Friday, January 29, 2016
Lazima Uwe Tayari Kufanya Jambo Hili Katika Safari Yako Ya Kuelekea Mafanikio.
Thursday, January 28, 2016
Fahamu Leo Kuwa Maneno Yana Nguvu Sana Katika Maisha Yako.
Habari za wakati huu ndugu msomaji wa mtandao huu wa kona
ya maarifa ni matumani yangu kuwa hu mzima na unaendelea vizuri katika
kupambana ili kuhakikisha kuwa unapata kile unachokitafuta katika maisha. Kwa
kuwa lengo la mtandao huu ni kuhakikisha kuwa unapata vitu vya kukusukuma mbele
zaidi katika kuelekea safari yako hiyo ya mafanikio, basi nasema pambana
endelea kupambana bila kuchoka hata pale unapohisi umechoka jilazimishe maana
kuridhika baaada ya hatua chache huleta anguko.
Najua umekuwa ukupambana sana katika kuhakikisha kuwa
unafanikisha mambo yako lakini kuna wakati ukikaa na kupiga tathimini unajikuta
ukitamani kukata tamaa hii ni baada ya kuona au kupata matokeo ya tathimini
yako na hapo ndipo wengi huwa tunapatwa
na hofu ya kuacha na mara nyingi sana huwa tunaanza kuona ni kama hatupigi
hatua hivyo basi tunatamani kuachana na harakati zetu ambazo tumekuwa
tukizianzisha na kuamini kuwa zitakuwa na msaada kwetu. Unatamani kuacha
nakuona unasoma hii makala na huku unasema dah yaani sioni matokeo yoyote,
niliambiwa hivi na vile, nilisoma hivi na vile lakini sioni matokeo yake,
naacha bwana.
Kabla hujafikiria kufanya kitu hicho unachotaka kufanya
nataka ujichunguze sehemu hii moja, yachunguze maneno yako. Kabla hujafikiria
kufanya uamuzi wa kuacha kufanya jambo fulani kwa kuwa tu hujapata matokeo
mazuri yachunguze maneno yako, narudia
tena yachunguze maneno yako. Unajua binadamu tuna namna mbili za kuongea,
nakuona unashangaa kusikia namna mbili za kuongea, namaanisha kuwa tunakule
kuongea kwa kawaida ambapo tunaongea na wenzetu huku kumezoeleka na ni maarufu
lakini aina ya pili ni ile ya kujiongelesha wenyewe, yaani kuna muda huwa unajikuta uwapo mwenyewe kuna
maneno unayojiongelea mwenyewe sasa maneno haya ndio nayo taka uyachunguze.
Jiulize mwenyewe hapo ulipo je kauli unazojisemesha
mwenyewe ni hasi au chanya, nakuona unasita kutoa jibu kwa kuwa unajua ni hasi.
Wengi tumekuwa hatujui nguvu iliyopo katika maneno yetu ambayo tumekuwa tukijisemesha
mara kwa mara na ndio maana tumekuwa tukihangaika kuchunguza mchawi wa maisha
yetu kumbe sisi wenyewe ndio tunao jiloga. Unajiloga kwa maneno yako mwenyewe
alafu unajikuta unalalama eti nalogwa na ndugu zangu hawataki nifanikiwe
kabisa. Dah wewe, nani asiyetaka ufanikiwe wewe au wao?, jibu unalo mwenyewe
mpaka hapo.
Pengine unajiuliza sasa mbona mimi sielewi ni kauli gani
sasa, sawa mimi nipo kukuletea hizo kauli, mara ngapi umekuwa ukijisemea kuwa
wewe unamikosi, nuksi au gundu. Ndio umekuwa ukijiambia ukisema unamikosi,
gundu au nuksi maana yake huwezi kufanikiwa sasa kwanini unataka kufanikiwa
ikiwa kila siku unajisemesha mwenyewe kuwa hauwezi kufanikiwa. Huoni kuwa
unafanya kazi ya kuchanganya maji machafu kwenye maji masafi alafu unategemea
maji masafi yaendelee kuwa masafi. Eti unataka kuacha kufanya mambo ya
kukusogeza mbele kisa unamikosi, na ukiamini na kujisemesha kuwa unamikosi
kweli utakuwa nayo tena mingi haswa. Acha kujisemesha na kujitazama kama mtu
mwenye mikosi, gundu, na nuksi. Acha mara tu baada ya kusoma makala hii.
Mara ngapi umekuwa ukisalimiwa asubuhi unaambiwa habari
ya asubuhi ndugu unajibu aa bora kumekucha, au dah bora ya jana, hivi unajua
maana ya hayo maneno unayoyasema. Unayasema maneno hayo alafu akilini mwako
unawaza kuwa biashara yako itakwenda sawa. Nani kakudanganya wewe acha
kujidanganya, ukisema bora kumekucha maana yake haukutaka kukuche sasa
unaendeleaje na shughuli kama hautamani kukuche?, ukisema dah bora ya jana
maana yake siku ya leo ni ya ovyo sasa unategemea vipi kudharisha katika siku
mbovu?, anza siku yako na kauli nzuri na mafanikio utayaona
.
Nakuona kila ikifika ijumaa unajifanya mzungu eti “thanks
God it is Friday” ukimaanisha asante mungu kwa kuwa leo ni ijumaa. Unajua
tafsiri yake hapo tafsiri yake ni kuwa siku zote zilikuwa mbaya kwako ndio
maana unafurahia kuiona ijumaa. Sasa kwanini utake kufanikiwa jumatatu wakati
kwako ni mbaya? Au alhamisi wakati ilikuwa mbayas?
Kuwa makini na kauli unazojinenea mwenyewe maana mnamo
maneno mna nguvu sana, maneno huumba hilo waswahili waliliona na sio kuumba tu,
maneno yanaamua maisha yetu ya sasa na baadae.hivyo basi kuwa makini sana tena
sana juu ya maneno yako kama kweli unataka kufanikiwa. TWENDE SOTE.
Ni mimi Baraka
Maganga, rafiki na mwalimu wako.
Wasiliana nami kwa nambari za simu 0754612413/0652612410. Au kwa barua
pepe ambayo ni Bmaganga22@gmail.com.
Wednesday, January 27, 2016
Hivi Ndivyo Mambo Yatakavyokuwa Baada Ya Wewe Kufanya Kitu Hiki Kimoja.
Habari za wakati huu ndugu msomaji wa mtandao huu wa kona
ya maarifa ni matumaini yangu kuwa hu mzima wa afya na unaendelea kupambana kwa
hali na mali ili tu uweze kufanikisha yale ambayo umekuwa ukiyahangaikia mara
kwa mara. Vizuri endelea kupambana naama hakuna kitu cha bure hapa duniani,
maana hata miujiza huja kwa wale ambao huwa wanakuwa wakiitafuta miujiza hiyo.
Sio waliokaa tu wakisubiri miujiza hivyo nakusihii endelea kupambana ndugu
msomaji wa mtandao huu.
Mafanikio yanahitaji ahadi
ndugu mpendwa msomaji wa makala hii. Hili ni jambo ambalo ningependa uweze
kulifahamu kuanzia sasa,kuwa mafanikio yanahitaji ahadi. Yaani baada ya
kujiwekewa malengo unapaswa sasa kuweka ahadi juu ya utekelezaji wa malengo
yako. Pengine umekuwa ukijiwekea ahadi bila kujua ahadi ni kama pale unaposema
kuwa nataka kupunguza uzito likiwa kama lengo lako sasa pale unaposema lazima
kila siku nifanye mazoezi kwa muda wa nusu saa, tayari hapo unakuwa umejiwekea
ahadi katika maisha yako. Au unasema nataka kuamka kila siku saa kumi na moja
alfajiri ili niweze kufanya shughuli zangu za ndani kabla ya kwenda katika
mihangaiko yangu, kuamka saa kumi na moja ni ahadi tayari uliyokwisha jiwekea
katika maisha yako.
