Monday, January 11, 2016

Zifahamu Kauli Kumi (10) Unazozitumia Na Zinakufanya Usifanikiwe.

Habari za wakati huu ndugu msomaji wa mtandao huu wa kona ya maarifa ni matumaini yangu kuwa umeshaianza siku yako vema na unaendelea kupambana ili kuhakikisha kuwa siku yako ya leo mpaka inaisha unakuwa umejisogeza vya kutosha katika kuyatekeleza malengo yako. Nami nakusihi usichoke maana mafanikio yanahitaji uvumilivu wa hali ya juu hata kama mambo hayajaenda sawa wewe usijali endelea kupambana tu na mafanikio utayaona.
Leo kuna jambo nataka kukushirikisha ndugu msomaji wa mtandao huu, tumekuwa tukiamini kuwa maneno huumba, au wengine husema kauli huumba tukiwa na maana kuwa kadri tujisemeshavyo wenyewe  juu ya maisha yetu ndivyo maisha yetu huwa. Sasa kutokana na hili ndio maana nimekuletea kauli kumi ambazo watu wamekuwa wakizitumia na zimekuwa zikiwafelisha na kuwaweka mbali na mafanikio kauli hizo ni kama ifuatavyo:-,





Sikuzaliwa au kukulia katika familia bora, kuna watu ambao huamini na kuhararisha kutokufanikiwa kwao na kutozaliwa au kuto kukulia katika familia bora. Hizi ni kauli ambazo hazina maana yoyote katika dunia ya leo maaana mafanikio ni wewe na sio familia uliyokulia, na kama wewe unaona hilo ni sahihi ni wangapi kwani ambao wamefanikiwa japo kuwa hawajatoka familia bora?, acha mara moja kauli hizi badala yake anza kufikiria utafanyaje ili ufanikiwe ijapokuwa hujatoka familia bora hilo ndilo jambo la msingi.

2.    Sikuzaliwa upande sahihi, hawa ni waleambao huona kuwa kutokana na wao kuzaliwa bara fulani, au nchi fulani ni mkosi kwao, maana huamini kuwa bara au nchi husika waliyomo haiwaruhusu kufanikiwa. Ni kauli za kijinga na ambazo hutumiwa na watu ambao hawajafanikiwa ndio husema bora kuzaliwa mbwa ulaya kuliko mtu afrika, hizi ni kauli za ajabu sana, kwani ni waafrika wangapi wapo afrika na wamefanikiwa, ni watanzania wangapi wanamafanikio hapa hapa Tanzania, ni wakenya, waganda n.k wangapi wenye mafanikio ndani ya nchi zao?. Acha kauli zisizo za msingi.

3.    Sina elimu ya kutosha, hii ilikuwa na umuhimu enzi zile za zama za kati za mawe lakini sio katika dunia ya sasa ya taarifa. Nani aliyekuambia mafanikio ni kutokana na elimu yako tu?, wangapi wanamafanikio makubwa na hawana hata digrii, masters, wala hizo phd ambazo wewe unaamini lazima uwe nazo ndizo zitakufanya ufanikiwe. Chukulia mfano wa mafanikio ya msanii Diamond na msakata kabumbu  Mbwana Samatta, je wanaelimu kiasi gani?. Jibu baki nalo.


4.    Hayo ni mambo yako sio yangu, kauli kama hizi ndizo huwafanya watu wakose fursa. Utamkuta mtu analetewa wazo la kibiashara ambalo tayari ni fursa kwake lakini utamsikia aa bwana ee hayo ni mambo yako sio yangu. Sasa endelea hivyo hivyo na utaendelea kukosa fursa siku hadi siku.

5.    Sina muda wa kutosha, wewe kila siku muda haukutoshi, wewe ni nani na unafanya nini mpaka muda usikutoshe kila siku?, je unataka upatiwe masaa 70 ndani ya siku moja? Kwanini wewe tu ndio muda haukutoshi? Mbona wengine masaa 24 yanamtosha. Jifunze kutumia muda ulopewa vizuri.


6.    Sina pesa za kutosha, unafikiri pesa inatosha kwa kukaa nayo tu? Au kwa kuiweka tu ndani na kuishangaa au benki?,  acha kufikiri pesa itakuja kukutosha bila kuizungusha, jifunze kuizungusha hiyo pesa ndipo itakutosha.

7.    Sifahamiani na watu sahihi, ni kweli hufamiani na watu sahihi kutokana na matendo yako na ndio maana huwezi kuwapata watu sahihi wa kukusukuma uende mbele. Kama unataka kupata kushirikiana na watu sahihi anza kufanya mambo yanayoendana na hao watu ambao kwako ni sahihi.


8.    Sina mtandao wa watu, hauna mtandao wa watu wa kushirikiana nawe kutokana na wewe mwenyewe ulivyo. Mtandao wa watu wa kushirikiana nao unakuja kutokana na kile ambacho unakifanya na kutokana na ushirikiano wako na watu wengine. Unashirikiana na nani haswa na huyo unayeshirikiana nae je? anamtandao au?.

9.    Mke wangu hanisaidi, ni kweli mke wako hakusaidi lakini wewe kama wewe umechukua juhudi gani kuhakikisha kuwa wewe kama wewe unapigana vilivyo katika kuhakikisha kuwa unasimama wewe kama wewe?,  je mafanikio yako yanamtegemea mke wako tu?, kama asingalikuwepo ungalifanyaje?, acha kutegemea tegemea bila msingi badala yake  jifunze kusimama mwenyewe muda mwingine.


10. Nina watoto wengi wa kulea, kama ulijua kuwa watoto wengi wanakufanya usifanikiwe kwanini umekuwa nao?. Na je ni kweli kwamba bila kuwa na watoto wengi ungefanikiwa au ni visingizio?, je tukiwachukua hao watoto na tukakuacha mtupu utafanikiwa?

Kimsingi kauli hizi kumi kwa maneno mengine tunaweza kuziita kama visingizio ambavyo mtu huwa navyo, na hii ni hatari sana maana visingizio havikufanyi kuwa mwenye mafanikio bali vinazidi kukurudisha nyuma. Hivyo basi uamuzi ni wako kuendelea na visingizio na sababu sababu za kuto kufanikiwa kwako ambzao zitazidi kukufanya usiwe na mafanikio au uziache na kuwa mwenye mafanikio.

Ni mimi rafiki yako,
Baraka Maganga
Wasiliana nami kwa.
 Simu: 0754612413 au 0652612410.
Barua pepe: Bmaganga22@gmail.com



No comments:

Post a Comment