Habari ndugu msomaji wa mtandao huu wa kona ya maarifa,
ni matumaini yangu kuwa unaendelea vizuri katika kuhakikisha kuwa
unashughulikia ipasavyo yale unayo yahangaikia ili tu kujiletea mafanikio
ambayo ndio kila mtu anayoyahangaikia. Nami nikusihi kwa moyo mmoja kuwa
endelea kupambana mpaka uyatimize yale unayoyaamini kama mafanikio kwako.
Pambana pambana bila kuchoka na mafanikio utayaona tu.
Katika maisha yetu sisi
wanadamu tumekuwa tukijikuta tunaunda timu ya watu ambao tunakuwa
tunashirikiana nao mara kwa mara. Najua kila mtu atakuwa na timu ya
kushirikiana nayo yaani una watu wako wa karibu ambao mara kwa mara umekuwa
ukishirikiana nao kufanya nao mambo mbalimbali. Hili ni jambo ambalo kila
binadamu huwa analifanya kila siku na kila wakati. Sina shida na hilo ila shida
iliyopo ni aina ya watu ambao tunashirikiana nao.
Je tunawafahamu
ipasavyo hawa watu ambao tumekuwa tukishirikiana nao mara kwa mara katika mambo
yetu yawe ya muhimu na yale yasiyo ya muhimu. Kama unataka kufanikiwa maishani
hakikisha kuwa unashirikiana na watu ambao ni sahihi na munaendana nao,
sisemi kuwa lazima muwe mnaendana
kielimu, kiumri, urefu na rangi za mwili lakini jambo la msingi ni kule kuendana
kimtazamo na mawazo.
Mafanikio yanahusisha sana fikira yaaani fikira zako
ndizo hukuletea mafanikio au kuto kukuletea mafanikio. Mwenendo wa fikira zako
ndio ambao huamua wewe uwe wapi. Ndio maana kama unataka kuwa mwenye mafanikio
basi hakikisha kuwa unazichunguza kwa kiwango kikubwa sana fikira zako. Na kama
unataka kutoka kule uliko kwenda mbele zaidi yaani kwenye mafanikio basi hakikisha kuwa una badili fikira zako
kama ulikuwa na fikira mbovu kuhusu maisha, mafanikio, utajiri na umiliki mali
basi anza kuzibadili na ukishazibadili nenda mbali zaidi kwa kutafuta timu
sahihi ya kushirikiana nayo.
Ni muhimu ukatambua
kuwa ndugu msomaji mafanikio huendana sana na watu ambao unashirikiana nao.
Wazungu wana msemo usemao kuwa “birds of feather floks tugeza” kwa tafsiri sisi
tunaweza sema ndege wenye mabawa hutembea pamoja. Msemo huu unamaana sana na
kama kweli unataka kufanikiwa basi hakikisha kuwa msemo huu unakukaa kichwani
na haukutoki kamwe, yaani ufanye msemo huu kama kichochea chako cha kuelekea
mafanikio.
Msemo huu unauhalisia mkubwa sana maishani hebu
yachunguze makundi mbalimbali ya watu hata hapo mtaani kwako na kwingineko,
waangalie watu ambao huwa wanashirikiana je wanaendana au huwa hawaendani?,
waangalie walevi au watu wanaokunywa pombe huwa wanakuwa wanafahamiana na huwa
hata wana namna yao ya kuwasiliana na wewe ambaye sio mlevi unaweza ukapata
shida kuwaelewa hii ni kutokana na lugha yao, waangalie vijana wa kijiweni,
waangalie walokole, waangalie watu wanaopenda michezo n.k.
Leo hii ni ngumiu kumkuta mlokole aliekomaa kijiweni akishirikiana
na vijana hao wa kijiweni, au ni vigumu sana kumkuta mlevi amekaa na mtu
ambayehatumii pombe wala kilevi cha aina yoyote ile. Sasa unajua kwanini watu
hawa huwa wanachagua watu wanao endana nao, ni kwasababu wanajua kupitia watu hao
watapata mawazo na fikira zenye kuendana nao. Yaani watakuwa wakibadilishana
mawazo yao juu ya yale ambayo wanayafanya.
Sasa kwa kupitia mifano ya watu hawa ambao nimekuwekea
hapo juu basi nawe unaetaka kufanikiwa hakikisha unajipatia timu sahihi ya
kushirikiana nayo, timu hii itakuwa chachu ya mafanikio yako, maana utapata
mawazo mbalimbali, utapata changamoto mbalimnbali ambazo zitakufanya uwe bora
zaidi na zaidi na uweze kusonga mbele.
Kama kweli unataka kufanikiwa hakikisha unakuwa na fikira
chanya na fikira chanya ndio utazipata kutokana na watu ambao unashirikiana
nao. Watu wapo tu shida ni kuwa wewe ukoje kama unamtazamo chanya basi utafanya
mambo chanya na utapata watu wenye fikira chanya hivyo ni wewe tu na sio kuwa
huwezi kupata watu, watu wapo tu.
Ni mimi rafiki yako,
Baraka Maganga
Wasiliana nami kwa.
Simu: 0754612413 au 0652612410.
Barua
pepe: Bmaganga22@gmail.com
No comments:
Post a Comment