Tumekuwa watu wa kujiwekea ahadi nyingi nyingi tena ahadi
zingine zinakuwa kubwa na zenye kututisha kiasi kwamba tunaweza kufikiri kuwa
hatutoweza kutimiza ahadi hizo. Kimsingi ahadi na malengo ni vitu ambavyo
vinaenda sambamba na vinaweza kukupatia shida katika kuvitofautisha lakini
tofauti ni kuwa malengo yanaanza alafu ndio ahadi hufata. Sasa kwa kuwa ahadi ni hatua
moja wapo katika kuyaelekea mafanikio basi ni vyema ukatambua kuwa yafuatayo ni
mambo ambayo yatakukumba baada ya kuwa umejiwekea ahadi zako wewe mwenyewe:-
1. Vikwazo vitaibuka,
baada ya kuwa umeshajiwekea ahadi zako vikwazo vitaibuka sana tena vingi kuliko
unavyodhani. Vitaibuka vikwazo vya aina mbili ambavyo ni vikwazo vya nje na vya
ndani. Vikwazo vya nje ni vile ambavyo vitatokana na wale watu wanaokuzunguka
kama vile marafiki, ndugu au hata wazazi, ambao wanaweza kukuzuia wewe katika
kuweza kutekeleza ahadi yako, zinaweza zikawa kauli zao juu ya ahadi yako au
hata kukucheka na kukupinga zaidi na zaidi. Vikwazo vya ndani ni vile ambavyo unajiwekea
mwenyewe kama vile uvivu, kukosa umakini, kupuuzia ahadi yako n.k. hivyo
vikwazo vyote hivi visikutishe katika kuweza kuishikiria ahadi yako na hatimaye
kuweza kuitekeleza ipasavyo.
2. Utafanya makosa,
katika kuelekea kutekeleza ahadi yako utafanya makosa kadha wa kadha, makosa
haya yapo ili tu kukufunza. Kama unataka kufanikiwa ni lazima uwe na mtazamo
tofauti juu ya makosa unayoyafanya. Kama kweli unataka kusonga mbele katika
safari yako ya mafanikio sasa ni wakati wa kubadili mtazamo wako katika makosa
unayoyafanya. Amini kuwa makosa yapo tu ili kuweza kukufunza na sio kingine.
Hivyo basi usirudi nyuma katika kuitekeleza ahadi yako uliyojiwekea, makosa
yasikutishe bali jifunze jifunze kutokana na makosa.
3. Utavunjwa moyo,
hili nalo litakukumba kwa kiasi kikubwa na hasa kitakacho kuvunja moyo ni pale
utakapo kuja kujikuta umefanya makosa mengi na pale utakapo ona kuwa unakumbwa
na vikwazo vingi sana. Mambo haya yote yanaweza kukuvunja moyo kwa kiasi kikubwa sana, lakini kwa wewe unae
yasaka mafanikio kamwe usivunjike moyo bali wewe endelea kuishikiria ahadi
yako.
Tambua kuwa haya yote ni majaribu ambayo
dunia itakuwekea ili kukupima ni jinsi gani uko makini juu ya ahadi yako. Mara
nyingi watu wengi hutamani kuachana na ahadi zako, lakini wewe unaye yasaka
mafanikio hutakiwi, hutakiwi kukata tamaa kamwe. Kama alivyosema bwana winstone
Churchill “never never never give up” au kama alivyosema bwana james .J.
Gorbelt “you become a champion by fighting one more round, when things are
tough you fight one more round”. Yaani unakuwa mshindi baada ya kupambana hatua
moja zaidi na zaidi hata kama mambo yakiwa magumu pambana hatua moja zaidi.
Twende sote.
Ni mimi rafiki yako,
Baraka Maganga
Wasiliana nami kwa.
Simu: 0754612413 au 0652612410.
Barua
pepe: Bmaganga22@gmail.com
Tuesday, January 26, 2016
Ni Muda Wa Kuachana Nazo Sasa
.
Habari za wakati huu ndugu msomaji wa mtandao huu wa kona
ya maarifa ni matumaini yangu kuwa hu mzima wa afya na unaendelea kupambana kwa
hali na mali ili tu uweze kufanikisha yale ambayo umekuwa ukiyahangaikia mara
kwa mara. Vizuri endelea kupambana naama hakuna kitu cha bure hapa duniani,
maana hata miujiza huja kwa wale ambao huwa wanakuwa wakiitafuta miujiza hiyo.
Sio waliokaa tu wakisubiri miujiza hivyo nakusihii endelea kupambana ndugu
msomaji wa mtandao huu.
Je unakumbwa na wasiwasi wa kufanikiwa kutokana na
historia yako ya nyuma zile kauli wanazokuambia wanaokuzunguka zinakurudisha
nyuma katika hali ya kutaka kusonga mbele katika kuhakikisha kuwa unafanikiwa
katika maisha yako. Je? unajua ni kwa nini kauli ulizopandikizwa kutoka
utotoni zinaendelea kukurudisha nyuma
katika safari yako ya kuyaelekea mafanikio, ni kwasababu umeziamini na
kuzifanya kuwa ukweli wako. Sasa jiambie mwenyewe kuwa ni wakati wa kuachana nazo sasa.
Zile imani ulizojijengea zamani ya kuwa hutofanikiwa na
kuwa tajiri kwa kuwa wazazi wako ni masikini, imani ya kuwa huto fanikiwa kwa
kuwa wazazi wako ni masikini, ni muda wa kuachana nazo maana hazina msingi
wowote na wala hazikujengi wala kukusaidia chochote bali zinakudidimiza zaidi
na zaidi badala yake wewe pambana kweli kweli hata kama unatokea katika familia
masikini, na mafanikio utayaona tu, maana wapo waliokuwa kama wewe na
waliotokea chini kama wewe na wakafanikiwa hivyo hilo lisikupe shide sana bali
achana na hiyo imani.
Uliambiwa kuwa wewe ni mjinga na hauwezi chochote na
mwalimu wako, ni wakati wa kuachana na kauli hii ambayo ulikuwa umeiamini kwa
kuwa ilitoka kwa mwalimu wako na kupitia kigezo cha sifa ya ualimu basi
ukaamini kuwa hauto fanikiwa fanya kama Thomas
Edison ambaye pamoja na kukataliwa na walimu watatu tofauti kuwa hafai kuwa
mwanafunzi wa kujifunza chochote lakini alijifunza na kuwa mwanasayansi mkubwa
duniani na mpaka leo anaheshimika kama mwanasayansi mashuhuri duniani. Hii ni
kutokana na sababu kuwa yeye aliachana na kauli za waalimu wake, hivyo basi
hata wewe unaweza kufanya hivyo na ukafanikiwa pia, hivyo achana na kauli mbovu
alizokuambia mwalimu wako.
Walikuita mbumbumbu mtaani kwenu, mtaani kwenu wewe ndio
ulionekana kuwa mtoto mbumbumbu kuliko wote na ukafutwa kabisa kwenye watoto
ambao wanaweza kuleta mabadiliko yoyote au kuleta mafanikio yoyote ambayo
yataisaidia jamii yako na wewe ukaamini kuwa kweli hauwezi kutokana na maneno
yao. Ni muda sasa wa kuachana na kauli hizo ambazo hazina msingi wowote bali ni
za ukatishaji taama.
Lazima utambue kuwa
tunakuwa kadri tunavyofikiri, hata bibilia imeliandika hilo kuwa kadri
ajionavyo mtu nafsini mwake ndivyo huwa. Hii inamaana kuwa wewe mwenye ndiye
mwamuzi wa maisha yako yaani ni kadiri unavyojiona wewe mwenyewe ndivyo huwa unakuwa.
