mimi naomba wewe mwanamafanikio penda pesa usitamani pesa maana tamaa ni mbaya.
Ndio maana nakuambia kuwa na kiasi. Hata kama unatamani kuwa na pesa basi hiyo
tamaa yako iwe na kiasi, isiwe tamaa iliyopitiliza ambayo itakufanya wewe sasa
kutaka kuwa mwizi, jambazi, kahaba au hata shoga. Ongezeko la vitendo
visivyokubalika na jamii kama vile ushoga,ukahaba, ujambazi na wizi ni
kiutokana na tamaa za pesa ambazo watu tumekuwa nazo. Nasisitiza kuwa na kiasi.
2. Kutaka kulipwa zaidi ya unavyositahiri, hili
ni jambo ambalo watu tumeanza kukumbwa nalo nami nakusihi wewe unayetaka
kufanikiwa hakikisha kuwa hautawaliwi na jambo hili la kutaka kulipwa zaidi ya
unavyositahiri. Hapa nacho maanisha kama unatoa huduma fulani usitake eti
kwamba wewe ulipwe zaidi kuliko ubora wa huduma yako. Kama unauza bidhaa fulani
basi hakikisha kuwa ule ubora wa hiyo bidhaa unaendana na pesa unayoitaka.
Unafikiri nini chanzo cha matukio ya
utapeli na udanganyifu ni kutokana na sababu kuwa watu wanataka kulipwa zaidi
ya wanavyostahiri, hiki ndio chanzo. Sasa nakuonya wewe unaetaka kufanikiwa
kuwa jambo hili wewe halikufai waache wafanya wengine ila sio wewe. Na nakuonya
kwasababu waswahili wanasema “njia ya muongo ni fupi” hivyo kama ukifanikiwa
kwa njia hii tambua kuwa njia hii haitakupa mafanikio ya milele.
Kingine nachokusisitiza kuwa usipende
kulipwa zaidi tofauti na huduma unayostahili ni kwa sababu dunia inabadilika na
ushindani ni mkubwa sana leo hii, hivyo kama unataka kushindana na wenzio na
ubaki katika ushindani huo hakikisha kuwa unatoa kitu bora na kitu hicho
kiendane na thamani unayotaka. Mfano utakaposema bidhaa fulani labda tuseme
unauza nguo fulani elfu hamsini kweli ionekana ni ya elfu hamsini sio nguo ya
elfu kumi na tano wewe unataka uiuze elfu hamsini. Huko ndio kulipwa zaidi nako
kuzungumzia.
Kila kheri katika kuyasaka mafanikio. Na
usisahau kutembelea blog hii ili kuweza kujifunza zaidi na zaidi.
Mwandishi:
Baraka Maganga.
Mawasiliano:-simu-0754612413/0652612410.
No comments:
Post a Comment