.
Habari za wakati huu ndugu msomaji wa mtandao huu wa kona
ya maarifa ni matumaini yangu kuwa hu mzima wa afya na unaendelea kupambana kwa
hali na mali ili tu uweze kufanikisha yale ambayo umekuwa ukiyahangaikia mara
kwa mara. Vizuri endelea kupambana naama hakuna kitu cha bure hapa duniani,
maana hata miujiza huja kwa wale ambao huwa wanakuwa wakiitafuta miujiza hiyo.
Sio waliokaa tu wakisubiri miujiza hivyo nakusihii endelea kupambana ndugu
msomaji wa mtandao huu.
Je unakumbwa na wasiwasi wa kufanikiwa kutokana na
historia yako ya nyuma zile kauli wanazokuambia wanaokuzunguka zinakurudisha
nyuma katika hali ya kutaka kusonga mbele katika kuhakikisha kuwa unafanikiwa
katika maisha yako. Je? unajua ni kwa nini kauli ulizopandikizwa kutoka
utotoni zinaendelea kukurudisha nyuma
katika safari yako ya kuyaelekea mafanikio, ni kwasababu umeziamini na
kuzifanya kuwa ukweli wako. Sasa jiambie mwenyewe kuwa ni wakati wa kuachana nazo sasa.
Zile imani ulizojijengea zamani ya kuwa hutofanikiwa na
kuwa tajiri kwa kuwa wazazi wako ni masikini, imani ya kuwa huto fanikiwa kwa
kuwa wazazi wako ni masikini, ni muda wa kuachana nazo maana hazina msingi
wowote na wala hazikujengi wala kukusaidia chochote bali zinakudidimiza zaidi
na zaidi badala yake wewe pambana kweli kweli hata kama unatokea katika familia
masikini, na mafanikio utayaona tu, maana wapo waliokuwa kama wewe na
waliotokea chini kama wewe na wakafanikiwa hivyo hilo lisikupe shide sana bali
achana na hiyo imani.
Uliambiwa kuwa wewe ni mjinga na hauwezi chochote na
mwalimu wako, ni wakati wa kuachana na kauli hii ambayo ulikuwa umeiamini kwa
kuwa ilitoka kwa mwalimu wako na kupitia kigezo cha sifa ya ualimu basi
ukaamini kuwa hauto fanikiwa fanya kama Thomas
Edison ambaye pamoja na kukataliwa na walimu watatu tofauti kuwa hafai kuwa
mwanafunzi wa kujifunza chochote lakini alijifunza na kuwa mwanasayansi mkubwa
duniani na mpaka leo anaheshimika kama mwanasayansi mashuhuri duniani. Hii ni
kutokana na sababu kuwa yeye aliachana na kauli za waalimu wake, hivyo basi
hata wewe unaweza kufanya hivyo na ukafanikiwa pia, hivyo achana na kauli mbovu
alizokuambia mwalimu wako.
Walikuita mbumbumbu mtaani kwenu, mtaani kwenu wewe ndio
ulionekana kuwa mtoto mbumbumbu kuliko wote na ukafutwa kabisa kwenye watoto
ambao wanaweza kuleta mabadiliko yoyote au kuleta mafanikio yoyote ambayo
yataisaidia jamii yako na wewe ukaamini kuwa kweli hauwezi kutokana na maneno
yao. Ni muda sasa wa kuachana na kauli hizo ambazo hazina msingi wowote bali ni
za ukatishaji taama.
Lazima utambue kuwa
tunakuwa kadri tunavyofikiri, hata bibilia imeliandika hilo kuwa kadri
ajionavyo mtu nafsini mwake ndivyo huwa. Hii inamaana kuwa wewe mwenye ndiye
mwamuzi wa maisha yako yaani ni kadiri unavyojiona wewe mwenyewe ndivyo huwa unakuwa.
Na biblia haijasema kadri wamwonavyo watu ndivyo mtu huwa, hilo ni jambo ambalo
halijaandikwa wala kusemwa. Hivyo basi kama wamesema hauwezi kufanikiwa ni wao
na sio wewe, wewe usizifuate kauli zao ambazo hazina msingi wowote bali wewe
endelea kushikilia ukweli ambao unauona nafsini mwako na katika kuushikilia
ukweli huu uwe ni ukweli ule ambao ni chanya achana na kauli hasi kabisa maana
hazikufikishi popote.
Kumbuka nimesema ni muda wa kuachana nazo zile kauli zote
ambazo ni hasi, ni muda wa kuachana nazo maana hazina msaada kwako ila zina
kudumaza na kukudidimiza zaidi na zaidi. Na kubwa zaidi juu ya kauli chanya ni
kuwa haziwezi kukuletea mafanikio yoyote.
Twende
sote.
Ni mimi rafiki yako,
Baraka Maganga
Wasiliana nami kwa.
Simu: 0754612413 au 0652612410.
Barua
pepe: Bmaganga22@gmail.com
No comments:
Post a Comment