Na biblia haijasema kadri wamwonavyo watu ndivyo mtu huwa, hilo ni jambo ambalo
halijaandikwa wala kusemwa. Hivyo basi kama wamesema hauwezi kufanikiwa ni wao
na sio wewe, wewe usizifuate kauli zao ambazo hazina msingi wowote bali wewe
endelea kushikilia ukweli ambao unauona nafsini mwako na katika kuushikilia
ukweli huu uwe ni ukweli ule ambao ni chanya achana na kauli hasi kabisa maana
hazikufikishi popote.
Kumbuka nimesema ni muda wa kuachana nazo zile kauli zote
ambazo ni hasi, ni muda wa kuachana nazo maana hazina msaada kwako ila zina
kudumaza na kukudidimiza zaidi na zaidi. Na kubwa zaidi juu ya kauli chanya ni
kuwa haziwezi kukuletea mafanikio yoyote.
Twende
sote.
Ni mimi rafiki yako,
Baraka Maganga
Wasiliana nami kwa.
Simu: 0754612413 au 0652612410.
Barua
pepe: Bmaganga22@gmail.com
Monday, January 25, 2016
Wajibika Ipasavyo Kama Kweli Unataka Kufanikiwa.
Habari za wakati huu ndugu msomaji wa mtandao huu wa kona
ya maarifa ni matumaini yangu kuwa hu mzima wa afya na unaendelea kupambana kwa
hali na mali ili tu uweze kufanikisha yale ambayo umekuwa ukiyahangaikia mara
kwa mara. Vizuri endelea kupambana naama hakuna kitu cha bure hapa duniani,
maana hata miujiza huja kwa wale ambao huwa wanakuwa wakiitafuta miujiza hiyo.
Sio waliokaa tu wakisubiri miujiza hivyo nakusihii endelea kupambana ndugu msomaji
wa mtandao huu.
Naamini umekuwa ukipambana sana katika kuhakikisha kuwa
unafanikiwa katika yale ambayo unayahangaikia nami na kusihi uendelee kupambana
maana katika mahangaiko ndiko mafanikio hutokea. Lakini lazima ujue kuwa lazima
kitu hiki ukifanye kama unataka kufanuiki. Kitu hiki ni kitu muhimu sana katika
maisha yetu na mafaniko kwa ujumla lakini jambo la kushangaza ni kuwa tumekuwa
hatulitili maanani sana na ndio maana wengi wetu tumekuwa tukijikuta hatusongi
mbele wala nini ila tunabaki pale pale au kurudi nyuma kabisa kimaisha.
Huwa unapata picha gani pindi unapoona mfanyakazi fulani katika
kampuni fulani kafukuzwa kazi. Au kasimamishwa kazi kwa muda. Unapata picha
gani pindi unapomwona mfanyabiashara fulani kashindwa kibiashara yaani biashara
yake imekufa. Unapata wazo gani unapomwona mtu anailaumu serikali yake kwa
kushindwa kwake wakati yeye ndiye aliyepaswa kufanya jambo husika. Hakika yote
hayo hutokea kutokana na kukosekana kwa kitu hiki kimoja nacho ni uwajibikaji.
Maishani bila kuwajibika tambua kuwa hauto kwenda kokote
kule bali utaishia pale pale. Dunia ya sasa imejaa ushindani wa hali ya juu
ambao unaongezeka siku hadi siku na atakae weza kusitaimili ushindani huu ni yule
tu mwenye kuweza kuwajibika ipasavyo. Kama wewe ni mfanyabiashara na
unawajibika bora liende tambua kuwa hauto kwenda popote bali utaishia kufulia
tu. Mfanyakazi pia ambae hutaki kuwajibika tambua kuwa utaishia tu kufukuzwa
kazi yako hiyo na hatimae kuukaribia umasikini nao utakukaribisha vizuri sana
kuliko unavyodhani.
Leo hii takwimu zinaonyesha kuwa kati ya biashara mia
moja zinazo anzishwa leo baada ya miaka kumi ni biashara chini ya ishirini
ndizo huwa zimekuwa. Hii ni kutokana na uwajibikaji mbovu wa wafanyabiashara
husika. Wafanyabiashara hawa wamekuwa hawahangaiki katika kutafuta taarifa
sahihi kabla ya kuzianzisha biashara zao na vile vile wamekuwa wagumu wa kuendelea
na utafiti baada ya kuanzisha biashara zao, hivyo hata yakitokea mabadiliko wao
hawashituki wala nini. Bali huendelea kufanya biashara zao kwa mazoea na
matokeo yao hujikuta wamefulia maana hujikuta hawapati wateja. Hii ni kutokana
na uvivu ulio letwa na kuto taka kuwajibika kwao na ndio maana wanajikuta
wameanguka.
Ukiwa mfanyakazi unajisikiaje pale unapoambiwa
tunakuwajibisha kutokana na utendaji wako mbovu angalia leo hii ni watu wangapi
wamesimamishwa kazi toka uongozi wa awamu ya tano uingie madarakani na wote
sababu zimekuwa zikionekana ni uwajibikaji mbovu na mengine, lakini kubwa ni
uwajibikaji mbovu ambao huwapelekea wafanye mambo kiholera holera na matokeo
yake ni kuja kuwajibishwa.
Kama unataka kufanikiwa hakikisha unayavaa majukumu yako
usisubiri mazingira yaje ya kushitaki na kukuwajibisha vikali. Au usisubiri
kufulia kukuwajibishe, ukiwa mfanyabiashara usisubiri anguko la biashara
likuwajibishe, mfanyakazi usisubiri kuwajibishwa na bosi wako bali vaa majukumu
yako mwenyewe na mafanikio utayaona tu. Ikiwa unasubiri kuwajibishwa basi sahau
kuhusu mafanikio na usilizungumzie tena neno hilo.
Ni mimi rafiki yako,
Baraka Maganga
Wasiliana nami kwa.
Simu: 0754612413 au 0652612410.
Barua
pepe: Bmaganga22@gmail.com
Thursday, January 21, 2016
Furahia Vitu Hivi Wala Usilaumu Sana Juu Yake.
Habari za wakati huu ndugu msomaji wa mtandao huu wa kona
ya maarifa ni matumaini yangu kuwa hu mzima wa afya na unaendelea kupambana kwa
hali na mali ili tu uweze kufanikisha yale ambayo umekuwa ukiyahangaikia mara
kwa mara. Vizuri endelea kupambana naama hakuna kitu cha bure hapa duniani,
maana hata miujiza huja kwa wale ambao huwa wanakuwa wakiitafuta miujiza hiyo.
Sio waliokaa tu wakisubiri miujiza hivyo nakusihii endelea kupambana ndugu msomaji
wa mtandao huu.
Ukiwa bado unaendelea
kupambana katika harakati zako basi jifunze
kufurahia mateso,matatizo na vipingamizi mbalimbali uvipatavyo kwa sasa.
Kwanini nasema jifunze kuyafurahia mateso, matatizo na vipingamizi vya sasa?.
Sababu ninazo kupa hapa basi zinaweza kuwa muhimu kwako kuweza kukufanya
uyafurahie mateso, matatizo na vipingamizi kadha wa kadha.
1.
