Friday, January 29, 2016

Lazima Uwe Tayari Kufanya Jambo Hili Katika Safari Yako Ya Kuelekea Mafanikio.


Habari za wakati huu ndugu msomaji wa mtandao huu wa kona ya maarifa ni matumani yangu kuwa hu mzima na unaendelea vizuri katika kupambana ili kuhakikisha kuwa

Thursday, January 28, 2016

Fahamu Leo Kuwa Maneno Yana Nguvu Sana Katika Maisha Yako.

Habari za wakati huu ndugu msomaji wa mtandao huu wa kona ya maarifa ni matumani yangu kuwa hu mzima na unaendelea vizuri katika kupambana ili kuhakikisha kuwa unapata kile unachokitafuta katika maisha. Kwa kuwa lengo la mtandao huu ni kuhakikisha kuwa unapata vitu vya kukusukuma mbele zaidi katika kuelekea safari yako hiyo ya mafanikio, basi nasema pambana endelea kupambana bila kuchoka hata pale unapohisi umechoka jilazimishe maana kuridhika baaada ya hatua chache huleta anguko.

Najua umekuwa ukupambana sana katika kuhakikisha kuwa unafanikisha mambo yako lakini kuna wakati ukikaa na kupiga tathimini unajikuta ukitamani kukata tamaa hii ni baada ya kuona au kupata matokeo ya tathimini yako  na hapo ndipo wengi huwa tunapatwa na hofu ya kuacha na mara nyingi sana huwa tunaanza kuona ni kama hatupigi hatua hivyo basi tunatamani kuachana na harakati zetu ambazo tumekuwa tukizianzisha na kuamini kuwa zitakuwa na msaada kwetu. Unatamani kuacha nakuona unasoma hii makala na huku unasema dah yaani sioni matokeo yoyote, niliambiwa hivi na vile, nilisoma hivi na vile lakini sioni matokeo yake, naacha bwana.








Kabla hujafikiria kufanya kitu hicho unachotaka kufanya nataka ujichunguze sehemu hii moja, yachunguze maneno yako. Kabla hujafikiria kufanya uamuzi wa kuacha kufanya jambo fulani kwa kuwa tu hujapata matokeo mazuri yachunguze maneno yako,  narudia tena yachunguze maneno yako. Unajua binadamu tuna namna mbili za kuongea, nakuona unashangaa kusikia namna mbili za kuongea, namaanisha kuwa tunakule kuongea kwa kawaida ambapo tunaongea na wenzetu huku kumezoeleka na ni maarufu lakini aina ya pili ni ile ya kujiongelesha wenyewe, yaani  kuna muda huwa unajikuta uwapo mwenyewe kuna maneno unayojiongelea mwenyewe sasa maneno haya ndio nayo taka uyachunguze.
Jiulize mwenyewe hapo ulipo je kauli unazojisemesha mwenyewe ni hasi au chanya, nakuona unasita kutoa jibu kwa kuwa unajua ni hasi. Wengi tumekuwa hatujui nguvu iliyopo katika maneno yetu ambayo tumekuwa tukijisemesha mara kwa mara na ndio maana tumekuwa tukihangaika kuchunguza mchawi wa maisha yetu kumbe sisi wenyewe ndio tunao jiloga. Unajiloga kwa maneno yako mwenyewe alafu unajikuta unalalama eti nalogwa na ndugu zangu hawataki nifanikiwe kabisa. Dah wewe, nani asiyetaka ufanikiwe wewe au wao?, jibu unalo mwenyewe mpaka hapo.

Pengine unajiuliza sasa mbona mimi sielewi ni kauli gani sasa, sawa mimi nipo kukuletea hizo kauli, mara ngapi umekuwa ukijisemea kuwa wewe unamikosi, nuksi au gundu. Ndio umekuwa ukijiambia ukisema unamikosi, gundu au nuksi maana yake huwezi kufanikiwa sasa kwanini unataka kufanikiwa ikiwa kila siku unajisemesha mwenyewe kuwa hauwezi kufanikiwa. Huoni kuwa unafanya kazi ya kuchanganya maji machafu kwenye maji masafi alafu unategemea maji masafi yaendelee kuwa masafi. Eti unataka kuacha kufanya mambo ya kukusogeza mbele kisa unamikosi, na ukiamini na kujisemesha kuwa unamikosi kweli utakuwa nayo tena mingi haswa. Acha kujisemesha na kujitazama kama mtu mwenye mikosi, gundu, na nuksi. Acha mara tu baada ya kusoma makala hii.

Mara ngapi umekuwa ukisalimiwa asubuhi unaambiwa habari ya asubuhi ndugu unajibu aa bora kumekucha, au dah bora ya jana, hivi unajua maana ya hayo maneno unayoyasema. Unayasema maneno hayo alafu akilini mwako unawaza kuwa biashara yako itakwenda sawa. Nani kakudanganya wewe acha kujidanganya, ukisema bora kumekucha maana yake haukutaka kukuche sasa unaendeleaje na shughuli kama hautamani kukuche?, ukisema dah bora ya jana maana yake siku ya leo ni ya ovyo sasa unategemea vipi kudharisha katika siku mbovu?, anza siku yako na kauli nzuri na mafanikio utayaona
.
Nakuona kila ikifika ijumaa unajifanya mzungu eti “thanks God it is Friday” ukimaanisha asante mungu kwa kuwa leo ni ijumaa. Unajua tafsiri yake hapo tafsiri yake ni kuwa siku zote zilikuwa mbaya kwako ndio maana unafurahia kuiona ijumaa. Sasa kwanini utake kufanikiwa jumatatu wakati kwako ni mbaya? Au alhamisi wakati ilikuwa mbayas?
Kuwa makini na kauli unazojinenea mwenyewe maana mnamo maneno mna nguvu sana, maneno huumba hilo waswahili waliliona na sio kuumba tu, maneno yanaamua maisha yetu ya sasa na baadae.hivyo basi kuwa makini sana tena sana juu ya maneno yako kama kweli unataka kufanikiwa. TWENDE SOTE.


Ni mimi Baraka Maganga, rafiki na mwalimu wako.  Wasiliana nami kwa nambari za simu 0754612413/0652612410. Au kwa barua pepe ambayo ni Bmaganga22@gmail.com.  

Wednesday, January 27, 2016

Hivi Ndivyo Mambo Yatakavyokuwa Baada Ya Wewe Kufanya Kitu Hiki Kimoja.


Habari za wakati huu ndugu msomaji wa mtandao huu wa kona ya maarifa ni matumaini yangu kuwa hu mzima wa afya na unaendelea kupambana kwa hali na mali ili tu uweze kufanikisha yale ambayo umekuwa ukiyahangaikia mara kwa mara. Vizuri endelea kupambana naama hakuna kitu cha bure hapa duniani, maana hata miujiza huja kwa wale ambao huwa wanakuwa wakiitafuta miujiza hiyo. Sio waliokaa tu wakisubiri miujiza hivyo nakusihii endelea kupambana ndugu msomaji wa mtandao huu.






Mafanikio yanahitaji ahadi ndugu mpendwa msomaji wa makala hii. Hili ni jambo ambalo ningependa uweze kulifahamu kuanzia sasa,kuwa mafanikio yanahitaji ahadi. Yaani baada ya kujiwekewa malengo unapaswa sasa kuweka ahadi juu ya utekelezaji wa malengo yako. Pengine umekuwa ukijiwekea ahadi bila kujua ahadi ni kama pale unaposema kuwa nataka kupunguza uzito likiwa kama lengo lako sasa pale unaposema lazima kila siku nifanye mazoezi kwa muda wa nusu saa, tayari hapo unakuwa umejiwekea ahadi katika maisha yako. Au unasema nataka kuamka kila siku saa kumi na moja alfajiri ili niweze kufanya shughuli zangu za ndani kabla ya kwenda katika mihangaiko yangu, kuamka saa kumi na moja ni ahadi tayari uliyokwisha jiwekea katika maisha yako.

