Habari za wakati huu ndugu msomaji wa mtandao huu wa kona
ya maarifa ni matumaini yangu kuwa hu mzima wa afya na unaendelea kupambana kwa
hali na mali ili tu uweze kufanikisha yale ambayo umekuwa ukiyahangaikia mara
kwa mara. Vizuri endelea kupambana naama hakuna kitu cha bure hapa duniani,
maana hata miujiza huja kwa wale ambao huwa wanakuwa wakiitafuta miujiza hiyo.
Sio waliokaa tu wakisubiri miujiza hivyo nakusihii endelea kupambana ndugu msomaji
wa mtandao huu.
Naamini umekuwa ukipambana sana katika kuhakikisha kuwa
unafanikiwa katika yale ambayo unayahangaikia nami na kusihi uendelee kupambana
maana katika mahangaiko ndiko mafanikio hutokea. Lakini lazima ujue kuwa lazima
kitu hiki ukifanye kama unataka kufanuiki. Kitu hiki ni kitu muhimu sana katika
maisha yetu na mafaniko kwa ujumla lakini jambo la kushangaza ni kuwa tumekuwa
hatulitili maanani sana na ndio maana wengi wetu tumekuwa tukijikuta hatusongi
mbele wala nini ila tunabaki pale pale au kurudi nyuma kabisa kimaisha.
Huwa unapata picha gani pindi unapoona mfanyakazi fulani katika
kampuni fulani kafukuzwa kazi. Au kasimamishwa kazi kwa muda. Unapata picha
gani pindi unapomwona mfanyabiashara fulani kashindwa kibiashara yaani biashara
yake imekufa. Unapata wazo gani unapomwona mtu anailaumu serikali yake kwa
kushindwa kwake wakati yeye ndiye aliyepaswa kufanya jambo husika. Hakika yote
hayo hutokea kutokana na kukosekana kwa kitu hiki kimoja nacho ni uwajibikaji.
Maishani bila kuwajibika tambua kuwa hauto kwenda kokote
kule bali utaishia pale pale. Dunia ya sasa imejaa ushindani wa hali ya juu
ambao unaongezeka siku hadi siku na atakae weza kusitaimili ushindani huu ni yule
tu mwenye kuweza kuwajibika ipasavyo. Kama wewe ni mfanyabiashara na
unawajibika bora liende tambua kuwa hauto kwenda popote bali utaishia kufulia
tu. Mfanyakazi pia ambae hutaki kuwajibika tambua kuwa utaishia tu kufukuzwa
kazi yako hiyo na hatimae kuukaribia umasikini nao utakukaribisha vizuri sana
kuliko unavyodhani.
Leo hii takwimu zinaonyesha kuwa kati ya biashara mia
moja zinazo anzishwa leo baada ya miaka kumi ni biashara chini ya ishirini
ndizo huwa zimekuwa. Hii ni kutokana na uwajibikaji mbovu wa wafanyabiashara
husika. Wafanyabiashara hawa wamekuwa hawahangaiki katika kutafuta taarifa
sahihi kabla ya kuzianzisha biashara zao na vile vile wamekuwa wagumu wa kuendelea
na utafiti baada ya kuanzisha biashara zao, hivyo hata yakitokea mabadiliko wao
hawashituki wala nini. Bali huendelea kufanya biashara zao kwa mazoea na
matokeo yao hujikuta wamefulia maana hujikuta hawapati wateja. Hii ni kutokana
na uvivu ulio letwa na kuto taka kuwajibika kwao na ndio maana wanajikuta
wameanguka.
Ukiwa mfanyakazi unajisikiaje pale unapoambiwa
tunakuwajibisha kutokana na utendaji wako mbovu angalia leo hii ni watu wangapi
wamesimamishwa kazi toka uongozi wa awamu ya tano uingie madarakani na wote
sababu zimekuwa zikionekana ni uwajibikaji mbovu na mengine, lakini kubwa ni
uwajibikaji mbovu ambao huwapelekea wafanye mambo kiholera holera na matokeo
yake ni kuja kuwajibishwa.
Kama unataka kufanikiwa hakikisha unayavaa majukumu yako
usisubiri mazingira yaje ya kushitaki na kukuwajibisha vikali. Au usisubiri
kufulia kukuwajibishe, ukiwa mfanyabiashara usisubiri anguko la biashara
likuwajibishe, mfanyakazi usisubiri kuwajibishwa na bosi wako bali vaa majukumu
yako mwenyewe na mafanikio utayaona tu. Ikiwa unasubiri kuwajibishwa basi sahau
kuhusu mafanikio na usilizungumzie tena neno hilo.
Ni mimi rafiki yako,
Baraka Maganga
Wasiliana nami kwa.
Simu: 0754612413 au 0652612410.
Barua
pepe: Bmaganga22@gmail.com
No comments:
Post a Comment