Vinakufunza,ni
kweli kuwa watu tulishawahi kupita, tunapitia na pengine tunaweza kuja kupitia
katika mateso, matatizo na vipingamizi vya aina mbalimbali. Kama ulishawahi
kupita katika mateso, vipingamizi au matatizo fulani basi utakubaliana nami
kuwa vitu hivi huwa vinafunza. Jiulize swali hili huwa unajisikiaje pindi
unapokuwa unapitia katika matatizo?, au pindi unapopitia vipingamizi fulani?,
kama huwa unachukulia vitu hivi kwa hasira alafu unaanza kulalamika basi tambua
kuwa una mtazamo hasi, na hivyo inabidi ubadili mtazamo huu na ujenge mtazamo
wa kuyaangalia mateso, matatizo na vipingamizi vyako kwa hasira kisha acha
kulaumu na baadae jiulize umejifunza nini kutokana na mambo hayo?. Huwa
unajifunza nini pindi unapopingwa na wenzio je? unajawa na hasira na kuishia
kulaumu au huwa unapatwa na hasira na unajifunza kuwa unapaswa kubadilika
pengine unapingwa kutokana na kutokuwa bora katika jambo fulani, hivyo jifunze
kutokana na kupingwa na ukajiboreshe zaidi na zaidi. Mateso unayoyaona leo
yageuze kuwa kama somo. Matatizo pia yawe somo mfano unapokuwa na tatizo la
pesa unajisikiaje?, unakubali hali au unajifunza na kulitatua tatizo hilo.
2.
Vinakuimalisha,
matatizo, vipingamizi na matatizo, muda mwingine huwa kama viimalisho vyetu.
Mfano matatizo yako yapo ili kukufanya uwe bora zaidi na zaidi. Mfano unapopata
pingamizi kutoka sehemu mbalimbali kama vile unapopingwa kutokana na kigezo cha
ukosefu wa elimu katika sehemu fulani ni muda wa kwenda kujiimalisha sasa ili
uwe bora zaidi na usije ukapigwa tena na tena. Mateso muda mwingine
usiyachukulie kama yapo kwa ajili ya kukutesa bali yapo kwa ajili ya
kukuimalisha zaidi katika Nyanja mbalimbali za maisha.
3.
Vinakuamsha
katika usingizi mzito, mateso, vipingamizi na matatizo yapo
ili kukuamsha katika usingizi mzito
ambao umelala. Mfano halisi ni kuwa sisi binadamu huwa tunakumbwa na hali ya
kujisahau pindi tunapojikuta kuwa tumefanikiwa kwa kiasi fulani na hapo ndipo
wakati mwingine vipingamizi huja kwa ajili ya kutuamsha kutoka katika usingizi
mzito ambao huwa tunakuwa tumelala pengine ni kutokana na baadhi ya mafanikio
ambayo tunakuwa tumelala kwa muda. Binadamu huwa tunakuwa na hali ya kujisahau
sana pindi tunapokuwa tumeona kuwa hali kwetu ni nzuri na hapo huwa tunajisahau
sasa kwa wakati huu ndio huwa ni muhimu sana tena sana kuweza kuamshwa kutoka
katika usingizi huu tulio lala. Matatizo mengi huja kwetu ili kutuamsha kutoka
katika usingizi mzito tuliokuwa tumelala na hivyo kuweza kutuamsha. Mfano kama
mfanyabiashara ukiwa umezoea kupeleka biadhaa zako mahali Fulani kwa wateja
wako, kutokana na kufanya biashara kwa mazoea maana unafanya tu hutaki
kuboresha bidhaa zako siku bidhaa yako ikipingwa na wateja wako, utakuwa
umeamshwa sana. Pengine unateswa kwa kuwa umelala sasa inatakiwa uamke ili
usiendelee kuteseka kama ukiendelea kulala maana yake utaendelea kuteseka.
Hivyo
basi furahia mateso, matatizo na vipingamizi kwa maana ndani yake vimebeba mafunzo
zaidi na zaidi.
Ni mimi rafiki yako,
Baraka Maganga
Wasiliana nami kwa.
Simu: 0754612413 au 0652612410.
Barua
pepe: Bmaganga22@gmail.com
Wednesday, January 20, 2016
Lazima Kitu Hiki Kiendelee Kuwepo Duniani, Na Ni Muhimu Kiwepo.
.Habari za wakati huu ndugu msomaji wa mtandao huu wa kona
ya maarifa ni matumaini yangu kuwa hu mzima wa afya na unaendelea kupambana kwa
hali na mali ili tu uweze kufanikisha yale ambayo umekuwa ukiyahangaikia mara
kwa mara. Vizuri endelea kupambana naama hakuna kitu cha bure hapa duniani,
maana hata miujiza huja kwa wale ambao huwa wanakuwa wakiitafuta miujiza hiyo.
Sio waliokaa tu wakisubiri miujiza hivyo nakusihii endelea kupambana ndugu
msomaji wa mtandao huu.
Ikiwa unapambana katika kuhakikisha unasonga mbele na
wala sio kurudi nyuma basi ni vyema ukaelewa kuwa kitu hiki kimoja kisikutishe
sana maana ni lazima kiendelee kuwepo hapa duniani, yaani usikihofie kitu hiki
kwa maana ni cha muhimu sana tena sana. Kitu chenyewe ni tofauti zilizopo baina yetu sisi wanadamu. Ni wazi na ukweli
usio pingika kuwa binadamu tunatofautiana sana tena sana na kwa kiasi kikubwa,
kama ulikuwa hujui kuwa binadamu tunatofautiana basi anza kuelewa kwanzia sasa
kuwa binadamu tunatofautiana na tofauti hizi zipo baina yetu na zinajionesha
wazi wazi miongoni mwetu. Ngoja nikuwekeee mifano kadhaa ili uwezo kuelewa ni
namna gani binadamu tunatofautiana tena kwa makundi tofauti tofauti.
Mfano katika maisha ya kawaida utofauti wetu unaweza
kujionesha kutokana na shughuli au kazi
zetu, ndio maana katika maisha tuna madaktari, tuna manesi, tuna waalimu, tuna
wafanyabiashara, tuna madereva, tuna wasio waajiriwa, tuna wawekezaji pamoja na
wajasiliamali n.k. bado katika makundi hayo hayo yanatofauti pia mfano katika kundi la
madaktari tuna madaktari bingwa wa macho na wale bingwa kwa magonjwa ya watoto,
katika waalimu tuna waalimu wakuu na waalimu wasio na cheo au kitengo chochote,
katika kundi la madereva tuna madereva wa mabasi ya mikoani, daladala na
madereva wa malori. Huu ni ufafanuzi kidogo ambao unaonesha jinsi gani binadamu tunatofautiana sana tena sana.
Sasa utofauti huu usikutishe maaana haupo ili ukutishe
bali upo ili kukupa changamoto na fursa wewe ili upate kuelewa ni wapi ambapo
panakufaa haswa. Utofauti huu upo ili kukufanya wewe ufanye uchaguzi sahihi ni
kundi gani linakufaa haswa na ni wapi unapataka. Hivyo basi badala ya kutishika
na utofauti huu wewe chukulia utofauti huu kama fursa ya wapi panakufaa.
Usitishike wala kuogopa unapoona mtu fulani kawa mfanyabiashara maarufu, fulani
kawa daktari bingwa, kawa mchezaji bora, kawa mwamasheria n.k bali chukulia
kama fursa ya wewe kuchagua ni wapi haswa panapokufaa na upange ni jinsi gani
haswa utaweza kufika pale.
Pia ni muhimu ukatambua kuwa utofauti huu wa kimaisha
unaweza kukusaidia wewe kufanya mambo fulani fulani, mfano utofauti unaweza
kupelekea yafuatayo kwako:-
1) Utofauti huu ndio hutukumbusha ya kuwa
tunapaswa kuwajibika, kupitia tofauti zilizopo au zinazojitokeza
kati yetu ndizo huwa kichocheo cha sisi kupambana ili kuhakikisha kuwa
tunasonga mbele au kupata molari ya kujikwamua katika hali ambazo tunazo. Hebu
chukulia mfano ni hali gani huwa unakuwa nayo pindi unapokutana na rafiki yako
ambaye mnaendana kwa baadhi ya vitu kama vile umri, elimu, historia ya kimalezi
na zaidi mlisoma na kucheza pamoja lakini
baada ya kuacha nae kwa muda anarudi akiwa na mafanikio makubwa sana
kuliko wewe, tayari mmeshatofautiana japo mlikua na kusoma pamoja, sasa baada
ya kuyaona mafanikio ya huyo rafiki yako, ni nini unachopata kwa mara ya kwanza?.