Tumekuwa watu wa kujiwekea ahadi nyingi nyingi tena ahadi zingine zinakuwa kubwa na zenye kututisha kiasi kwamba tunaweza kufikiri kuwa hatutoweza kutimiza ahadi hizo. Kimsingi ahadi na malengo ni vitu ambavyo vinaenda sambamba na vinaweza kukupatia shida katika kuvitofautisha lakini tofauti ni kuwa malengo yanaanza alafu ndio ahadi hufata. Sasa kwa kuwa ahadi ni hatua moja wapo katika kuyaelekea mafanikio basi ni vyema ukatambua kuwa yafuatayo ni mambo ambayo yatakukumba baada ya kuwa umejiwekea ahadi zako wewe mwenyewe:-

1.    Vikwazo vitaibuka, baada ya kuwa umeshajiwekea ahadi zako vikwazo vitaibuka sana tena vingi kuliko unavyodhani. Vitaibuka vikwazo vya aina mbili ambavyo ni vikwazo vya nje na vya ndani. Vikwazo vya nje ni vile ambavyo vitatokana na wale watu wanaokuzunguka kama vile marafiki, ndugu au hata wazazi, ambao wanaweza kukuzuia wewe katika kuweza kutekeleza ahadi yako, zinaweza zikawa kauli zao juu ya ahadi yako au hata kukucheka na kukupinga zaidi na zaidi. Vikwazo vya ndani ni vile ambavyo unajiwekea mwenyewe kama vile uvivu, kukosa umakini, kupuuzia ahadi yako n.k. hivyo vikwazo vyote hivi visikutishe katika kuweza kuishikiria ahadi yako na hatimaye kuweza kuitekeleza ipasavyo.

2.    Utafanya makosa, katika kuelekea kutekeleza ahadi yako utafanya makosa kadha wa kadha, makosa haya yapo ili tu kukufunza. Kama unataka kufanikiwa ni lazima uwe na mtazamo tofauti juu ya makosa unayoyafanya. Kama kweli unataka kusonga mbele katika safari yako ya mafanikio sasa ni wakati wa kubadili mtazamo wako katika makosa unayoyafanya. Amini kuwa makosa yapo tu ili kuweza kukufunza na sio kingine. Hivyo basi usirudi nyuma katika kuitekeleza ahadi yako uliyojiwekea, makosa yasikutishe bali jifunze jifunze kutokana na makosa.


3.    Utavunjwa moyo, hili nalo litakukumba kwa kiasi kikubwa na hasa kitakacho kuvunja moyo ni pale utakapo kuja kujikuta umefanya makosa mengi na pale utakapo ona kuwa unakumbwa na vikwazo vingi sana. Mambo haya yote yanaweza kukuvunja moyo  kwa kiasi kikubwa sana, lakini kwa wewe unae yasaka mafanikio kamwe usivunjike moyo bali wewe endelea kuishikiria ahadi yako.

Tambua kuwa haya yote ni majaribu ambayo dunia itakuwekea ili kukupima ni jinsi gani uko makini juu ya ahadi yako. Mara nyingi watu wengi hutamani kuachana na ahadi zako, lakini wewe unaye yasaka mafanikio hutakiwi, hutakiwi kukata tamaa kamwe. Kama alivyosema bwana winstone Churchill “never never never give up” au kama alivyosema bwana james .J. Gorbelt “you become a champion by fighting one more round, when things are tough you fight one more round”. Yaani unakuwa mshindi baada ya kupambana hatua moja zaidi na zaidi hata kama mambo yakiwa magumu pambana hatua moja zaidi.
Twende sote.

Ni mimi rafiki yako,
Baraka Maganga
Wasiliana nami kwa.
 Simu: 0754612413 au 0652612410.
Barua pepe: Bmaganga22@gmail.com


Tuesday, January 26, 2016

Ni Muda Wa Kuachana Nazo Sasa

.
Habari za wakati huu ndugu msomaji wa mtandao huu wa kona ya maarifa ni matumaini yangu kuwa hu mzima wa afya na unaendelea kupambana kwa hali na mali ili tu uweze kufanikisha yale ambayo umekuwa ukiyahangaikia mara kwa mara. Vizuri endelea kupambana naama hakuna kitu cha bure hapa duniani, maana hata miujiza huja kwa wale ambao huwa wanakuwa wakiitafuta miujiza hiyo. Sio waliokaa tu wakisubiri miujiza hivyo nakusihii endelea kupambana ndugu msomaji wa mtandao huu.






Je unakumbwa na wasiwasi wa kufanikiwa kutokana na historia yako ya nyuma zile kauli wanazokuambia wanaokuzunguka zinakurudisha nyuma katika hali ya kutaka kusonga mbele katika kuhakikisha kuwa unafanikiwa katika maisha yako. Je? unajua ni kwa nini kauli ulizopandikizwa kutoka utotoni  zinaendelea kukurudisha nyuma katika safari yako ya kuyaelekea mafanikio, ni kwasababu umeziamini na kuzifanya kuwa ukweli wako. Sasa jiambie mwenyewe kuwa ni wakati wa kuachana nazo sasa.

Zile imani ulizojijengea zamani ya kuwa hutofanikiwa na kuwa tajiri kwa kuwa wazazi wako ni masikini, imani ya kuwa huto fanikiwa kwa kuwa wazazi wako ni masikini, ni muda wa kuachana nazo maana hazina msingi wowote na wala hazikujengi wala kukusaidia chochote bali zinakudidimiza zaidi na zaidi badala yake wewe pambana kweli kweli hata kama unatokea katika familia masikini, na mafanikio utayaona tu, maana wapo waliokuwa kama wewe na waliotokea chini kama wewe na wakafanikiwa hivyo hilo lisikupe shide sana bali achana na hiyo imani.

Uliambiwa kuwa wewe ni mjinga na hauwezi chochote na mwalimu wako, ni wakati wa kuachana na kauli hii ambayo ulikuwa umeiamini kwa kuwa ilitoka kwa mwalimu wako na kupitia kigezo cha sifa ya ualimu basi ukaamini kuwa hauto fanikiwa fanya kama Thomas Edison ambaye pamoja na kukataliwa na walimu watatu tofauti kuwa hafai kuwa mwanafunzi wa kujifunza chochote lakini alijifunza na kuwa mwanasayansi mkubwa duniani na mpaka leo anaheshimika kama mwanasayansi mashuhuri duniani. Hii ni kutokana na sababu kuwa yeye aliachana na kauli za waalimu wake, hivyo basi hata wewe unaweza kufanya hivyo na ukafanikiwa pia, hivyo achana na kauli mbovu alizokuambia mwalimu wako.

Walikuita mbumbumbu mtaani kwenu, mtaani kwenu wewe ndio ulionekana kuwa mtoto mbumbumbu kuliko wote na ukafutwa kabisa kwenye watoto ambao wanaweza kuleta mabadiliko yoyote au kuleta mafanikio yoyote ambayo yataisaidia jamii yako na wewe ukaamini kuwa kweli hauwezi kutokana na maneno yao. Ni muda sasa wa kuachana na kauli hizo ambazo hazina msingi wowote bali ni za ukatishaji taama.

