Thursday, January 21, 2016

Furahia Vitu Hivi Wala Usilaumu Sana Juu Yake.

Habari za wakati huu ndugu msomaji wa mtandao huu wa kona ya maarifa ni matumaini yangu kuwa hu mzima wa afya na unaendelea kupambana kwa hali na mali ili tu uweze kufanikisha yale ambayo umekuwa ukiyahangaikia mara kwa mara. Vizuri endelea kupambana naama hakuna kitu cha bure hapa duniani, maana hata miujiza huja kwa wale ambao huwa wanakuwa wakiitafuta miujiza hiyo. Sio waliokaa tu wakisubiri miujiza hivyo nakusihii endelea kupambana ndugu msomaji wa mtandao huu.






Ukiwa bado unaendelea kupambana katika harakati zako basi jifunze kufurahia mateso,matatizo na vipingamizi mbalimbali uvipatavyo kwa sasa. Kwanini nasema jifunze kuyafurahia mateso, matatizo na vipingamizi vya sasa?. Sababu ninazo kupa hapa basi zinaweza kuwa muhimu kwako kuweza kukufanya uyafurahie mateso, matatizo na vipingamizi kadha wa kadha.
1.    Vinakufunza,ni kweli kuwa watu tulishawahi kupita, tunapitia na pengine tunaweza kuja kupitia katika mateso, matatizo na vipingamizi vya aina mbalimbali. Kama ulishawahi kupita katika mateso, vipingamizi au matatizo fulani basi utakubaliana nami kuwa vitu hivi huwa vinafunza. Jiulize swali hili huwa unajisikiaje pindi unapokuwa unapitia katika matatizo?, au pindi unapopitia vipingamizi fulani?, kama huwa unachukulia vitu hivi kwa hasira alafu unaanza kulalamika basi tambua kuwa una mtazamo hasi, na hivyo inabidi ubadili mtazamo huu na ujenge mtazamo wa kuyaangalia mateso, matatizo na vipingamizi vyako kwa hasira kisha acha kulaumu na baadae jiulize umejifunza nini kutokana na mambo hayo?. Huwa unajifunza nini pindi unapopingwa na wenzio je? unajawa na hasira na kuishia kulaumu au huwa unapatwa na hasira na unajifunza kuwa unapaswa kubadilika pengine unapingwa kutokana na kutokuwa bora katika jambo fulani, hivyo jifunze kutokana na kupingwa na ukajiboreshe zaidi na zaidi. Mateso unayoyaona leo yageuze kuwa kama somo. Matatizo pia yawe somo mfano unapokuwa na tatizo la pesa unajisikiaje?, unakubali hali au unajifunza na kulitatua tatizo hilo.

2.    Vinakuimalisha, matatizo, vipingamizi na matatizo, muda mwingine huwa kama viimalisho vyetu. Mfano matatizo yako yapo ili kukufanya uwe bora zaidi na zaidi. Mfano unapopata pingamizi kutoka sehemu mbalimbali kama vile unapopingwa kutokana na kigezo cha ukosefu wa elimu katika sehemu fulani ni muda wa kwenda kujiimalisha sasa ili uwe bora zaidi na usije ukapigwa tena na tena. Mateso muda mwingine usiyachukulie kama yapo kwa ajili ya kukutesa bali yapo kwa ajili ya kukuimalisha zaidi katika Nyanja mbalimbali za maisha.

3.    Vinakuamsha katika usingizi mzito, mateso, vipingamizi na matatizo yapo ili  kukuamsha katika usingizi mzito ambao umelala. Mfano halisi ni kuwa sisi binadamu huwa tunakumbwa na hali ya kujisahau pindi tunapojikuta kuwa tumefanikiwa kwa kiasi fulani na hapo ndipo wakati mwingine vipingamizi huja kwa ajili ya kutuamsha kutoka katika usingizi mzito ambao huwa tunakuwa tumelala pengine ni kutokana na baadhi ya mafanikio ambayo tunakuwa tumelala kwa muda. Binadamu huwa tunakuwa na hali ya kujisahau sana pindi tunapokuwa tumeona kuwa hali kwetu ni nzuri na hapo huwa tunajisahau sasa kwa wakati huu ndio huwa ni muhimu sana tena sana kuweza kuamshwa kutoka katika usingizi huu tulio lala. Matatizo mengi huja kwetu ili kutuamsha kutoka katika usingizi mzito tuliokuwa tumelala na hivyo kuweza kutuamsha. Mfano kama mfanyabiashara ukiwa umezoea kupeleka biadhaa zako mahali Fulani kwa wateja wako, kutokana na kufanya biashara kwa mazoea maana unafanya tu hutaki kuboresha bidhaa zako siku bidhaa yako ikipingwa na wateja wako, utakuwa umeamshwa sana. Pengine unateswa kwa kuwa umelala sasa inatakiwa uamke ili usiendelee kuteseka kama ukiendelea kulala maana yake utaendelea kuteseka.

Hivyo basi furahia mateso, matatizo na vipingamizi kwa maana ndani yake vimebeba mafunzo zaidi na zaidi.
Ni mimi rafiki yako,
Baraka Maganga
Wasiliana nami kwa.
 Simu: 0754612413 au 0652612410.
Barua pepe: Bmaganga22@gmail.com



No comments:

Post a Comment