Nadhani ni hisia za kuwajibika ili uweze kuwa kama rafiki yako.
2) Hutufanya tuzichukie hali fulani,
kupitia utofauti tulionao basi hutufanya tuzichukie baadhi ya hali zetu. Mfano
pindi unapowaona wenzio wakifanikiwa ili hali wewe unabaki kuwa masikini wa
kutupwa basi hapa ndipo huwa unapata hasira na kuanza kuuchukia umasikini
lakini kiuhakika ni kuwa usingeweza kupata hasira ya kuichukia hali hii ya
umasikini. Lakini sababu ya kukufanya uanze kuuchukia umasikini ni baada tu ya
kuona tofauti iliyopo kati yako na wengine.
3) Hutufanya tujifunze zaidi,tofauti
zilizopo baina yetu na wengine wakati mwingine huwa kama somo kwetu maana
tofauti hizi hutufanya tuanze kujihoji sana ni kwanini wengine wako hivi na
sisi tuko hivi. Mfano leo hii unapata wazo gani unapowaona watu waliofanikiwa
mbele yako, sina shaka kuwa itakuwa uwa unapata hamu ya kujifunza zaidi kutoka
kwa watu hao.
Ni muhimu tofauti ziendelee kuwepo
miongoni mwetu ili tuweze kuchagua ni wapi panatufaa, ili tuweze kubadilishana
huduma maana wote tukiwa wafanyabiashara
nani atakuwa mnunuzi tena isitoshe wote tukiwa tunauza bidhaa sawa, ingekuwaje
kama wote tungekuwa madereva na kila mtu, angelikuwa na gari lake, bila shaka
kusingekuwepo abiri kwa sababu hizo na nyingine nyingi ni dhahiri kuwa tofauti
ni lazima ziendelee kuwepo miongoni mwetu.
Ni mimi rafiki yako,
Baraka Maganga
Wasiliana nami kwa.
Simu: 0754612413 au 0652612410.
Barua
pepe: Bmaganga22@gmail.com
Tuesday, January 19, 2016
Chagua Timu Sahihi Ya Kushirikiana Nayo.
Habari ndugu msomaji wa mtandao huu wa kona ya maarifa,
ni matumaini yangu kuwa unaendelea vizuri katika kuhakikisha kuwa
unashughulikia ipasavyo yale unayo yahangaikia ili tu kujiletea mafanikio
ambayo ndio kila mtu anayoyahangaikia. Nami nikusihi kwa moyo mmoja kuwa
endelea kupambana mpaka uyatimize yale unayoyaamini kama mafanikio kwako.
Pambana pambana bila kuchoka na mafanikio utayaona tu.
Katika maisha yetu sisi
wanadamu tumekuwa tukijikuta tunaunda timu ya watu ambao tunakuwa
tunashirikiana nao mara kwa mara. Najua kila mtu atakuwa na timu ya
kushirikiana nayo yaani una watu wako wa karibu ambao mara kwa mara umekuwa
ukishirikiana nao kufanya nao mambo mbalimbali. Hili ni jambo ambalo kila
binadamu huwa analifanya kila siku na kila wakati. Sina shida na hilo ila shida
iliyopo ni aina ya watu ambao tunashirikiana nao.
Je tunawafahamu
ipasavyo hawa watu ambao tumekuwa tukishirikiana nao mara kwa mara katika mambo
yetu yawe ya muhimu na yale yasiyo ya muhimu. Kama unataka kufanikiwa maishani
hakikisha kuwa unashirikiana na watu ambao ni sahihi na munaendana nao,
sisemi kuwa lazima muwe mnaendana
kielimu, kiumri, urefu na rangi za mwili lakini jambo la msingi ni kule kuendana
kimtazamo na mawazo.
Mafanikio yanahusisha sana fikira yaaani fikira zako
ndizo hukuletea mafanikio au kuto kukuletea mafanikio. Mwenendo wa fikira zako
ndio ambao huamua wewe uwe wapi. Ndio maana kama unataka kuwa mwenye mafanikio
basi hakikisha kuwa unazichunguza kwa kiwango kikubwa sana fikira zako. Na kama
unataka kutoka kule uliko kwenda mbele zaidi yaani kwenye mafanikio basi hakikisha kuwa una badili fikira zako
kama ulikuwa na fikira mbovu kuhusu maisha, mafanikio, utajiri na umiliki mali
basi anza kuzibadili na ukishazibadili nenda mbali zaidi kwa kutafuta timu
sahihi ya kushirikiana nayo.
Ni muhimu ukatambua
kuwa ndugu msomaji mafanikio huendana sana na watu ambao unashirikiana nao.
Wazungu wana msemo usemao kuwa “birds of feather floks tugeza” kwa tafsiri sisi
tunaweza sema ndege wenye mabawa hutembea pamoja. Msemo huu unamaana sana na
kama kweli unataka kufanikiwa basi hakikisha kuwa msemo huu unakukaa kichwani
na haukutoki kamwe, yaani ufanye msemo huu kama kichochea chako cha kuelekea
mafanikio.
Msemo huu unauhalisia mkubwa sana maishani hebu
yachunguze makundi mbalimbali ya watu hata hapo mtaani kwako na kwingineko,
waangalie watu ambao huwa wanashirikiana je wanaendana au huwa hawaendani?,
waangalie walevi au watu wanaokunywa pombe huwa wanakuwa wanafahamiana na huwa
hata wana namna yao ya kuwasiliana na wewe ambaye sio mlevi unaweza ukapata
shida kuwaelewa hii ni kutokana na lugha yao, waangalie vijana wa kijiweni,
waangalie walokole, waangalie watu wanaopenda michezo n.k.
Leo hii ni ngumiu kumkuta mlokole aliekomaa kijiweni akishirikiana
na vijana hao wa kijiweni, au ni vigumu sana kumkuta mlevi amekaa na mtu
ambayehatumii pombe wala kilevi cha aina yoyote ile. Sasa unajua kwanini watu
hawa huwa wanachagua watu wanao endana nao, ni kwasababu wanajua kupitia watu hao
watapata mawazo na fikira zenye kuendana nao. Yaani watakuwa wakibadilishana
mawazo yao juu ya yale ambayo wanayafanya.
Sasa kwa kupitia mifano ya watu hawa ambao nimekuwekea
hapo juu basi nawe unaetaka kufanikiwa hakikisha unajipatia timu sahihi ya
kushirikiana nayo, timu hii itakuwa chachu ya mafanikio yako, maana utapata
mawazo mbalimbali, utapata changamoto mbalimnbali ambazo zitakufanya uwe bora
zaidi na zaidi na uweze kusonga mbele.
Kama kweli unataka kufanikiwa hakikisha unakuwa na fikira
chanya na fikira chanya ndio utazipata kutokana na watu ambao unashirikiana
nao. Watu wapo tu shida ni kuwa wewe ukoje kama unamtazamo chanya basi utafanya
mambo chanya na utapata watu wenye fikira chanya hivyo ni wewe tu na sio kuwa
huwezi kupata watu, watu wapo tu.
Ni mimi rafiki yako,
Baraka Maganga
Wasiliana nami kwa.
Simu: 0754612413 au 0652612410.
Barua
pepe: Bmaganga22@gmail.com
Friday, January 15, 2016
Huwezi Kufanikiwa Kama Utashindwa Kuepuka Jambo Hili.