Lazima utambue kuwa  tunakuwa kadri tunavyofikiri, hata bibilia imeliandika hilo kuwa kadri ajionavyo mtu nafsini mwake ndivyo huwa. Hii inamaana kuwa wewe mwenye ndiye mwamuzi wa maisha yako yaani ni kadiri unavyojiona wewe mwenyewe ndivyo huwa unakuwa. Na biblia haijasema kadri wamwonavyo watu ndivyo mtu huwa, hilo ni jambo ambalo halijaandikwa wala kusemwa. Hivyo basi kama wamesema hauwezi kufanikiwa ni wao na sio wewe, wewe usizifuate kauli zao ambazo hazina msingi wowote bali wewe endelea kushikilia ukweli ambao unauona nafsini mwako na katika kuushikilia ukweli huu uwe ni ukweli ule ambao ni  chanya achana na kauli hasi kabisa maana hazikufikishi popote.

Kumbuka nimesema ni muda wa kuachana nazo zile kauli zote ambazo ni hasi, ni muda wa kuachana nazo maana hazina msaada kwako ila zina kudumaza na kukudidimiza zaidi na zaidi. Na kubwa zaidi juu ya kauli chanya ni kuwa haziwezi kukuletea mafanikio yoyote.

Twende sote.

Ni mimi rafiki yako,
Baraka Maganga
Wasiliana nami kwa.
 Simu: 0754612413 au 0652612410.
Barua pepe: Bmaganga22@gmail.com



Monday, January 25, 2016

Wajibika Ipasavyo Kama Kweli Unataka Kufanikiwa.


Habari za wakati huu ndugu msomaji wa mtandao huu wa kona ya maarifa ni matumaini yangu kuwa hu mzima wa afya na unaendelea kupambana kwa hali na mali ili tu uweze kufanikisha yale ambayo umekuwa ukiyahangaikia mara kwa mara. Vizuri endelea kupambana naama hakuna kitu cha bure hapa duniani, maana hata miujiza huja kwa wale ambao huwa wanakuwa wakiitafuta miujiza hiyo. Sio waliokaa tu wakisubiri miujiza hivyo nakusihii endelea kupambana ndugu msomaji wa mtandao huu.







Naamini umekuwa ukipambana sana katika kuhakikisha kuwa unafanikiwa katika yale ambayo unayahangaikia nami na kusihi uendelee kupambana maana katika mahangaiko ndiko mafanikio hutokea. Lakini lazima ujue kuwa lazima kitu hiki ukifanye kama unataka kufanuiki. Kitu hiki ni kitu muhimu sana katika maisha yetu na mafaniko kwa ujumla lakini jambo la kushangaza ni kuwa tumekuwa hatulitili maanani sana na ndio maana wengi wetu tumekuwa tukijikuta hatusongi mbele wala nini ila tunabaki pale pale au kurudi nyuma kabisa kimaisha.

Huwa unapata picha gani pindi unapoona mfanyakazi fulani katika kampuni fulani kafukuzwa kazi. Au kasimamishwa kazi kwa muda. Unapata picha gani pindi unapomwona mfanyabiashara fulani kashindwa kibiashara yaani biashara yake imekufa. Unapata wazo gani unapomwona mtu anailaumu serikali yake kwa kushindwa kwake wakati yeye ndiye aliyepaswa kufanya jambo husika. Hakika yote hayo hutokea kutokana na kukosekana kwa kitu hiki kimoja nacho ni uwajibikaji.

Maishani bila kuwajibika tambua kuwa hauto kwenda kokote kule bali utaishia pale pale. Dunia ya sasa imejaa ushindani wa hali ya juu ambao unaongezeka siku hadi siku na atakae weza kusitaimili ushindani huu ni yule tu mwenye kuweza kuwajibika ipasavyo. Kama wewe ni mfanyabiashara na unawajibika bora liende tambua kuwa hauto kwenda popote bali utaishia kufulia tu. Mfanyakazi pia ambae hutaki kuwajibika tambua kuwa utaishia tu kufukuzwa kazi yako hiyo na hatimae kuukaribia umasikini nao utakukaribisha vizuri sana kuliko unavyodhani.

Leo hii takwimu zinaonyesha kuwa kati ya biashara mia moja zinazo anzishwa leo baada ya miaka kumi ni biashara chini ya ishirini ndizo huwa zimekuwa. Hii ni kutokana na uwajibikaji mbovu wa wafanyabiashara husika. Wafanyabiashara hawa wamekuwa hawahangaiki katika kutafuta taarifa sahihi kabla ya kuzianzisha biashara zao na vile vile wamekuwa wagumu wa kuendelea na utafiti baada ya kuanzisha biashara zao, hivyo hata yakitokea mabadiliko wao hawashituki wala nini. Bali huendelea kufanya biashara zao kwa mazoea na matokeo yao hujikuta wamefulia maana hujikuta hawapati wateja. Hii ni kutokana na uvivu ulio letwa na kuto taka kuwajibika kwao na ndio maana wanajikuta wameanguka.

Ukiwa mfanyakazi unajisikiaje pale unapoambiwa tunakuwajibisha kutokana na utendaji wako mbovu angalia leo hii ni watu wangapi wamesimamishwa kazi toka uongozi wa awamu ya tano uingie madarakani na wote sababu zimekuwa zikionekana ni uwajibikaji mbovu na mengine, lakini kubwa ni uwajibikaji mbovu ambao huwapelekea wafanye mambo kiholera holera na matokeo yake ni kuja kuwajibishwa.

Kama unataka kufanikiwa hakikisha unayavaa majukumu yako usisubiri mazingira yaje ya kushitaki na kukuwajibisha vikali. Au usisubiri kufulia kukuwajibishe, ukiwa mfanyabiashara usisubiri anguko la biashara likuwajibishe, mfanyakazi usisubiri kuwajibishwa na bosi wako bali vaa majukumu yako mwenyewe na mafanikio utayaona tu. Ikiwa unasubiri kuwajibishwa basi sahau kuhusu mafanikio na usilizungumzie tena neno hilo.
Ni mimi rafiki yako,
Baraka Maganga
Wasiliana nami kwa.
 Simu: 0754612413 au 0652612410.
Barua pepe: Bmaganga22@gmail.com




Thursday, January 21, 2016

Furahia Vitu Hivi Wala Usilaumu Sana Juu Yake.

Habari za wakati huu ndugu msomaji wa mtandao huu wa kona ya maarifa ni matumaini yangu kuwa hu mzima wa afya na unaendelea kupambana kwa hali na mali ili tu uweze kufanikisha yale ambayo umekuwa ukiyahangaikia mara kwa mara. Vizuri endelea kupambana naama hakuna kitu cha bure hapa duniani, maana hata miujiza huja kwa wale ambao huwa wanakuwa wakiitafuta miujiza hiyo. Sio waliokaa tu wakisubiri miujiza hivyo nakusihii endelea kupambana ndugu msomaji wa mtandao huu.






