Habari za leo mpendwa msomaji wa mtandao huu wa kona ya
maarifa ni matumaini yangu kuwa hu mzima wa afya na unaendelea vizuri katika
kuhakikisha kuwa unaupokea mwaka mpya vizuri ikizingatiwa kuwa tumebakiza masaa
sasa kuukamilisha mwaka 2015 na kuingia mwaka mpya wa 2016. Basi katika
kumaliza mwaka nataka umalize na wazo hili ili ukalitumie vizuri mnamo mwaka wa
2016 na kuendelea.
Je unazijua silaha muhimu za watu waliofanikiwa?, pengine
unazijua baadhi kama vile kujiamini, kujituma, kujiwekea malengo, uwajibikaji,
kushirikiana na timu sahihi n.k. hizo ni baadhi kati ya silaha nyingi ambazo
waweza kuwa unazijua, lakini leo nakupatia silaha moja muhimu sana ya watu
waliofanikiwa na kwa kuwa nawe unataka kufanikiwa ichukue na uitumie silaha hii
ipasavyo.
Matumizi sahihi ya muda, hii ndio silaha muhimu ya watu
waliofanikiwa na kama nawe kweli unataka kufanikiwa hakikisha unaichukua silaha
hii na kuitumia katika safari yako. Watu waliofanikiwa wanajua kutumia muda ipasavyo,
wanajua kuwa kwa kila siku tuna masaa ishirini na nne (24) na katika hayo masaa
kuna muda wa uzalishaji na muda usio zalishi (uzalishaji). Kwa kutambua hilo
uhakikisha kuwa hawapotezi muda ovyo.
Watu waliofanikiwa wanatumia muda wao mwingi sana katika
shughuli zao na sio katika starehe wala kupumzika, au kuangalia televisheni.
Hii ni kwa kuwa wanatambua kuwa kuna muda wa uzalishaji na muda usio zalishi na
kwa kuwa wanalitambua hilo basi wao hutumia muda vizuri katika shughuli zao
yaani kama ana biashara basi muda mwingi sana atautumia katika biashara yake na
sio kukaa kijiweni kupiga stori. Na kama ni mwekezaji basi muda wake mwingi
atautumia katika shughuli zake za kiuwekezaji.
Watu waliofanikiwa wanatumia muda wao vizuri kwa kuwa
wanajua kuwa muda ni mali ya kipekee ambayo ukiipoteza huwezi kuitafuta na
kuipata tena yaani wao wanafalsafa ya kuwa muda ni kitu cha kipekee kisichoweza
kurudishwa. Kama kweli unataka kufanikiwa naomba ujenge picha hii akilini mwako
ili ukusaidie kuutumia muda wako vizuri. Ufananishe muda wako sawa na mafuta
katika gari, mafuta katika gari ni kitu cha muhimu sana maana bila mafuta gari
haliwezi kwenda popote, lakini mafuta haya huwa hayana kuongezeka bali ni
kupungua tu na hatimaye kuisha ambapo ukitaka gari liendelee kwenda inabidi
ukatafute mengine (kununua), uweke ndipo gari liendeleee na safari zake. Ndivyo
ulivyo muda kama ambavyo hakuna nyongeza ya mafuta katika tenki la gari basi
hata muda ni hivyo hivyo yaani tuna masaa ishirini na nne kwa siku moja basi
hakuna pungufu wala nyongeza ya hapo. Hivyo basi inabidi ujifunze kufanya
shughuli zako ipasavyo kulingana na muda
husika uliopewa.
Muda ni kitu ambacho kimekuwa kikidharauliwa na
watanzania wengi sana tena sana na kwangu mimi matumizi mabovu ya muda ni
sababu moja wapo ya watu wengi kutofanikiwa maishani. Watanzania wengi sana
tumekuwa na tatizo ya kutojua kutumia muda na ndio maana hatuuthamini. Hauwezi
kukithamini kitu bila kujua umuhimu wake, leo nataka utambue kuwa muda ni kitu
muhimu sana tena sana na kwanzia sasa anza kuuthamini muda maana muda unaweza
kuwa kigezo cha kutofautisha mafanikio na kushindwa.
Dunia imebadilika na itaendelea kubadilika na kubadilika,
maendeleo ya sayansi na teknolojia yameleta vitu vingi sana vya kukuibia muda
usipokuwa makini utajikuta kila siku ukiwauzia watu wengine muda bila wewe
kunufaika na chochote bali kuwanufaisha wengine, zinduka wewe ukiyekatika
usingizi mzito, acha kupoteza muda wako ovyo kwani muda ni rasilimali muhimu
kwako ambayo ni ya bure kabisa kwako.
Ni
mimi rafiki yako,
Baraka
Maganga
Wasiliana
nami kwa.
Simu:
0754612413 au 0652612410.
Barua pepe:
Bmaganga22@gmail.com.
No comments:
Post a Comment