Habari za wakati huu ndugu mpendwa msomaji wa makala za
mtandao huu wa kona ya maarifa, ni matumaini yangu kuwa hu mzima wa afya na
unaendelea vizuri katika kuhakikisha kuwa unayatekeleza yale ambayo umepanga
kuyatekeleza. Vizuri endelea kupigana mpaka yale unayoyataka yamekamilika.
Wakati unaendelea kupambana, ili kuhakikisha kuwa
unayatekeleza yale unayoyataka basi nakusihii epuka kitu hiki kimoja kama kweli
unataka kufanikiwa katika maisha yako.jambo lenyewe ni kukosa ubunifu. Nimeamua kukuandikia hili ndugu msomaji ili uweze
kuelewa madhara ya jambo hili. Na hili nimeamua kuliandika kutokana na ongezeko
la tabia hii miongoni mwa watu wengi, na watanzania tukiwa ndio tunao ongoza
kwa tabia hii ambayo kwangu naiona kama tabia isiyofaa kabisa kuigwa wala
kufuatwa na jamii.
Tabia yenyewe ni ya kukosa ubunifu miongoni mwetu. Ukitazama
shughuli nyingi sana za watanzania ni shughuli ambazo zimwekosa ubunifu, kabisa
angalia sanaa zetu, biashara n.k, ni shughuli chache sana zenye kubeba ubunifu
ndani yake. Watu siku hizi hawaangaiki kubuni kitu chochote badala yake
wamekuwa ni watu wa kuhamisha mambo kama yalivyo kutoka walikoyatoa na kuyaleta
kwetu,(coping and pasting), na kwa kuwa watu pia ubunifu umewapiga chenga basi
nao huwa wanakubali kuamini mambo hayo hata kama wanajua hayaendani na sisi. Kutokana
na ukosefu wa ubunifu ndio maana leo hii kumekuwa na tabia kubwa sana ya mambo
ya kuigana igana tu na matokeo yake hakuna jipya linalo fanyika bali ni yale
yale.
Ikiwa unataka kufanikiwa katika dunia ya leo basi
hakikisha kuwa unakuwa mbunifu. Dunia ya leo imejaa ushindani wa hali ya juu,
hii ikimaanisha kuwa kwa kila unalolifanya unaweza usiwe peke yako badala yake
mtakuwa wengi. Sasa kama ikitokea mmekuwa wengi basi jambo la msingi la wewe
kufanya ni kutafuta namna ya pekee ya kuweza kulifanya jambo lile ambalo
litakutofautisha wewe na wengine. Kama ukishindwa kufanya hivyo basi tambua
kuwa hautopata mafanikio makubwa katika yale unayoyafanya.
Chukulia mfano wa wachezaji Ronaldo na Messi, unajua ni
kwa nini wanakuwa wachezaji bora wao tu kuliko wengine?, je wao ndio wachezaji
pekee duniani kwamba hakuna wenzao. Ukiwaangalia wao kama wao hawana tofauti na
wachezaji wengine maana wao wana miguu miwili kama wenzao wapo watu duniani
ambao wanacheza namba kama zao lakini nini kinachofanya wao wafanikiwae kuliko
wenzao, hakuna kingine bali ni ubunifu ambao wanao. Ubunifu wao ndio
unawatofautisha wao na wenzao na kuwafanya waonekane bora kuliko wao. Wote wanafunga
magoli, wanapiga chenga na bwebwe zingine zote unazozijua katika mpira lakini
nini kinawatofautisha na wengine? Ni ubunifu walio nao ndio maana unakuta
wanamagoli mengi kuliko wenzao. Wamebuni mbinu tofauti za kucheza mpira ambazo
wenzao hawana muda wa kuzibuni ndio maana wanakuwa bora.
Tukirudi katika biashara za hapa kwetu Tanzania, ni
biashara bora kwa kiasi chake lakini ni biashara ambazo zimejaa maswala ya
kuigana tu hakuna jipya. Leo hii kumezuka maswala ya biashara za mtandao sasa
kila mtu anataka afanye, achilia mbali maswala hayo, kutokana na maendeleo ya
watu kutumia mitandao ya kijamiii watu wamekuwa na uwezo wa kutangaza biashara
zao katika mitandao hiyo, lakini angalia namna ya utangazaji wao, kila mtu
anapiga picha ya bidhaa na kuipost kisha ataandika tu kwa anae hitaji
mawasiliano haya hapa, anatoa namba yake pale. Kama sio hivyo utasikia, jipatie laba kali, tisheti
n.k tunakuletea ulipo. Sasa biashara hizi sio kuwa nazipinga au kuwacheka wanaozifanya
lakini nalo hoji ni kuwa ni lazima wote tuandike matangazo sawa hakuna anaeweza
kubuni namna nyingine ambayo itamtofautisha na mwingine.
Angalia leo kuna makundi kibao katika mitandao mbalimbali
makundi haya huanza kwa namna nzuri sana lakini kutokana na kuwa wote
tumeathiriwa na namna moja ya kufikiri na hivyo tukakosa ubunifu, utakuta mtu
kaanzisha kundi kaliita jina la kibiashara kabisa lakini ukiingia kwenye kundi
hilo unakutana na stori za mapenzi, kwa kuwa ameona kuwa stori hizo ndizo
zinazopendwa na kufuatiliwa na kuwapatia watu wengi sana umaarufu mkubwa. Angalia
leo hii ni makundi mangapi yanazungumzia mapenzi, hakika yatakuwa mengi sana na
yote yanaandika kitu kile kile hii inaonyesha kuwa hatuna ubunifu wa
kutuwezesha watu kuweza kufanya kitu cha
tofauti.
Kimsingi ni vyema ukatambua kuwa katika dunia ya sasa,
yenye kujaa ushindani wa hali ya juu huitaji kufanya kitu cha tofauti sana ila
unatakiwa ufanye kitu kwa utofauti na hiyo ndio tabia ya watu walio fanikiwa. Sio
kuwa wanafanya vitu tofauti bali wanafanya vitu kwa utofauti, na utofauti huo
ndio ujulikanao kama ubunifu. Na ndio
huwafanya waonekane watu wa tofauti sana duniani.
Ni mimi rafiki yako,
Baraka Maganga.
Wasiliana nami kwa.
Simu: 0754612413 au 0652612410.
Barua
pepe: Bmaganga22@gmail.com.
Wednesday, January 13, 2016
Ifahamu Njia Ya Kutumia Ili Kupanga Shughuli Zako Katika Vipaumbele.
Habari za wakati huu ndugu msomaji wa mtandao huu wa kona
ya maarifa ni matumaini yangu kuwa hu mzima wa afya na unaendelea vizuri katika
kuyatekeleza majukumu yako ya kila siku. Nami nasema vizuri endelea kupambana
mpaka uyatekeleze yale uliyokwisha kujiwekea.
Wakati unaendelea kupambana ili kuhakikisha kuwa
unafanikiwa, wapo watu ambao wanahisi kuwa wanashughuli nyingi sana na hawajui
ni ipi shughuli waanze nayo. Ikiwa unaona au kuhisi kuwa unashughuli nyingi
sana na haujui ni ipi sahihi kuanza nayo basi hapa nakuletea njia sahihi ya
kutumia ili uweze kujua ni shughuli ipi ya kuanza nayo, njia yenyewe inaitwa ABCDE. Hii ndiyo njia yetu ya kuweza
kukusaidia kupanga shughuli zako. Ntaifafanua njia hii kama ifuatavyo:-,
Shughuli
A-
shughuli ya kuwa katika kundi hili inapaswa kuwa shughuli ya muhimu sana, hapa
kinapaswa kuwa kitu cha muhimu sana ambacho ni lazima ukifanye au kifanyike. Shughuli
ambayo inapaswa kuwa na jina la A ni lazima utambue kuwa ni shughulia ambayo
isipofanyika basi ina madhara makubwa sana. Mfano wewe ni mfanyabiashara na
unaitegemea biashara husika katika kuendesha maisha yako basi hiyo shughuli
ndio inapaswa kuwa hapo, maana kwanza ni muhimu, lazima ufanye ili uishi na mwisho
ukiacha kufanya basi madhara yapo.