Ukiwa bado unaendelea kupambana katika harakati zako basi jifunze kufurahia mateso,matatizo na vipingamizi mbalimbali uvipatavyo kwa sasa. Kwanini nasema jifunze kuyafurahia mateso, matatizo na vipingamizi vya sasa?. Sababu ninazo kupa hapa basi zinaweza kuwa muhimu kwako kuweza kukufanya uyafurahie mateso, matatizo na vipingamizi kadha wa kadha.
1.    Vinakufunza,ni kweli kuwa watu tulishawahi kupita, tunapitia na pengine tunaweza kuja kupitia katika mateso, matatizo na vipingamizi vya aina mbalimbali. Kama ulishawahi kupita katika mateso, vipingamizi au matatizo fulani basi utakubaliana nami kuwa vitu hivi huwa vinafunza. Jiulize swali hili huwa unajisikiaje pindi unapokuwa unapitia katika matatizo?, au pindi unapopitia vipingamizi fulani?, kama huwa unachukulia vitu hivi kwa hasira alafu unaanza kulalamika basi tambua kuwa una mtazamo hasi, na hivyo inabidi ubadili mtazamo huu na ujenge mtazamo wa kuyaangalia mateso, matatizo na vipingamizi vyako kwa hasira kisha acha kulaumu na baadae jiulize umejifunza nini kutokana na mambo hayo?. Huwa unajifunza nini pindi unapopingwa na wenzio je? unajawa na hasira na kuishia kulaumu au huwa unapatwa na hasira na unajifunza kuwa unapaswa kubadilika pengine unapingwa kutokana na kutokuwa bora katika jambo fulani, hivyo jifunze kutokana na kupingwa na ukajiboreshe zaidi na zaidi. Mateso unayoyaona leo yageuze kuwa kama somo. Matatizo pia yawe somo mfano unapokuwa na tatizo la pesa unajisikiaje?, unakubali hali au unajifunza na kulitatua tatizo hilo.

2.    Vinakuimalisha, matatizo, vipingamizi na matatizo, muda mwingine huwa kama viimalisho vyetu. Mfano matatizo yako yapo ili kukufanya uwe bora zaidi na zaidi. Mfano unapopata pingamizi kutoka sehemu mbalimbali kama vile unapopingwa kutokana na kigezo cha ukosefu wa elimu katika sehemu fulani ni muda wa kwenda kujiimalisha sasa ili uwe bora zaidi na usije ukapigwa tena na tena. Mateso muda mwingine usiyachukulie kama yapo kwa ajili ya kukutesa bali yapo kwa ajili ya kukuimalisha zaidi katika Nyanja mbalimbali za maisha.

3.    Vinakuamsha katika usingizi mzito, mateso, vipingamizi na matatizo yapo ili  kukuamsha katika usingizi mzito ambao umelala. Mfano halisi ni kuwa sisi binadamu huwa tunakumbwa na hali ya kujisahau pindi tunapojikuta kuwa tumefanikiwa kwa kiasi fulani na hapo ndipo wakati mwingine vipingamizi huja kwa ajili ya kutuamsha kutoka katika usingizi mzito ambao huwa tunakuwa tumelala pengine ni kutokana na baadhi ya mafanikio ambayo tunakuwa tumelala kwa muda. Binadamu huwa tunakuwa na hali ya kujisahau sana pindi tunapokuwa tumeona kuwa hali kwetu ni nzuri na hapo huwa tunajisahau sasa kwa wakati huu ndio huwa ni muhimu sana tena sana kuweza kuamshwa kutoka katika usingizi huu tulio lala. Matatizo mengi huja kwetu ili kutuamsha kutoka katika usingizi mzito tuliokuwa tumelala na hivyo kuweza kutuamsha. Mfano kama mfanyabiashara ukiwa umezoea kupeleka biadhaa zako mahali Fulani kwa wateja wako, kutokana na kufanya biashara kwa mazoea maana unafanya tu hutaki kuboresha bidhaa zako siku bidhaa yako ikipingwa na wateja wako, utakuwa umeamshwa sana. Pengine unateswa kwa kuwa umelala sasa inatakiwa uamke ili usiendelee kuteseka kama ukiendelea kulala maana yake utaendelea kuteseka.

Hivyo basi furahia mateso, matatizo na vipingamizi kwa maana ndani yake vimebeba mafunzo zaidi na zaidi.
Ni mimi rafiki yako,
Baraka Maganga
Wasiliana nami kwa.
 Simu: 0754612413 au 0652612410.
Barua pepe: Bmaganga22@gmail.com



Wednesday, January 20, 2016

Lazima Kitu Hiki Kiendelee Kuwepo Duniani, Na Ni Muhimu Kiwepo.

.Habari za wakati huu ndugu msomaji wa mtandao huu wa kona ya maarifa ni matumaini yangu kuwa hu mzima wa afya na unaendelea kupambana kwa hali na mali ili tu uweze kufanikisha yale ambayo umekuwa ukiyahangaikia mara kwa mara. Vizuri endelea kupambana naama hakuna kitu cha bure hapa duniani, maana hata miujiza huja kwa wale ambao huwa wanakuwa wakiitafuta miujiza hiyo. Sio waliokaa tu wakisubiri miujiza hivyo nakusihii endelea kupambana ndugu msomaji wa mtandao huu.



Ikiwa unapambana katika kuhakikisha unasonga mbele na wala sio kurudi nyuma basi ni vyema ukaelewa kuwa kitu hiki kimoja kisikutishe sana maana ni lazima kiendelee kuwepo hapa duniani, yaani usikihofie kitu hiki kwa maana ni cha muhimu sana tena sana. Kitu chenyewe ni tofauti zilizopo baina yetu sisi wanadamu. Ni wazi na ukweli usio pingika kuwa binadamu tunatofautiana sana tena sana na kwa kiasi kikubwa, kama ulikuwa hujui kuwa binadamu tunatofautiana basi anza kuelewa kwanzia sasa kuwa binadamu tunatofautiana na tofauti hizi zipo baina yetu na zinajionesha wazi wazi miongoni mwetu. Ngoja nikuwekeee mifano kadhaa ili uwezo kuelewa ni namna gani binadamu tunatofautiana tena kwa makundi tofauti tofauti.
Mfano katika maisha ya kawaida utofauti wetu unaweza kujionesha kutokana na  shughuli au kazi zetu, ndio maana katika maisha tuna madaktari, tuna manesi, tuna waalimu, tuna wafanyabiashara, tuna madereva, tuna wasio waajiriwa, tuna wawekezaji pamoja na wajasiliamali n.k. bado katika makundi hayo hayo  yanatofauti pia mfano katika kundi la madaktari tuna madaktari bingwa wa macho na wale bingwa kwa magonjwa ya watoto, katika waalimu tuna waalimu wakuu na waalimu wasio na cheo au kitengo chochote, katika kundi la madereva tuna madereva wa mabasi ya mikoani, daladala na madereva wa malori. Huu ni ufafanuzi kidogo ambao unaonesha  jinsi gani binadamu tunatofautiana sana tena sana.
Sasa utofauti huu usikutishe maaana haupo ili ukutishe bali upo ili kukupa changamoto na fursa wewe ili upate kuelewa ni wapi ambapo panakufaa haswa. Utofauti huu upo ili kukufanya wewe ufanye uchaguzi sahihi ni kundi gani linakufaa haswa na ni wapi unapataka. Hivyo basi badala ya kutishika na utofauti huu wewe chukulia utofauti huu kama fursa ya wapi panakufaa. Usitishike wala kuogopa unapoona mtu fulani kawa mfanyabiashara maarufu, fulani kawa daktari bingwa, kawa mchezaji bora, kawa mwamasheria n.k bali chukulia kama fursa ya wewe kuchagua ni wapi haswa panapokufaa na upange ni jinsi gani haswa utaweza kufika pale.
Pia ni muhimu ukatambua kuwa utofauti huu wa kimaisha unaweza kukusaidia wewe kufanya mambo fulani fulani, mfano utofauti unaweza kupelekea yafuatayo kwako:-
1)    Utofauti huu ndio hutukumbusha ya kuwa tunapaswa kuwajibika, kupitia tofauti zilizopo au zinazojitokeza kati yetu ndizo huwa kichocheo cha sisi kupambana ili kuhakikisha kuwa tunasonga mbele au kupata molari ya kujikwamua katika hali ambazo tunazo. Hebu chukulia mfano ni hali gani huwa unakuwa nayo pindi unapokutana na rafiki yako ambaye mnaendana kwa baadhi ya vitu kama vile umri, elimu, historia ya kimalezi na zaidi mlisoma na kucheza pamoja lakini  baada ya kuacha nae kwa muda anarudi akiwa na mafanikio makubwa sana kuliko wewe, tayari mmeshatofautiana japo mlikua na kusoma pamoja, sasa baada ya kuyaona mafanikio ya huyo rafiki yako, ni nini unachopata kwa mara ya kwanza?. Nadhani ni hisia za kuwajibika ili uweze kuwa kama rafiki yako.

