.Habari za wakati huu ndugu msomaji wa mtandao huu wa kona
ya maarifa ni matumaini yangu kuwa hu mzima wa afya na unaendelea kupambana kwa
hali na mali ili tu uweze kufanikisha yale ambayo umekuwa ukiyahangaikia mara
kwa mara. Vizuri endelea kupambana naama hakuna kitu cha bure hapa duniani,
maana hata miujiza huja kwa wale ambao huwa wanakuwa wakiitafuta miujiza hiyo.
Sio waliokaa tu wakisubiri miujiza hivyo nakusihii endelea kupambana ndugu
msomaji wa mtandao huu.
Ikiwa unapambana katika kuhakikisha unasonga mbele na
wala sio kurudi nyuma basi ni vyema ukaelewa kuwa kitu hiki kimoja kisikutishe
sana maana ni lazima kiendelee kuwepo hapa duniani, yaani usikihofie kitu hiki
kwa maana ni cha muhimu sana tena sana. Kitu chenyewe ni tofauti zilizopo baina yetu sisi wanadamu. Ni wazi na ukweli
usio pingika kuwa binadamu tunatofautiana sana tena sana na kwa kiasi kikubwa,
kama ulikuwa hujui kuwa binadamu tunatofautiana basi anza kuelewa kwanzia sasa
kuwa binadamu tunatofautiana na tofauti hizi zipo baina yetu na zinajionesha
wazi wazi miongoni mwetu. Ngoja nikuwekeee mifano kadhaa ili uwezo kuelewa ni
namna gani binadamu tunatofautiana tena kwa makundi tofauti tofauti.
Mfano katika maisha ya kawaida utofauti wetu unaweza
kujionesha kutokana na shughuli au kazi
zetu, ndio maana katika maisha tuna madaktari, tuna manesi, tuna waalimu, tuna
wafanyabiashara, tuna madereva, tuna wasio waajiriwa, tuna wawekezaji pamoja na
wajasiliamali n.k. bado katika makundi hayo hayo yanatofauti pia mfano katika kundi la
madaktari tuna madaktari bingwa wa macho na wale bingwa kwa magonjwa ya watoto,
katika waalimu tuna waalimu wakuu na waalimu wasio na cheo au kitengo chochote,
katika kundi la madereva tuna madereva wa mabasi ya mikoani, daladala na
madereva wa malori. Huu ni ufafanuzi kidogo ambao unaonesha jinsi gani binadamu tunatofautiana sana tena sana.
Sasa utofauti huu usikutishe maaana haupo ili ukutishe
bali upo ili kukupa changamoto na fursa wewe ili upate kuelewa ni wapi ambapo
panakufaa haswa. Utofauti huu upo ili kukufanya wewe ufanye uchaguzi sahihi ni
kundi gani linakufaa haswa na ni wapi unapataka. Hivyo basi badala ya kutishika
na utofauti huu wewe chukulia utofauti huu kama fursa ya wapi panakufaa.
Usitishike wala kuogopa unapoona mtu fulani kawa mfanyabiashara maarufu, fulani
kawa daktari bingwa, kawa mchezaji bora, kawa mwamasheria n.k bali chukulia
kama fursa ya wewe kuchagua ni wapi haswa panapokufaa na upange ni jinsi gani
haswa utaweza kufika pale.
Pia ni muhimu ukatambua kuwa utofauti huu wa kimaisha
unaweza kukusaidia wewe kufanya mambo fulani fulani, mfano utofauti unaweza
kupelekea yafuatayo kwako:-
1) Utofauti huu ndio hutukumbusha ya kuwa
tunapaswa kuwajibika, kupitia tofauti zilizopo au zinazojitokeza
kati yetu ndizo huwa kichocheo cha sisi kupambana ili kuhakikisha kuwa
tunasonga mbele au kupata molari ya kujikwamua katika hali ambazo tunazo. Hebu
chukulia mfano ni hali gani huwa unakuwa nayo pindi unapokutana na rafiki yako
ambaye mnaendana kwa baadhi ya vitu kama vile umri, elimu, historia ya kimalezi
na zaidi mlisoma na kucheza pamoja lakini
baada ya kuacha nae kwa muda anarudi akiwa na mafanikio makubwa sana
kuliko wewe, tayari mmeshatofautiana japo mlikua na kusoma pamoja, sasa baada
ya kuyaona mafanikio ya huyo rafiki yako, ni nini unachopata kwa mara ya kwanza?.
Nadhani ni hisia za kuwajibika ili uweze kuwa kama rafiki yako.
2) Hutufanya tuzichukie hali fulani,
kupitia utofauti tulionao basi hutufanya tuzichukie baadhi ya hali zetu. Mfano
pindi unapowaona wenzio wakifanikiwa ili hali wewe unabaki kuwa masikini wa
kutupwa basi hapa ndipo huwa unapata hasira na kuanza kuuchukia umasikini
lakini kiuhakika ni kuwa usingeweza kupata hasira ya kuichukia hali hii ya
umasikini. Lakini sababu ya kukufanya uanze kuuchukia umasikini ni baada tu ya
kuona tofauti iliyopo kati yako na wengine.
3) Hutufanya tujifunze zaidi,tofauti
zilizopo baina yetu na wengine wakati mwingine huwa kama somo kwetu maana
tofauti hizi hutufanya tuanze kujihoji sana ni kwanini wengine wako hivi na
sisi tuko hivi. Mfano leo hii unapata wazo gani unapowaona watu waliofanikiwa
mbele yako, sina shaka kuwa itakuwa uwa unapata hamu ya kujifunza zaidi kutoka
kwa watu hao.
Ni muhimu tofauti ziendelee kuwepo
miongoni mwetu ili tuweze kuchagua ni wapi panatufaa, ili tuweze kubadilishana
huduma maana wote tukiwa wafanyabiashara
nani atakuwa mnunuzi tena isitoshe wote tukiwa tunauza bidhaa sawa, ingekuwaje
kama wote tungekuwa madereva na kila mtu, angelikuwa na gari lake, bila shaka
kusingekuwepo abiri kwa sababu hizo na nyingine nyingi ni dhahiri kuwa tofauti
ni lazima ziendelee kuwepo miongoni mwetu.
Ni mimi rafiki yako,
Baraka Maganga
Wasiliana nami kwa.
Simu: 0754612413 au 0652612410.
Barua
pepe: Bmaganga22@gmail.com
No comments:
Post a Comment