Shughuli
B-
hii ni shughuli ambayo inatakiwa uifanye, shughuli ambayo inatakiwa iwepo hapa
ni ile ambayo pia isipofanyika ina madhara lakini sio muhimu sana kama ilivyo
katika shughuli A. mfano kama umeamua kuanzisha program ya kufanya mazoezi kila
siku asubuhi kabla ya kuelekea katika shughuli zako ni muhimu ukafanya hivyo
ingawa kuto kufanya kuna madhara ya kuwa afya yako itadhoofika lakini sio
muhimu sana maana wapo ambao hawafanyi zoezi na afya zao ni nzuri tu.
Shughuli
C-
katika kundi hili linapaswa kuwa na shughuli ambayo ni vizuri ifanyike lakini
haina madhara yoyote. Mfano kuamua kwenda kuwatembelea ndugu mahali fulani kama
vile dada, kaka, shangazi, bibi au babu, ukitazama vizuri swala la kwenda kuwatembelea
ndugu mara kwa mara ni vizuri lakini hakuna madhara yoyote makubwa. Au shughuli
nyingine ni kama vile kwa mfanyakazi ambae anataka kwenda kunywa chai au kula
chakula pahali fulani na wafanyakazi wenzake, ni vizuri kufanya hivyo lakini
kuto fanya hivyo hakuna madhara makubwa. Au kwa yule aliyeoa ni vizuri kupiga
simu kuulizia leo mkeo kapika nini lakini hakuna madhara yoyote usipo fanya
hivyo. Hivyo basi shughuli zote zenye kufanana na hizo zinapaswa kuwa hapa
katika kundi hili.
Shughuli
D-
hapa pana husisha shughuli yoyote ile ambayo unaweza kumwachia mtu
aifanye. Ni muhimu utambue kuwa yakupasa
uyaache yale ambayo yanaweza kufanywa na mtu fulani ili ayafanye yeye badala
yako. Hii itasaidia nini haswa?, hii itakusaidia wewe kuokoa muda ambao
ungeupoteza kufanya jambo ambalo linaweza kufanywa na mtu mwingine. Mfano mama
mwenye binti zake wakubwa nyumbani anapaswa kuwaachia shughuli kama vile za
usafi wa nyumba na yeye akawahi katika shughuli zake kama vile biashara zake.
Shughuli
E-
hapa ni shughuli ambazo unaweza kuamua kutokuzifanya kabisa. Hizi ni shughuli
ambazo unaweza kuamua kuzifanya au kutokuzifanya na hazina madhara yoyote. Mfano
shughuli ya kujibu kila jumbe au kila
unachokiona katika makundi ya whatsapp.
Mara nyingi sana watu huwa tunakabiliwa na changamoto
pale ambapo tunapaswa kufanya jambo fulani, hii ni kutokana na kuwa na shughuli
nyingi sana ambazo tunaamini kuwa zote ni za muhimu, utakuta mtu anataka kwenda
kwenye biashara, mara kufanya zoezi, mara kwenda kumtembelea shangazi n.k. huyu
ni mtu mmoja ambae anataka kuyafanya yote haya na hajui aanze na lipi. Kama unakubwa
na shida hizo basi dawa ndiyo hiyo nimekupatia.
Ni mimi rafiki yako,
Baraka Maganga
Wasiliana nami kwa.
Simu: 0754612413 au 0652612410.
Barua
pepe: Bmaganga22@gmail.com
Monday, January 11, 2016
Zifahamu Kauli Kumi (10) Unazozitumia Na Zinakufanya Usifanikiwe.
Habari za wakati huu ndugu msomaji wa mtandao huu wa kona
ya maarifa ni matumaini yangu kuwa umeshaianza siku yako vema na unaendelea
kupambana ili kuhakikisha kuwa siku yako ya leo mpaka inaisha unakuwa
umejisogeza vya kutosha katika kuyatekeleza malengo yako. Nami nakusihi
usichoke maana mafanikio yanahitaji uvumilivu wa hali ya juu hata kama mambo
hayajaenda sawa wewe usijali endelea kupambana tu na mafanikio utayaona.
Leo kuna jambo nataka kukushirikisha ndugu msomaji wa
mtandao huu, tumekuwa tukiamini kuwa maneno huumba, au wengine husema kauli
huumba tukiwa na maana kuwa kadri tujisemeshavyo wenyewe juu ya maisha yetu ndivyo maisha yetu huwa. Sasa
kutokana na hili ndio maana nimekuletea kauli kumi ambazo watu wamekuwa
wakizitumia na zimekuwa zikiwafelisha na kuwaweka mbali na mafanikio kauli hizo
ni kama ifuatavyo:-,
Sikuzaliwa au kukulia katika familia
bora,
kuna watu ambao huamini na kuhararisha kutokufanikiwa kwao na kutozaliwa au
kuto kukulia katika familia bora. Hizi ni kauli ambazo hazina maana yoyote
katika dunia ya leo maaana mafanikio ni wewe na sio familia uliyokulia, na kama
wewe unaona hilo ni sahihi ni wangapi kwani ambao wamefanikiwa japo kuwa
hawajatoka familia bora?, acha mara moja kauli hizi badala yake anza kufikiria
utafanyaje ili ufanikiwe ijapokuwa hujatoka familia bora hilo ndilo jambo la
msingi.
2. Sikuzaliwa upande sahihi,
hawa ni waleambao huona kuwa kutokana na wao kuzaliwa bara fulani, au nchi fulani
ni mkosi kwao, maana huamini kuwa bara au nchi husika waliyomo haiwaruhusu
kufanikiwa. Ni kauli za kijinga na ambazo hutumiwa na watu ambao hawajafanikiwa
ndio husema bora kuzaliwa mbwa ulaya kuliko mtu afrika, hizi ni kauli za ajabu
sana, kwani ni waafrika wangapi wapo afrika na wamefanikiwa, ni watanzania
wangapi wanamafanikio hapa hapa Tanzania, ni wakenya, waganda n.k wangapi wenye
mafanikio ndani ya nchi zao?. Acha kauli zisizo za msingi.
3. Sina elimu ya kutosha,
hii ilikuwa na umuhimu enzi zile za zama za kati za mawe lakini sio katika
dunia ya sasa ya taarifa. Nani aliyekuambia mafanikio ni kutokana na elimu yako
tu?, wangapi wanamafanikio makubwa na hawana hata digrii, masters, wala hizo
phd ambazo wewe unaamini lazima uwe nazo ndizo zitakufanya ufanikiwe. Chukulia mfano
wa mafanikio ya msanii Diamond na msakata kabumbu Mbwana Samatta, je wanaelimu kiasi gani?. Jibu
baki nalo.
4. Hayo ni mambo yako sio yangu,
kauli kama hizi ndizo huwafanya watu wakose fursa. Utamkuta mtu analetewa wazo
la kibiashara ambalo tayari ni fursa kwake lakini utamsikia aa bwana ee hayo ni
mambo yako sio yangu. Sasa endelea hivyo hivyo na utaendelea kukosa fursa siku
hadi siku.
5. Sina muda wa kutosha,
wewe kila siku muda haukutoshi, wewe ni nani na unafanya nini mpaka muda
usikutoshe kila siku?, je unataka upatiwe masaa 70 ndani ya siku moja? Kwanini wewe
tu ndio muda haukutoshi? Mbona wengine masaa 24 yanamtosha. Jifunze kutumia
muda ulopewa vizuri.