2)    Hutufanya tuzichukie hali fulani, kupitia utofauti tulionao basi hutufanya tuzichukie baadhi ya hali zetu. Mfano pindi unapowaona wenzio wakifanikiwa ili hali wewe unabaki kuwa masikini wa kutupwa basi hapa ndipo huwa unapata hasira na kuanza kuuchukia umasikini lakini kiuhakika ni kuwa usingeweza kupata hasira ya kuichukia hali hii ya umasikini. Lakini sababu ya kukufanya uanze kuuchukia umasikini ni baada tu ya kuona tofauti iliyopo kati yako na wengine.


3)    Hutufanya tujifunze zaidi,tofauti zilizopo baina yetu na wengine wakati mwingine huwa kama somo kwetu maana tofauti hizi hutufanya tuanze kujihoji sana ni kwanini wengine wako hivi na sisi tuko hivi. Mfano leo hii unapata wazo gani unapowaona watu waliofanikiwa mbele yako, sina shaka kuwa itakuwa uwa unapata hamu ya kujifunza zaidi kutoka kwa watu hao.

Ni muhimu tofauti ziendelee kuwepo miongoni mwetu ili tuweze kuchagua ni wapi panatufaa, ili tuweze kubadilishana huduma maana  wote tukiwa wafanyabiashara nani atakuwa mnunuzi tena isitoshe wote tukiwa tunauza bidhaa sawa, ingekuwaje kama wote tungekuwa madereva na kila mtu, angelikuwa na gari lake, bila shaka kusingekuwepo abiri kwa sababu hizo na nyingine nyingi ni dhahiri kuwa tofauti ni lazima ziendelee kuwepo miongoni mwetu.


Ni mimi rafiki yako,
Baraka Maganga
Wasiliana nami kwa.
 Simu: 0754612413 au 0652612410.
Barua pepe: Bmaganga22@gmail.com


Tuesday, January 19, 2016

Chagua Timu Sahihi Ya Kushirikiana Nayo.


Habari ndugu msomaji wa mtandao huu wa kona ya maarifa, ni matumaini yangu kuwa unaendelea vizuri katika kuhakikisha kuwa unashughulikia ipasavyo yale unayo yahangaikia ili tu kujiletea mafanikio ambayo ndio kila mtu anayoyahangaikia. Nami nikusihi kwa moyo mmoja kuwa endelea kupambana mpaka uyatimize yale unayoyaamini kama mafanikio kwako. Pambana pambana bila kuchoka na mafanikio utayaona tu.





Katika maisha yetu sisi  wanadamu tumekuwa tukijikuta tunaunda timu ya watu ambao tunakuwa tunashirikiana nao mara kwa mara. Najua kila mtu atakuwa na timu ya kushirikiana nayo yaani una watu wako wa karibu ambao mara kwa mara umekuwa ukishirikiana nao kufanya nao mambo mbalimbali. Hili ni jambo ambalo kila binadamu huwa analifanya kila siku na kila wakati. Sina shida na hilo ila shida iliyopo ni aina ya watu ambao tunashirikiana nao.

 Je tunawafahamu ipasavyo hawa watu ambao tumekuwa tukishirikiana nao mara kwa mara katika mambo yetu yawe ya muhimu na yale yasiyo ya muhimu. Kama unataka kufanikiwa maishani hakikisha kuwa unashirikiana na watu ambao ni sahihi na munaendana nao, sisemi  kuwa lazima muwe mnaendana kielimu, kiumri, urefu na rangi za mwili lakini jambo la msingi ni kule kuendana kimtazamo na mawazo.

Mafanikio yanahusisha sana fikira yaaani fikira zako ndizo hukuletea mafanikio au kuto kukuletea mafanikio. Mwenendo wa fikira zako ndio ambao huamua wewe uwe wapi. Ndio maana kama unataka kuwa mwenye mafanikio basi hakikisha kuwa unazichunguza kwa kiwango kikubwa sana fikira zako. Na kama unataka kutoka kule uliko kwenda mbele zaidi yaani kwenye mafanikio  basi hakikisha kuwa una badili fikira zako kama ulikuwa na fikira mbovu kuhusu maisha, mafanikio, utajiri na umiliki mali basi anza kuzibadili na ukishazibadili nenda mbali zaidi kwa kutafuta timu sahihi ya kushirikiana nayo.

 Ni muhimu ukatambua kuwa ndugu msomaji mafanikio huendana sana na watu ambao unashirikiana nao. Wazungu wana msemo usemao kuwa “birds of feather floks tugeza” kwa tafsiri sisi tunaweza sema ndege wenye mabawa hutembea pamoja. Msemo huu unamaana sana na kama kweli unataka kufanikiwa basi hakikisha kuwa msemo huu unakukaa kichwani na haukutoki kamwe, yaani ufanye msemo huu kama kichochea chako cha kuelekea mafanikio.

Msemo huu unauhalisia mkubwa sana maishani hebu yachunguze makundi mbalimbali ya watu hata hapo mtaani kwako na kwingineko, waangalie watu ambao huwa wanashirikiana je wanaendana au huwa hawaendani?, waangalie walevi au watu wanaokunywa pombe huwa wanakuwa wanafahamiana na huwa hata wana namna yao ya kuwasiliana na wewe ambaye sio mlevi unaweza ukapata shida kuwaelewa hii ni kutokana na lugha yao, waangalie vijana wa kijiweni, waangalie walokole, waangalie watu wanaopenda michezo n.k.

Leo hii ni ngumiu kumkuta mlokole aliekomaa kijiweni akishirikiana na vijana hao wa kijiweni, au ni vigumu sana kumkuta mlevi amekaa na mtu ambayehatumii pombe wala kilevi cha aina yoyote ile. Sasa unajua kwanini watu hawa huwa wanachagua watu wanao endana nao, ni kwasababu wanajua kupitia watu hao watapata mawazo na fikira zenye kuendana nao. Yaani watakuwa wakibadilishana mawazo yao juu ya yale ambayo wanayafanya.

Sasa kwa kupitia mifano ya watu hawa ambao nimekuwekea hapo juu basi nawe unaetaka kufanikiwa hakikisha unajipatia timu sahihi ya kushirikiana nayo, timu hii itakuwa chachu ya mafanikio yako, maana utapata mawazo mbalimbali, utapata changamoto mbalimnbali ambazo zitakufanya uwe bora zaidi na zaidi na uweze kusonga mbele.
Kama kweli unataka kufanikiwa hakikisha unakuwa na fikira chanya na fikira chanya ndio utazipata kutokana na watu ambao unashirikiana nao. Watu wapo tu shida ni kuwa wewe ukoje kama unamtazamo chanya basi utafanya mambo chanya na utapata watu wenye fikira chanya hivyo ni wewe tu na sio kuwa huwezi kupata watu, watu wapo tu.

Ni mimi rafiki yako,
Baraka Maganga
Wasiliana nami kwa.
 Simu: 0754612413 au 0652612410.
Barua pepe: Bmaganga22@gmail.com



Friday, January 15, 2016

Huwezi Kufanikiwa Kama Utashindwa Kuepuka Jambo Hili.

