Habari za wakati huu ndugu mpendwa msomaji wa makala za
mtandao huu wa kona ya maarifa, ni matumaini yangu kuwa hu mzima wa afya na
unaendelea vizuri katika kuhakikisha kuwa unayatekeleza yale ambayo umepanga
kuyatekeleza. Vizuri endelea kupigana mpaka yale unayoyataka yamekamilika.
Wakati unaendelea kupambana, ili kuhakikisha kuwa
unayatekeleza yale unayoyataka basi nakusihii epuka kitu hiki kimoja kama kweli
unataka kufanikiwa katika maisha yako.jambo lenyewe ni kukosa ubunifu. Nimeamua kukuandikia hili ndugu msomaji ili uweze
kuelewa madhara ya jambo hili. Na hili nimeamua kuliandika kutokana na ongezeko
la tabia hii miongoni mwa watu wengi, na watanzania tukiwa ndio tunao ongoza
kwa tabia hii ambayo kwangu naiona kama tabia isiyofaa kabisa kuigwa wala
kufuatwa na jamii.
Tabia yenyewe ni ya kukosa ubunifu miongoni mwetu. Ukitazama
shughuli nyingi sana za watanzania ni shughuli ambazo zimwekosa ubunifu, kabisa
angalia sanaa zetu, biashara n.k, ni shughuli chache sana zenye kubeba ubunifu
ndani yake. Watu siku hizi hawaangaiki kubuni kitu chochote badala yake
wamekuwa ni watu wa kuhamisha mambo kama yalivyo kutoka walikoyatoa na kuyaleta
kwetu,(coping and pasting), na kwa kuwa watu pia ubunifu umewapiga chenga basi
nao huwa wanakubali kuamini mambo hayo hata kama wanajua hayaendani na sisi. Kutokana
na ukosefu wa ubunifu ndio maana leo hii kumekuwa na tabia kubwa sana ya mambo
ya kuigana igana tu na matokeo yake hakuna jipya linalo fanyika bali ni yale
yale.
Ikiwa unataka kufanikiwa katika dunia ya leo basi
hakikisha kuwa unakuwa mbunifu. Dunia ya leo imejaa ushindani wa hali ya juu,
hii ikimaanisha kuwa kwa kila unalolifanya unaweza usiwe peke yako badala yake
mtakuwa wengi. Sasa kama ikitokea mmekuwa wengi basi jambo la msingi la wewe
kufanya ni kutafuta namna ya pekee ya kuweza kulifanya jambo lile ambalo
litakutofautisha wewe na wengine. Kama ukishindwa kufanya hivyo basi tambua
kuwa hautopata mafanikio makubwa katika yale unayoyafanya.
Chukulia mfano wa wachezaji Ronaldo na Messi, unajua ni
kwa nini wanakuwa wachezaji bora wao tu kuliko wengine?, je wao ndio wachezaji
pekee duniani kwamba hakuna wenzao. Ukiwaangalia wao kama wao hawana tofauti na
wachezaji wengine maana wao wana miguu miwili kama wenzao wapo watu duniani
ambao wanacheza namba kama zao lakini nini kinachofanya wao wafanikiwae kuliko
wenzao, hakuna kingine bali ni ubunifu ambao wanao. Ubunifu wao ndio
unawatofautisha wao na wenzao na kuwafanya waonekane bora kuliko wao. Wote wanafunga
magoli, wanapiga chenga na bwebwe zingine zote unazozijua katika mpira lakini
nini kinawatofautisha na wengine? Ni ubunifu walio nao ndio maana unakuta
wanamagoli mengi kuliko wenzao. Wamebuni mbinu tofauti za kucheza mpira ambazo
wenzao hawana muda wa kuzibuni ndio maana wanakuwa bora.
Tukirudi katika biashara za hapa kwetu Tanzania, ni
biashara bora kwa kiasi chake lakini ni biashara ambazo zimejaa maswala ya
kuigana tu hakuna jipya. Leo hii kumezuka maswala ya biashara za mtandao sasa
kila mtu anataka afanye, achilia mbali maswala hayo, kutokana na maendeleo ya
watu kutumia mitandao ya kijamiii watu wamekuwa na uwezo wa kutangaza biashara
zao katika mitandao hiyo, lakini angalia namna ya utangazaji wao, kila mtu
anapiga picha ya bidhaa na kuipost kisha ataandika tu kwa anae hitaji
mawasiliano haya hapa, anatoa namba yake pale. Kama sio hivyo utasikia, jipatie laba kali, tisheti
n.k tunakuletea ulipo. Sasa biashara hizi sio kuwa nazipinga au kuwacheka wanaozifanya
lakini nalo hoji ni kuwa ni lazima wote tuandike matangazo sawa hakuna anaeweza
kubuni namna nyingine ambayo itamtofautisha na mwingine.
Angalia leo kuna makundi kibao katika mitandao mbalimbali
makundi haya huanza kwa namna nzuri sana lakini kutokana na kuwa wote
tumeathiriwa na namna moja ya kufikiri na hivyo tukakosa ubunifu, utakuta mtu
kaanzisha kundi kaliita jina la kibiashara kabisa lakini ukiingia kwenye kundi
hilo unakutana na stori za mapenzi, kwa kuwa ameona kuwa stori hizo ndizo
zinazopendwa na kufuatiliwa na kuwapatia watu wengi sana umaarufu mkubwa. Angalia
leo hii ni makundi mangapi yanazungumzia mapenzi, hakika yatakuwa mengi sana na
yote yanaandika kitu kile kile hii inaonyesha kuwa hatuna ubunifu wa
kutuwezesha watu kuweza kufanya kitu cha
tofauti.
Kimsingi ni vyema ukatambua kuwa katika dunia ya sasa,
yenye kujaa ushindani wa hali ya juu huitaji kufanya kitu cha tofauti sana ila
unatakiwa ufanye kitu kwa utofauti na hiyo ndio tabia ya watu walio fanikiwa. Sio
kuwa wanafanya vitu tofauti bali wanafanya vitu kwa utofauti, na utofauti huo
ndio ujulikanao kama ubunifu. Na ndio
huwafanya waonekane watu wa tofauti sana duniani.
Ni mimi rafiki yako,
Baraka Maganga.
Wasiliana nami kwa.
Simu: 0754612413 au 0652612410.
Barua
pepe: Bmaganga22@gmail.com.
No comments:
Post a Comment