Habari za wakati huu ndugu msomaji wa mtandao huu wa kona
ya maarifa ni matumaini yangu kuwa hu mzima wa afya na unaendelea vizuri katika
kuyatekeleza majukumu yako ya kila siku. Nami nasema vizuri endelea kupambana
mpaka uyatekeleze yale uliyokwisha kujiwekea.
Wakati unaendelea kupambana ili kuhakikisha kuwa
unafanikiwa, wapo watu ambao wanahisi kuwa wanashughuli nyingi sana na hawajui
ni ipi shughuli waanze nayo. Ikiwa unaona au kuhisi kuwa unashughuli nyingi
sana na haujui ni ipi sahihi kuanza nayo basi hapa nakuletea njia sahihi ya
kutumia ili uweze kujua ni shughuli ipi ya kuanza nayo, njia yenyewe inaitwa ABCDE. Hii ndiyo njia yetu ya kuweza
kukusaidia kupanga shughuli zako. Ntaifafanua njia hii kama ifuatavyo:-,
Shughuli
A-
shughuli ya kuwa katika kundi hili inapaswa kuwa shughuli ya muhimu sana, hapa
kinapaswa kuwa kitu cha muhimu sana ambacho ni lazima ukifanye au kifanyike. Shughuli
ambayo inapaswa kuwa na jina la A ni lazima utambue kuwa ni shughulia ambayo
isipofanyika basi ina madhara makubwa sana. Mfano wewe ni mfanyabiashara na
unaitegemea biashara husika katika kuendesha maisha yako basi hiyo shughuli
ndio inapaswa kuwa hapo, maana kwanza ni muhimu, lazima ufanye ili uishi na mwisho
ukiacha kufanya basi madhara yapo.
Shughuli
B-
hii ni shughuli ambayo inatakiwa uifanye, shughuli ambayo inatakiwa iwepo hapa
ni ile ambayo pia isipofanyika ina madhara lakini sio muhimu sana kama ilivyo
katika shughuli A. mfano kama umeamua kuanzisha program ya kufanya mazoezi kila
siku asubuhi kabla ya kuelekea katika shughuli zako ni muhimu ukafanya hivyo
ingawa kuto kufanya kuna madhara ya kuwa afya yako itadhoofika lakini sio
muhimu sana maana wapo ambao hawafanyi zoezi na afya zao ni nzuri tu.
Shughuli
C-
katika kundi hili linapaswa kuwa na shughuli ambayo ni vizuri ifanyike lakini
haina madhara yoyote. Mfano kuamua kwenda kuwatembelea ndugu mahali fulani kama
vile dada, kaka, shangazi, bibi au babu, ukitazama vizuri swala la kwenda kuwatembelea
ndugu mara kwa mara ni vizuri lakini hakuna madhara yoyote makubwa. Au shughuli
nyingine ni kama vile kwa mfanyakazi ambae anataka kwenda kunywa chai au kula
chakula pahali fulani na wafanyakazi wenzake, ni vizuri kufanya hivyo lakini
kuto fanya hivyo hakuna madhara makubwa. Au kwa yule aliyeoa ni vizuri kupiga
simu kuulizia leo mkeo kapika nini lakini hakuna madhara yoyote usipo fanya
hivyo. Hivyo basi shughuli zote zenye kufanana na hizo zinapaswa kuwa hapa
katika kundi hili.
Shughuli
D-
hapa pana husisha shughuli yoyote ile ambayo unaweza kumwachia mtu
aifanye. Ni muhimu utambue kuwa yakupasa
uyaache yale ambayo yanaweza kufanywa na mtu fulani ili ayafanye yeye badala
yako. Hii itasaidia nini haswa?, hii itakusaidia wewe kuokoa muda ambao
ungeupoteza kufanya jambo ambalo linaweza kufanywa na mtu mwingine. Mfano mama
mwenye binti zake wakubwa nyumbani anapaswa kuwaachia shughuli kama vile za
usafi wa nyumba na yeye akawahi katika shughuli zake kama vile biashara zake.
Shughuli
E-
hapa ni shughuli ambazo unaweza kuamua kutokuzifanya kabisa. Hizi ni shughuli
ambazo unaweza kuamua kuzifanya au kutokuzifanya na hazina madhara yoyote. Mfano
shughuli ya kujibu kila jumbe au kila
unachokiona katika makundi ya whatsapp.
Mara nyingi sana watu huwa tunakabiliwa na changamoto
pale ambapo tunapaswa kufanya jambo fulani, hii ni kutokana na kuwa na shughuli
nyingi sana ambazo tunaamini kuwa zote ni za muhimu, utakuta mtu anataka kwenda
kwenye biashara, mara kufanya zoezi, mara kwenda kumtembelea shangazi n.k. huyu
ni mtu mmoja ambae anataka kuyafanya yote haya na hajui aanze na lipi. Kama unakubwa
na shida hizo basi dawa ndiyo hiyo nimekupatia.
Ni mimi rafiki yako,
Baraka Maganga
Wasiliana nami kwa.
Simu: 0754612413 au 0652612410.
Barua
pepe: Bmaganga22@gmail.com
No comments:
Post a Comment