Habari za wakati huu ndugu mpendwa msomaji wa makala za mtandao huu wa kona ya maarifa, ni matumaini yangu kuwa hu mzima wa afya na unaendelea vizuri katika kuhakikisha kuwa unayatekeleza yale ambayo umepanga kuyatekeleza. Vizuri endelea kupigana mpaka yale unayoyataka yamekamilika.





Wakati unaendelea kupambana, ili kuhakikisha kuwa unayatekeleza yale unayoyataka basi nakusihii epuka kitu hiki kimoja kama kweli unataka kufanikiwa katika maisha yako.jambo lenyewe ni kukosa ubunifu. Nimeamua kukuandikia hili ndugu msomaji ili uweze kuelewa madhara ya jambo hili. Na hili nimeamua kuliandika kutokana na ongezeko la tabia hii miongoni mwa watu wengi, na watanzania tukiwa ndio tunao ongoza kwa tabia hii ambayo kwangu naiona kama tabia isiyofaa kabisa kuigwa wala kufuatwa na jamii.


Tabia yenyewe ni ya kukosa ubunifu miongoni mwetu. Ukitazama shughuli nyingi sana za watanzania ni shughuli ambazo zimwekosa ubunifu, kabisa angalia sanaa zetu, biashara n.k, ni shughuli chache sana zenye kubeba ubunifu ndani yake. Watu siku hizi hawaangaiki kubuni kitu chochote badala yake wamekuwa ni watu wa kuhamisha mambo kama yalivyo kutoka walikoyatoa na kuyaleta kwetu,(coping and pasting), na kwa kuwa watu pia ubunifu umewapiga chenga basi nao huwa wanakubali kuamini mambo hayo hata kama wanajua hayaendani na sisi. Kutokana na ukosefu wa ubunifu ndio maana leo hii kumekuwa na tabia kubwa sana ya mambo ya kuigana igana tu na matokeo yake hakuna jipya linalo fanyika bali ni yale yale.


Ikiwa unataka kufanikiwa katika dunia ya leo basi hakikisha kuwa unakuwa mbunifu. Dunia ya leo imejaa ushindani wa hali ya juu, hii ikimaanisha kuwa kwa kila unalolifanya unaweza usiwe peke yako badala yake mtakuwa wengi. Sasa kama ikitokea mmekuwa wengi basi jambo la msingi la wewe kufanya ni kutafuta namna ya pekee ya kuweza kulifanya jambo lile ambalo litakutofautisha wewe na wengine. Kama ukishindwa kufanya hivyo basi tambua kuwa hautopata mafanikio makubwa katika yale unayoyafanya.


Chukulia mfano wa wachezaji Ronaldo na Messi, unajua ni kwa nini wanakuwa wachezaji bora wao tu kuliko wengine?, je wao ndio wachezaji pekee duniani kwamba hakuna wenzao. Ukiwaangalia wao kama wao hawana tofauti na wachezaji wengine maana wao wana miguu miwili kama wenzao wapo watu duniani ambao wanacheza namba kama zao lakini nini kinachofanya wao wafanikiwae kuliko wenzao, hakuna kingine bali ni ubunifu ambao wanao. Ubunifu wao ndio unawatofautisha wao na wenzao na kuwafanya waonekane bora kuliko wao. Wote wanafunga magoli, wanapiga chenga na bwebwe zingine zote unazozijua katika mpira lakini nini kinawatofautisha na wengine? Ni ubunifu walio nao ndio maana unakuta wanamagoli mengi kuliko wenzao. Wamebuni mbinu tofauti za kucheza mpira ambazo wenzao hawana muda wa kuzibuni ndio maana wanakuwa bora.


Tukirudi katika biashara za hapa kwetu Tanzania, ni biashara bora kwa kiasi chake lakini ni biashara ambazo zimejaa maswala ya kuigana tu hakuna jipya. Leo hii kumezuka maswala ya biashara za mtandao sasa kila mtu anataka afanye, achilia mbali maswala hayo, kutokana na maendeleo ya watu kutumia mitandao ya kijamiii watu wamekuwa na uwezo wa kutangaza biashara zao katika mitandao hiyo, lakini angalia namna ya utangazaji wao, kila mtu anapiga picha ya bidhaa na kuipost kisha ataandika tu kwa anae hitaji mawasiliano haya hapa, anatoa namba yake pale. Kama  sio hivyo utasikia, jipatie laba kali, tisheti n.k tunakuletea ulipo. Sasa biashara hizi sio kuwa nazipinga au kuwacheka wanaozifanya lakini nalo hoji ni kuwa ni lazima wote tuandike matangazo sawa hakuna anaeweza kubuni namna nyingine ambayo itamtofautisha na mwingine.


Angalia leo kuna makundi kibao katika mitandao mbalimbali makundi haya huanza kwa namna nzuri sana lakini kutokana na kuwa wote tumeathiriwa na namna moja ya kufikiri na hivyo tukakosa ubunifu, utakuta mtu kaanzisha kundi kaliita jina la kibiashara kabisa lakini ukiingia kwenye kundi hilo unakutana na stori za mapenzi, kwa kuwa ameona kuwa stori hizo ndizo zinazopendwa na kufuatiliwa na kuwapatia watu wengi sana umaarufu mkubwa. Angalia leo hii ni makundi mangapi yanazungumzia mapenzi, hakika yatakuwa mengi sana na yote yanaandika kitu kile kile hii inaonyesha kuwa hatuna ubunifu wa kutuwezesha watu  kuweza kufanya kitu cha tofauti.


Kimsingi ni vyema ukatambua kuwa katika dunia ya sasa, yenye kujaa ushindani wa hali ya juu huitaji kufanya kitu cha tofauti sana ila unatakiwa ufanye kitu kwa utofauti na hiyo ndio tabia ya watu walio fanikiwa. Sio kuwa wanafanya vitu tofauti bali wanafanya vitu kwa utofauti, na utofauti huo ndio ujulikanao kama ubunifu.  Na ndio huwafanya waonekane watu wa tofauti sana duniani.


Ni mimi rafiki yako,
Baraka Maganga.
Wasiliana nami kwa.
 Simu: 0754612413 au 0652612410.
Barua pepe: Bmaganga22@gmail.com.


Wednesday, January 13, 2016

Ifahamu Njia Ya Kutumia Ili Kupanga Shughuli Zako Katika Vipaumbele.

Habari za wakati huu ndugu msomaji wa mtandao huu wa kona ya maarifa ni matumaini yangu kuwa hu mzima wa afya na unaendelea vizuri katika kuyatekeleza majukumu yako ya kila siku. Nami nasema vizuri endelea kupambana mpaka uyatekeleze yale uliyokwisha kujiwekea.
Wakati unaendelea kupambana ili kuhakikisha kuwa unafanikiwa, wapo watu ambao wanahisi kuwa wanashughuli nyingi sana na hawajui ni ipi shughuli waanze nayo. Ikiwa unaona au kuhisi kuwa unashughuli nyingi sana na haujui ni ipi sahihi kuanza nayo basi hapa nakuletea njia sahihi ya kutumia ili uweze kujua ni shughuli ipi ya kuanza nayo, njia yenyewe inaitwa ABCDE. Hii ndiyo njia yetu ya kuweza kukusaidia kupanga shughuli zako. Ntaifafanua njia hii kama ifuatavyo:-,





