Saturday, January 9, 2016

Sababu Sita (6) Za Kwanini Watu Hawajiwekei Malengo.



Habari za leo ndugu msomaji wa mtandao huu wa kona ya maarifa ni matumaini yangu kuwa hu mzima wa afya na unaendeleo kupambana vilivyo katika kuhakikisha kuwa unajiletea mafanikio makubwa maishani mwako. Nami nakusihi ndugu msomaji wa mtandao huu kuwa endelea kupambana, usichoke hata siku mpaka uhakikishe kuwa unajipatia mafanikio makubwa, ambayo umekwisha jiwekea.
Ukiwa unaendelea kujishighulisha na shughuli zako za kila siku basi leo nakuletea kitu kingine ambacho unapaswa ukifahamu vyema. Kama  kichwa cha makala kinavyosema kuwa sababu za kwanini watu huwa hawajiwekei malengp maishani. Tumekuwa tukisisitizana na kuambiana mara nyingi sana juu ya umuhimu wa kuweka malengo, lakini ukweli ni kwamba ni watu wachache sana kati ya wengi ambao wamekuwa na utamaduni wa kujiwekea malengo. Na walio wengi wamekuwa hawajiwekei malengo, sasa kwanini watu hawa huwa hawajiwekei malengo maishani, zifuatazo ni sababu za kwanini watu hawajiwekei malengo:-,




Hawako makini, sababu moja wapo ya kwanini watu hawajiwekei malengo ni kutokana na sababu kuwa hawapo makini maishani. Mtu makini na anayetaka kufanikiwa kwa hali na mali lazima ajiwekee malengo. Lakini kutokana na ukosefu wa umakini miongoni mwetu tumekuwa tukiishi hivyo hivyo bila malengo
.
2.    Hawajayakubali majukumu yao, kama mpaka sasa hujathubutu hata kujiwekea malengo basi tambua kuwa bado hujataka kuyavaa majukumu yako. Yaani watu ambao bado hawajajiwekea malengo ni wale ambao bado wanahisi kuwa yupo mtu fulani maishani ambae ndiye yupo kwa ajili ya kusubiri kufanyiwa kitu fulani jambo ambalo kiukweli ni kujidanganya. Hivyo basi ukosefu wa ile hali ya kuvaa majukumu ndio kimekuwa kikwazo cha watu kujiwekea malengo.

3.    Hawatambui umuhimu wa kujiwekea malengo, watu wamekuwa hawajiwekei malengo kwa sababu hawajui umuhimu wa kujiwekea malengo. Inaonekana kuwa miongoni mwa watu wengi sana hawana uelewa juu ya maswala haya ya kujiwekea malengo ndio maana wamekuwa hawajiwekei malengo maishani mwao. Watu hawaoni umuhimu wowote wa kujiwekea malengo ndio maana wamekuwa hawajiwekei, lakini naomba niseme kuwa hii ni kosa kubwa sana ambalo watu hulifanya, nasema hivyo kwa sababu ni vyema kila mtu akatambua umuhimu wa kuweza malengo na akijua umuhimu atakuwa amejikomboa kwa kiwango kikubwa.

4.    Hawajui ni vipi watapanga/ kuyaandika malengo yao, sababu nyingine ambayo inawafanya watu wasijiwekee malengo ni kutokana na ukweli kwamba hawajui ni vipi wajiwekee malengo. Hii nadhani ndio sababu namba moja ya kwanini watu hawajiwekei malengo maishani, yaani hawaweki malengo kwa sababu hawajui watafanyaje. Kama hujui mpaka leo basi jua kuwa upo katika hatari.
5.    Wanaogopa kukosolewa/ kukataliwa, uoga umekuwa ukichangia sana miongoni mwa watu, na imekuwa sababu inayofanya watu washindwe kujiwekea malengo, watu wamekuwa wakiogopa kujiwekea malengo kwa kuwa wanaogopa kuwa endapo wakimwonesha mtu malengo yake atakosolewa sana hivyo kutokana na woga huu basi unamfanya arudi nyuma na kukaa bila kuweka malengo.

6.    Wanaogopa kushindwa, watu wengi hawaweki malengo kwa kuwa wanaogopa kushindwa yaani anaogopa kuwa itakuwaje nikiweka malengo alafu nisiyatimize hivyo kutokana na kuogopa huko katika kushindwa basi anakaa tu na kutokujiwekea malengo.


Ikiwa unataka kufanikiwa zaidi na zaidi ni muhimu ukatambua kuwa malengo ni kitu muhimu sana tena sana, malengo ni dira katika maisha yako. Ikiwa hujajiwekea malengo basi nishakuwekea sababu sita za kwanini hujafanya hivyo. Kupitia sababu hizo unaweza ukaelewa ufanye nini ili kujiwekea malengo. Mfano umeshajua sababu moja wapo inayokufanya usijiwekee malengo ni kuwa hujayakubali majukumu, sasa nini cha kufanya ni kuyavaa majukumu kisha baada ya hapo utapata uwezo na uelewa wa ni vipi ujiwekee  malengo.


Ni mimi rafiki yako,
Baraka Maganga
Wasiliana nami kwa.
 Simu: 0754612413 au 0652612410.
Barua pepe: Bmaganga22@gmail.com


No comments:

Post a Comment