Wednesday, December 30, 2015

Jifunze Kupitia Vitu Hivi Viwili.


Habari za leo ndugu msomaji wa mtandao huu wa kona ya maarifa ni matumaini yangu kua hu mzima na waendelea vizuri katika kuyasaka mafanikio. Kama ilivyokawaida ya mtandao huu, ambao umejidhatiti katika kuhakikisha kuwa unakupatia maarifa ambayo ukiyatumia vyema yatakuwa kama chachu na kirainisho katika safari yako ya mafanikio. Leo natakaa ujifunze jambo hili nndugu msomaji nalo ni kujifunza kupitia vitu hivi viwili. Je vitu hivyo ni vipi?, endelea….
Leo nataka ujifunze kupitia vitu viwili kama nilivyokutambulisha hapo awali lakini najua vitu hivyo bado ni fumbo kwako. Basi vitu hivyo ni hivi hapa:-


1.       Vikwazo, najua wengi wetu tunaamini kuwa vikwazo vipo kwa ajili ya kutuzamisha au kutukwamisha na kutudidimiza kabisa na kutufanya tusipige hatua yoyote ile katika maisha. Hii ni imani ya watu wengi juu ya vikwazo.  Sasa leo nataka uvunje hii imani kabisa maana haina msingi wowote kwa wale ambao wanataka mafanikio,lakini kama hautaki kufanikiwa endelea kushikiria imani hiyo hivyo hivyo ilivyo.
Nimesema uachane na imani kuwa vikwazo vipo ili vikukwamishe na badala yake tumia vikwazo kama somo ambalo ukilielewa basi itakuwa chachu ya mafanikio yako. Vikwazo huja kwa malengo fulani haviji tu. Vikwazo vinaweza kuja kwa sura kama hizi:-
(a)    Vikwazo huja ili kutukomaza, kumbuka kuwa safari ya mafanikio sio safari nyoofu siku zote na wala sio safari rahisi, hivyo basi uwepo wa vikwazo upo ili kutukomaza vyema. Kabla hujapata mafanikio vikwazo vipo ili kukufanya ukabiliane navyo na ukishaweza kufanya hivyo hata pale utakapofanikiwa basi hata vikija vikwazo wewe utakuwa na uzowefu navyo na hivyo hauto shindwa kupambana navyo.  Yaani vikwazo ni kama mafunzo ya awali kwa askari ambaye hajawa askari bado.
(b)   Vikwazo huja kupima imani zetu, muda mwingine vikwazo huja kama kipimo cha imani zetu yaani kupitia vikwazo imani zetu hupimwa. Tambua kuwa kuna uhusiano wa moja kwa moja kati ya mafanikio na imani ya mtu yaani anaeamini kuwa atafanikiwa mara nyingi huwa anafanikiwa na asiye amini kuwa atafanikiwa nae huwa hivyo. Hivyo basi vikwazo huja kupima imani zetu. Kumbuka mfano wa ayubu katika biblia ambaye aliwekewa vikwazo mbalimbali ili tu kupimwa imani yake.
(c)    Vikwazo huwa kipimo cha uvumilivu, mafanikio huusisha watu ambao ni wavumilivu watu ambao wanaweza kukisubiria kile wanachokitaka hata kwa miaka saba mpaka kumi hata kama hakiji. Na wala hayahusishi watu ambao wanakata tama kirahisi rahisi. Hivyo basi vikwazo huja ili kutaka kupima uvumilivu wako.
2.       Makosa, hakuna asiyekosea  katika kutaka kujifunza kitu hapa duniani, ni vyema ujenge tabia ya kujifunza kupitia makosa yako na wala sio vinginevyo. Unapofanya makosa usianze kujilaumu kuwa kwanini imekuwa hivi au kwanini nimefanya hivi nina tatizo gani. Bali jifunze kupitia makosa unayoyafanya maana ni jambo la kawaida kukosea. Pengine makosa huweza kuwa na malengo haya yafuatayo:-
(a)    Kukurekebisha, makosa huja ili yakurekebishe na hii hutokea haswa pale ambapo unajiona au kujikuta kuwa umekamilika. Mfano unaweza kuwa unajifunza ukajiona umeshafuzu masomo husika, kwa kuwa hakukuwa kosa ambalo ulilifanya hapo awali hivyo kosa linapojitokeza linakuwa limekuja kukurekebisha ili ujue kuwa bado kuna mengi inabidi ufanye.
(b)   Kukuongezea ujuzi, makosa huja ili kukupatia ujuzi mpya hasa kwa yale mambo ambayo ulikuwa huwezi kuyafanya katika hali ya kujaribu hiki na kile alafu ukawa unakosea hapo ndipo hujikuta umepata ujuzi fulani.
(c)    Kukufanya uende na wakati, hii hutokea kwa wale ambao hufanya mambo kwa mazoea, pindi wafanyapo makosa kutokana na kuwa wamefanya vitu kinyume na wakati ndipo huwa wanashituka kuwa wapo nyuma ya wakati. Nini kimewafanya washituke basi, hakika ni makosa waliyoyafanya.
Kimsingi mtu anaetaka kufanikiwa huwa anatumi vikwazo na makosa kama darasa na wala sio kama nuksi au mkosi. Hivyo basi jifunze nawe kufanya hivyo maana naamini unatamani kufanikiwa na utafanikiwa tu.
Ni mimi rafiki yako,
Baraka Maganga
Wasiliana nami kwa.
Simu: 0754612413 au 0652612410.
Barua pepe: Bmaganga22@gmail.com. 

No comments:

Post a Comment