Shughuli A- shughuli ya kuwa katika kundi hili inapaswa kuwa shughuli ya muhimu sana, hapa kinapaswa kuwa kitu cha muhimu sana ambacho ni lazima ukifanye au kifanyike. Shughuli ambayo inapaswa kuwa na jina la A ni lazima utambue kuwa ni shughulia ambayo isipofanyika basi ina madhara makubwa sana. Mfano wewe ni mfanyabiashara na unaitegemea biashara husika katika kuendesha maisha yako basi hiyo shughuli ndio inapaswa kuwa hapo, maana kwanza ni muhimu, lazima ufanye ili uishi na mwisho ukiacha kufanya basi madhara yapo.
Shughuli B- hii ni shughuli ambayo inatakiwa uifanye, shughuli ambayo inatakiwa iwepo hapa ni ile ambayo pia isipofanyika ina madhara lakini sio muhimu sana kama ilivyo katika shughuli A. mfano kama umeamua kuanzisha program ya kufanya mazoezi kila siku asubuhi kabla ya kuelekea katika shughuli zako ni muhimu ukafanya hivyo ingawa kuto kufanya kuna madhara ya kuwa afya yako itadhoofika lakini sio muhimu sana maana wapo ambao hawafanyi zoezi na afya zao ni nzuri tu.
Shughuli C- katika kundi hili linapaswa kuwa na shughuli ambayo ni vizuri ifanyike lakini haina madhara yoyote. Mfano kuamua kwenda kuwatembelea ndugu mahali fulani kama vile dada, kaka, shangazi, bibi au babu, ukitazama vizuri swala la kwenda kuwatembelea ndugu mara kwa mara ni vizuri lakini hakuna madhara yoyote makubwa. Au shughuli nyingine ni kama vile kwa mfanyakazi ambae anataka kwenda kunywa chai au kula chakula pahali fulani na wafanyakazi wenzake, ni vizuri kufanya hivyo lakini kuto fanya hivyo hakuna madhara makubwa. Au kwa yule aliyeoa ni vizuri kupiga simu kuulizia leo mkeo kapika nini lakini hakuna madhara yoyote usipo fanya hivyo. Hivyo basi shughuli zote zenye kufanana na hizo zinapaswa kuwa hapa katika kundi hili.
Shughuli D- hapa pana husisha shughuli yoyote ile ambayo unaweza kumwachia mtu aifanye.  Ni muhimu utambue kuwa yakupasa uyaache yale ambayo yanaweza kufanywa na mtu fulani ili ayafanye yeye badala yako. Hii itasaidia nini haswa?, hii itakusaidia wewe kuokoa muda ambao ungeupoteza kufanya jambo ambalo linaweza kufanywa na mtu mwingine. Mfano mama mwenye binti zake wakubwa nyumbani anapaswa kuwaachia shughuli kama vile za usafi wa nyumba na yeye akawahi katika shughuli zake kama vile biashara zake.
Shughuli E- hapa ni shughuli ambazo unaweza kuamua kutokuzifanya kabisa. Hizi ni shughuli ambazo unaweza kuamua kuzifanya au kutokuzifanya na hazina madhara yoyote. Mfano shughuli ya kujibu kila jumbe au  kila unachokiona katika makundi ya whatsapp.
Mara nyingi sana watu huwa tunakabiliwa na changamoto pale ambapo tunapaswa kufanya jambo fulani, hii ni kutokana na kuwa na shughuli nyingi sana ambazo tunaamini kuwa zote ni za muhimu, utakuta mtu anataka kwenda kwenye biashara, mara kufanya zoezi, mara kwenda kumtembelea shangazi n.k. huyu ni mtu mmoja ambae anataka kuyafanya yote haya na hajui aanze na lipi. Kama unakubwa na shida hizo basi dawa ndiyo hiyo nimekupatia.  

Ni mimi rafiki yako,
Baraka Maganga
Wasiliana nami kwa.
 Simu: 0754612413 au 0652612410.
Barua pepe: Bmaganga22@gmail.com





Monday, January 11, 2016

Zifahamu Kauli Kumi (10) Unazozitumia Na Zinakufanya Usifanikiwe.

Habari za wakati huu ndugu msomaji wa mtandao huu wa kona ya maarifa ni matumaini yangu kuwa umeshaianza siku yako vema na unaendelea kupambana ili kuhakikisha kuwa siku yako ya leo mpaka inaisha unakuwa umejisogeza vya kutosha katika kuyatekeleza malengo yako. Nami nakusihi usichoke maana mafanikio yanahitaji uvumilivu wa hali ya juu hata kama mambo hayajaenda sawa wewe usijali endelea kupambana tu na mafanikio utayaona.
Leo kuna jambo nataka kukushirikisha ndugu msomaji wa mtandao huu, tumekuwa tukiamini kuwa maneno huumba, au wengine husema kauli huumba tukiwa na maana kuwa kadri tujisemeshavyo wenyewe  juu ya maisha yetu ndivyo maisha yetu huwa. Sasa kutokana na hili ndio maana nimekuletea kauli kumi ambazo watu wamekuwa wakizitumia na zimekuwa zikiwafelisha na kuwaweka mbali na mafanikio kauli hizo ni kama ifuatavyo:-,





Sikuzaliwa au kukulia katika familia bora, kuna watu ambao huamini na kuhararisha kutokufanikiwa kwao na kutozaliwa au kuto kukulia katika familia bora. Hizi ni kauli ambazo hazina maana yoyote katika dunia ya leo maaana mafanikio ni wewe na sio familia uliyokulia, na kama wewe unaona hilo ni sahihi ni wangapi kwani ambao wamefanikiwa japo kuwa hawajatoka familia bora?, acha mara moja kauli hizi badala yake anza kufikiria utafanyaje ili ufanikiwe ijapokuwa hujatoka familia bora hilo ndilo jambo la msingi.

2.    Sikuzaliwa upande sahihi, hawa ni waleambao huona kuwa kutokana na wao kuzaliwa bara fulani, au nchi fulani ni mkosi kwao, maana huamini kuwa bara au nchi husika waliyomo haiwaruhusu kufanikiwa. Ni kauli za kijinga na ambazo hutumiwa na watu ambao hawajafanikiwa ndio husema bora kuzaliwa mbwa ulaya kuliko mtu afrika, hizi ni kauli za ajabu sana, kwani ni waafrika wangapi wapo afrika na wamefanikiwa, ni watanzania wangapi wanamafanikio hapa hapa Tanzania, ni wakenya, waganda n.k wangapi wenye mafanikio ndani ya nchi zao?. Acha kauli zisizo za msingi.

3.    Sina elimu ya kutosha, hii ilikuwa na umuhimu enzi zile za zama za kati za mawe lakini sio katika dunia ya sasa ya taarifa. Nani aliyekuambia mafanikio ni kutokana na elimu yako tu?, wangapi wanamafanikio makubwa na hawana hata digrii, masters, wala hizo phd ambazo wewe unaamini lazima uwe nazo ndizo zitakufanya ufanikiwe. Chukulia mfano wa mafanikio ya msanii Diamond na msakata kabumbu  Mbwana Samatta, je wanaelimu kiasi gani?. Jibu baki nalo.


4.    Hayo ni mambo yako sio yangu, kauli kama hizi ndizo huwafanya watu wakose fursa. Utamkuta mtu analetewa wazo la kibiashara ambalo tayari ni fursa kwake lakini utamsikia aa bwana ee hayo ni mambo yako sio yangu. Sasa endelea hivyo hivyo na utaendelea kukosa fursa siku hadi siku.

5.    Sina muda wa kutosha, wewe kila siku muda haukutoshi, wewe ni nani na unafanya nini mpaka muda usikutoshe kila siku?, je unataka upatiwe masaa 70 ndani ya siku moja? Kwanini wewe tu ndio muda haukutoshi? Mbona wengine masaa 24 yanamtosha. Jifunze kutumia muda ulopewa vizuri.


