Monday, January 4, 2016

Mambo (6) Muhimu Ya Kuzingatia Ili Uweze Kufanikiwa.


Habari ndugu msomaji wa mtandao huu wa kona ya maarifa, ni matumaini yangu kuwa unaendelea vizuri katika kuhakikisha kuwa unashughulikia ipasavyo yale unayo yahangaikia ili tu kujiletea mafanikio ambayo ndio kila mtu anayoyahangaikia. Nami nikusihi kwa moyo mmoja kuwa endelea kupambana mpaka uyatimize yale unayoyaamini kama mafanikio kwako. Pambana pambana bila kuchoka na mafanikio utayaona tu.
Wakati unaendelea kupambana katika kuhakikisha kuwa unafanikiwa ni vyema ukatambua kuwa yafuatayo ni mambo ya msingi ambayo yatakufanya ufanikiwe zaidi na zaidi. Mambo hayo ni yafuatayo:-


  Wazo, wazo ni kitu muhimu sana katika maisha ya binadamu lakini cha ajabu ni kuwa watu hawaelewi na badala yake wamekuwa wakihangaika na vitu vingine na kujikuta wakipoteza muda bure bila mafanikio na hatimaye huanza kuhangaika huku na kule na kutafuta tatizo la kutofanikiwa kwao kumbe tatizo ni kuwa mawazo yao ndio yenye matatizo. Kuna msemo maarufu miongoni mwa watu waliofanikiwa kuwa wazo ni pesa/fedha. Hivyo basi hata katika biashara wazo ndio mtaji muhimu kwa maana hiyo ni kuwa wazo ndilo huleta pesa sio pesa kuleta wazo. Na sio kila wazo huleta pesa bali lile wazo sahihi juu ya pesa ndilo liletalo pesa. Wataalamu wanasema tunakuwa kadri ya fikira zetu. Hivyo kama kweli unataka kufanikiwa jenga mawazo chanya akilini mwako juu ya maisha yako na utafanikiwa tu.

2.    Malengo,hili ni jambo la msingi sana maishani mwako. Zunguka kote duniani tafuta mtu yoyote aliyefanikiwa maishani na ambaye unaamini kuwa anamafanikio unayoyataka muulize siri ya mafanikio yake jambo la msingi atakalokuambia ni kuwa weka malengo. Malengo ni kama dira katika meli, meli haiwezi kwenda bila dira, ndivyo ilivyo kwa binadamu binadamu asiye na malengo juu ya maisha yake hana tofauti na mfugo ambao upo upo tu. Hivyo basi weka malengo kama kweli unataka kufanikiwa maishani.


3.    kujituma, hakika hakuna mtu awezae kufanikiwa pasipo kujituma katika shughuli zile zenye kumletea maendeleo. Kujituma ni jambo la msingi sana maishani jitume katika shughulli zako, zifanye kwa kujitoa kisawasawa, hakikisha unafanya shughuli kiuhakika usifanye tu bora umefanya bali fanya kama mtu anayejielewa kuwa anafanya kitu chenye tija kwake na hapo ndipo utauona umuhimu wa kujituma. Na hatimae mafanikio utayaona.

4.    Uwajibikaji, kama hutaki kuwajibika katika shughuli zako jua kuwa mafanikio kwako yatapita kushoto. Hili naomba nikuambie dhahiri hata kama ikitokea leo umeanzisha kampuni ukaajili wafanyakazi usikae ukabweteka kuwa si kunawafanyakazi watafanya tu, usikae nyumbani kuangalia tamthiliya eti kisa umewaajili watu wanakufanyia kazi. Jiunge nawe kuwa sehemu ya wafanyakazi na utayaona mafanikio kwa kuwa wewe ndiye mwenye wazo la kuanzisha kampuni husika wala sio wafanyakazi hivyo ukiwaachia wafanyakazi pekee hii inamaanisha kuwa umejitoa na wazo lako pia umetoka nalo hivyo basi ni rahisi sana kwako kushindwa kufanikiwa. Uwajibikaji umekuwa tatizo kubwa sana miongonui mwa watanzania wengi ndio maana leo hii utawakuta watu wakiilaumu serikali hata kwa yale ambayo ilibidi wayafanye wao wenyewe.


5.    Kujiamini, maishani lazima ujiamini, amini kuwa unaweza kufanya mambo makubwa na kuwa na mafanikio makubwa sana maishani japo watu wengi wanaweza kuwa wanakukatisha tama kwa kusema kuwa hauwezi lolote. Hakuna aliyezaliwa anajua kila kitu au anajua bali kila mmoja wetu hujifunza kupitia watu fulani, hivyo basi kama waliweza kujifunza basi hata wewe unaweza kujifunza pia. Jambo la msingi ni kujituma, kuweka nia na kuwa na imani kuwa unaweza.

6.    Shirikiana na watu sahihi, sio lazima ushirikiane na kila mwanajamii maana jamii ina watu tofauti tofauti na kila mtu huwa anachagua lile kundi analoliona kuwa lina tija kwake na sio kila mtu. Leo hii inabidi uchague ni nani haswa wa kushirikiana nae na ni kwanini kama unataka kufanikiwa shirikiana na watu wenye mtazamo chanya. Tambua kuwa kila watu hukaa katika makundi yanayofana nao hivyo usije ukajichanganya ukaka katika kundi lisilo kufaa maana utaumia na laweza kuwa kikwazo cha kufanikiwa kwako.

Ni mimi rafiki yako,
Baraka Maganga
Wasiliana nami kwa.
 Simu: 0754612413 au 0652612410.

Barua pepe: Bmaganga22@gmail.com

No comments:

Post a Comment