6. Sina pesa za kutosha,
unafikiri pesa inatosha kwa kukaa nayo tu? Au kwa kuiweka tu ndani na
kuishangaa au benki?, acha kufikiri pesa
itakuja kukutosha bila kuizungusha, jifunze kuizungusha hiyo pesa ndipo
itakutosha.
7. Sifahamiani na watu sahihi, ni
kweli hufamiani na watu sahihi kutokana na matendo yako na ndio maana huwezi kuwapata
watu sahihi wa kukusukuma uende mbele. Kama unataka kupata kushirikiana na watu
sahihi anza kufanya mambo yanayoendana na hao watu ambao kwako ni sahihi.
8. Sina mtandao wa watu,
hauna mtandao wa watu wa kushirikiana nawe kutokana na wewe mwenyewe ulivyo. Mtandao
wa watu wa kushirikiana nao unakuja kutokana na kile ambacho unakifanya na
kutokana na ushirikiano wako na watu wengine. Unashirikiana na nani haswa na
huyo unayeshirikiana nae je? anamtandao au?.
9. Mke wangu hanisaidi, ni
kweli mke wako hakusaidi lakini wewe kama wewe umechukua juhudi gani
kuhakikisha kuwa wewe kama wewe unapigana vilivyo katika kuhakikisha kuwa
unasimama wewe kama wewe?, je mafanikio
yako yanamtegemea mke wako tu?, kama asingalikuwepo ungalifanyaje?, acha
kutegemea tegemea bila msingi badala yake jifunze kusimama mwenyewe muda mwingine.
10. Nina watoto wengi wa kulea,
kama ulijua kuwa watoto wengi wanakufanya usifanikiwe kwanini umekuwa nao?. Na je
ni kweli kwamba bila kuwa na watoto wengi ungefanikiwa au ni visingizio?, je
tukiwachukua hao watoto na tukakuacha mtupu utafanikiwa?
Kimsingi kauli hizi kumi kwa maneno
mengine tunaweza kuziita kama visingizio ambavyo mtu huwa navyo, na hii ni
hatari sana maana visingizio havikufanyi kuwa mwenye mafanikio bali vinazidi
kukurudisha nyuma. Hivyo basi uamuzi ni wako kuendelea na visingizio na sababu
sababu za kuto kufanikiwa kwako ambzao zitazidi kukufanya usiwe na mafanikio au
uziache na kuwa mwenye mafanikio.
Ni mimi rafiki yako,
Baraka Maganga
Wasiliana nami kwa.
Simu: 0754612413 au 0652612410.
Barua
pepe: Bmaganga22@gmail.com
Saturday, January 9, 2016
Sababu Sita (6) Za Kwanini Watu Hawajiwekei Malengo.
Habari za leo ndugu msomaji wa mtandao huu wa kona ya
maarifa ni matumaini yangu kuwa hu mzima wa afya na unaendeleo kupambana
vilivyo katika kuhakikisha kuwa unajiletea mafanikio makubwa maishani mwako.
Nami nakusihi ndugu msomaji wa mtandao huu kuwa endelea kupambana, usichoke
hata siku mpaka uhakikishe kuwa unajipatia mafanikio makubwa, ambayo umekwisha
jiwekea.
Ukiwa unaendelea kujishighulisha na shughuli zako za kila
siku basi leo nakuletea kitu kingine ambacho unapaswa ukifahamu vyema. Kama kichwa cha makala kinavyosema kuwa sababu za
kwanini watu huwa hawajiwekei malengp maishani. Tumekuwa tukisisitizana na
kuambiana mara nyingi sana juu ya umuhimu wa kuweka malengo, lakini ukweli ni
kwamba ni watu wachache sana kati ya wengi ambao wamekuwa na utamaduni wa
kujiwekea malengo. Na walio wengi wamekuwa hawajiwekei malengo, sasa kwanini
watu hawa huwa hawajiwekei malengo maishani, zifuatazo ni sababu za kwanini
watu hawajiwekei malengo:-,
Hawako makini,
sababu moja wapo ya kwanini watu hawajiwekei malengo ni kutokana na sababu kuwa
hawapo makini maishani. Mtu makini na anayetaka kufanikiwa kwa hali na mali
lazima ajiwekee malengo. Lakini kutokana na ukosefu wa umakini miongoni mwetu
tumekuwa tukiishi hivyo hivyo bila malengo
.
2. Hawajayakubali majukumu yao,
kama mpaka sasa hujathubutu hata kujiwekea malengo basi tambua kuwa bado
hujataka kuyavaa majukumu yako. Yaani watu ambao bado hawajajiwekea malengo ni
wale ambao bado wanahisi kuwa yupo mtu fulani maishani ambae ndiye yupo kwa
ajili ya kusubiri kufanyiwa kitu fulani jambo ambalo kiukweli ni kujidanganya.
Hivyo basi ukosefu wa ile hali ya kuvaa majukumu ndio kimekuwa kikwazo cha watu
kujiwekea malengo.
3. Hawatambui umuhimu wa kujiwekea malengo,
watu wamekuwa hawajiwekei malengo kwa sababu hawajui umuhimu wa kujiwekea
malengo. Inaonekana kuwa miongoni mwa watu wengi sana hawana uelewa juu ya
maswala haya ya kujiwekea malengo ndio maana wamekuwa hawajiwekei malengo
maishani mwao. Watu hawaoni umuhimu wowote wa kujiwekea malengo ndio maana
wamekuwa hawajiwekei, lakini naomba niseme kuwa hii ni kosa kubwa sana ambalo
watu hulifanya, nasema hivyo kwa sababu ni vyema kila mtu akatambua umuhimu wa
kuweza malengo na akijua umuhimu atakuwa amejikomboa kwa kiwango kikubwa.
4. Hawajui ni vipi watapanga/ kuyaandika
malengo yao, sababu nyingine ambayo inawafanya watu
wasijiwekee malengo ni kutokana na ukweli kwamba hawajui ni vipi wajiwekee
malengo. Hii nadhani ndio sababu namba moja ya kwanini watu hawajiwekei malengo
maishani, yaani hawaweki malengo kwa sababu hawajui watafanyaje. Kama hujui
mpaka leo basi jua kuwa upo katika hatari.
5. Wanaogopa kukosolewa/ kukataliwa,
uoga umekuwa ukichangia sana miongoni mwa watu, na imekuwa sababu inayofanya
watu washindwe kujiwekea malengo, watu wamekuwa wakiogopa kujiwekea malengo kwa
kuwa wanaogopa kuwa endapo wakimwonesha mtu malengo yake atakosolewa sana hivyo
kutokana na woga huu basi unamfanya arudi nyuma na kukaa bila kuweka malengo.
6. Wanaogopa kushindwa,
watu wengi hawaweki malengo kwa kuwa wanaogopa kushindwa yaani anaogopa kuwa
itakuwaje nikiweka malengo alafu nisiyatimize hivyo kutokana na kuogopa huko
katika kushindwa basi anakaa tu na kutokujiwekea malengo.
Ikiwa unataka kufanikiwa zaidi na zaidi
ni muhimu ukatambua kuwa malengo ni kitu muhimu sana tena sana, malengo ni dira
katika maisha yako. Ikiwa hujajiwekea malengo basi nishakuwekea sababu sita za
kwanini hujafanya hivyo. Kupitia sababu hizo unaweza ukaelewa ufanye nini ili
kujiwekea malengo. Mfano umeshajua sababu moja wapo inayokufanya usijiwekee
malengo ni kuwa hujayakubali majukumu, sasa nini cha kufanya ni kuyavaa
majukumu kisha baada ya hapo utapata uwezo na uelewa wa ni vipi ujiwekee malengo.
Ni mimi rafiki yako,
Baraka Maganga
Wasiliana nami kwa.
Simu: 0754612413 au 0652612410.
Barua
pepe: Bmaganga22@gmail.com
Subscribe to:
Posts (Atom)