6.    Sina pesa za kutosha, unafikiri pesa inatosha kwa kukaa nayo tu? Au kwa kuiweka tu ndani na kuishangaa au benki?,  acha kufikiri pesa itakuja kukutosha bila kuizungusha, jifunze kuizungusha hiyo pesa ndipo itakutosha.

7.    Sifahamiani na watu sahihi, ni kweli hufamiani na watu sahihi kutokana na matendo yako na ndio maana huwezi kuwapata watu sahihi wa kukusukuma uende mbele. Kama unataka kupata kushirikiana na watu sahihi anza kufanya mambo yanayoendana na hao watu ambao kwako ni sahihi.


8.    Sina mtandao wa watu, hauna mtandao wa watu wa kushirikiana nawe kutokana na wewe mwenyewe ulivyo. Mtandao wa watu wa kushirikiana nao unakuja kutokana na kile ambacho unakifanya na kutokana na ushirikiano wako na watu wengine. Unashirikiana na nani haswa na huyo unayeshirikiana nae je? anamtandao au?.

9.    Mke wangu hanisaidi, ni kweli mke wako hakusaidi lakini wewe kama wewe umechukua juhudi gani kuhakikisha kuwa wewe kama wewe unapigana vilivyo katika kuhakikisha kuwa unasimama wewe kama wewe?,  je mafanikio yako yanamtegemea mke wako tu?, kama asingalikuwepo ungalifanyaje?, acha kutegemea tegemea bila msingi badala yake  jifunze kusimama mwenyewe muda mwingine.


10. Nina watoto wengi wa kulea, kama ulijua kuwa watoto wengi wanakufanya usifanikiwe kwanini umekuwa nao?. Na je ni kweli kwamba bila kuwa na watoto wengi ungefanikiwa au ni visingizio?, je tukiwachukua hao watoto na tukakuacha mtupu utafanikiwa?

Kimsingi kauli hizi kumi kwa maneno mengine tunaweza kuziita kama visingizio ambavyo mtu huwa navyo, na hii ni hatari sana maana visingizio havikufanyi kuwa mwenye mafanikio bali vinazidi kukurudisha nyuma. Hivyo basi uamuzi ni wako kuendelea na visingizio na sababu sababu za kuto kufanikiwa kwako ambzao zitazidi kukufanya usiwe na mafanikio au uziache na kuwa mwenye mafanikio.

Ni mimi rafiki yako,
Baraka Maganga
Wasiliana nami kwa.
 Simu: 0754612413 au 0652612410.
Barua pepe: Bmaganga22@gmail.com



Saturday, January 9, 2016

Sababu Sita (6) Za Kwanini Watu Hawajiwekei Malengo.



Habari za leo ndugu msomaji wa mtandao huu wa kona ya maarifa ni matumaini yangu kuwa hu mzima wa afya na unaendeleo kupambana vilivyo katika kuhakikisha kuwa unajiletea mafanikio makubwa maishani mwako. Nami nakusihi ndugu msomaji wa mtandao huu kuwa endelea kupambana, usichoke hata siku mpaka uhakikishe kuwa unajipatia mafanikio makubwa, ambayo umekwisha jiwekea.
Ukiwa unaendelea kujishighulisha na shughuli zako za kila siku basi leo nakuletea kitu kingine ambacho unapaswa ukifahamu vyema. Kama  kichwa cha makala kinavyosema kuwa sababu za kwanini watu huwa hawajiwekei malengp maishani. Tumekuwa tukisisitizana na kuambiana mara nyingi sana juu ya umuhimu wa kuweka malengo, lakini ukweli ni kwamba ni watu wachache sana kati ya wengi ambao wamekuwa na utamaduni wa kujiwekea malengo. Na walio wengi wamekuwa hawajiwekei malengo, sasa kwanini watu hawa huwa hawajiwekei malengo maishani, zifuatazo ni sababu za kwanini watu hawajiwekei malengo:-,




Hawako makini, sababu moja wapo ya kwanini watu hawajiwekei malengo ni kutokana na sababu kuwa hawapo makini maishani. Mtu makini na anayetaka kufanikiwa kwa hali na mali lazima ajiwekee malengo. Lakini kutokana na ukosefu wa umakini miongoni mwetu tumekuwa tukiishi hivyo hivyo bila malengo
.
2.    Hawajayakubali majukumu yao, kama mpaka sasa hujathubutu hata kujiwekea malengo basi tambua kuwa bado hujataka kuyavaa majukumu yako. Yaani watu ambao bado hawajajiwekea malengo ni wale ambao bado wanahisi kuwa yupo mtu fulani maishani ambae ndiye yupo kwa ajili ya kusubiri kufanyiwa kitu fulani jambo ambalo kiukweli ni kujidanganya. Hivyo basi ukosefu wa ile hali ya kuvaa majukumu ndio kimekuwa kikwazo cha watu kujiwekea malengo.

3.    Hawatambui umuhimu wa kujiwekea malengo, watu wamekuwa hawajiwekei malengo kwa sababu hawajui umuhimu wa kujiwekea malengo. Inaonekana kuwa miongoni mwa watu wengi sana hawana uelewa juu ya maswala haya ya kujiwekea malengo ndio maana wamekuwa hawajiwekei malengo maishani mwao. Watu hawaoni umuhimu wowote wa kujiwekea malengo ndio maana wamekuwa hawajiwekei, lakini naomba niseme kuwa hii ni kosa kubwa sana ambalo watu hulifanya, nasema hivyo kwa sababu ni vyema kila mtu akatambua umuhimu wa kuweza malengo na akijua umuhimu atakuwa amejikomboa kwa kiwango kikubwa.

4.    Hawajui ni vipi watapanga/ kuyaandika malengo yao, sababu nyingine ambayo inawafanya watu wasijiwekee malengo ni kutokana na ukweli kwamba hawajui ni vipi wajiwekee malengo. Hii nadhani ndio sababu namba moja ya kwanini watu hawajiwekei malengo maishani, yaani hawaweki malengo kwa sababu hawajui watafanyaje. Kama hujui mpaka leo basi jua kuwa upo katika hatari.
5.    Wanaogopa kukosolewa/ kukataliwa, uoga umekuwa ukichangia sana miongoni mwa watu, na imekuwa sababu inayofanya watu washindwe kujiwekea malengo, watu wamekuwa wakiogopa kujiwekea malengo kwa kuwa wanaogopa kuwa endapo wakimwonesha mtu malengo yake atakosolewa sana hivyo kutokana na woga huu basi unamfanya arudi nyuma na kukaa bila kuweka malengo.

6.    Wanaogopa kushindwa, watu wengi hawaweki malengo kwa kuwa wanaogopa kushindwa yaani anaogopa kuwa itakuwaje nikiweka malengo alafu nisiyatimize hivyo kutokana na kuogopa huko katika kushindwa basi anakaa tu na kutokujiwekea malengo.


Ikiwa unataka kufanikiwa zaidi na zaidi ni muhimu ukatambua kuwa malengo ni kitu muhimu sana tena sana, malengo ni dira katika maisha yako. Ikiwa hujajiwekea malengo basi nishakuwekea sababu sita za kwanini hujafanya hivyo. Kupitia sababu hizo unaweza ukaelewa ufanye nini ili kujiwekea malengo. Mfano umeshajua sababu moja wapo inayokufanya usijiwekee malengo ni kuwa hujayakubali majukumu, sasa nini cha kufanya ni kuyavaa majukumu kisha baada ya hapo utapata uwezo na uelewa wa ni vipi ujiwekee  malengo.


Ni mimi rafiki yako,
Baraka Maganga
Wasiliana nami kwa.
 Simu: 0754612413 au 0652612410.
Barua pepe: Bmaganga22@gmail.com