Habari za wakati huu ndugu msomaji wa mtandao huu wa kona
ya maarifa ni matumani yangu kuwa hu mzima na unaendelea vizuri katika
kupambana ili kuhakikisha kuwa
unapata kile unachokitafuta katika maisha. Kwa kuwa lengo la mtandao huu ni kuhakikisha kuwa unapata vitu vya kukusukuma mbele zaidi katika kuelekea safari yako hiyo ya mafanikio, basi nasema pambana endelea kupambana bila kuchoka hata pale unapohisi umechoka jilazimishe maana kuridhika baaada ya hatua chache huleta anguko.
unapata kile unachokitafuta katika maisha. Kwa kuwa lengo la mtandao huu ni kuhakikisha kuwa unapata vitu vya kukusukuma mbele zaidi katika kuelekea safari yako hiyo ya mafanikio, basi nasema pambana endelea kupambana bila kuchoka hata pale unapohisi umechoka jilazimishe maana kuridhika baaada ya hatua chache huleta anguko.
Mafanikio yanahusu kulipia gharama je upo tayari kulipia
gharama hizo?. Ndio mafanikio yanahusu kulipia gharama, mbona unashituka ndugu
msomaji, nakuona ukiwa umeanza kutahamaki baada ya kusikia kuwa mafanikio
yanahusu gharama. Hii ni kwa kuwa umeanza kuhusianisha gharama na pesa hivyo
umeanza kuhisi ni kama unahitaji kujiandaa kwa kiwango fulani cha pesa kisha ukilipie
hicho kiasi husika ndipo utakuwa umejikatia tiketi ya kufanikiwa. Kama umewaza
hivyo pole sana ndugu msomaji maana gharama nayo maanisha sio pesa bali ni kitu
kingine ndugu mpendwa msomaji wangu.
Awali ya yote ningependa kufafanua kwa kusema tunaposema
gharama namaanisha kuwa hivi ni vitu ambavyo unatakiwa uvifanye kama kweli
unataka kufanikiwa au kuwa mwenye mafanikio. Chukulia mfano kama unataka
kusafiri kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine ni lazima ulipe nauli
hauwezi kusafiri pasipo nauli kwa hiyo kitendo cha wewe kulipa nauli na kuweza
kupata huduma ya kusafiri hii inamaanisha kuwa umekubali kulipia gharama za
safari yako.
Unapokuwa unataka kununua kitu fulani hulazimishwi wala
kushikiriwa bali unapotaka kununua kitu kwanza ni kile kitu ndicho
kinachokuvutia na kwa kuwa umevutiwa nacho basi unatakiwa ukubali gharama yake
ndipo uweze kukinunua kitu hicho. Kama haujakubali gharama yake maana yake huta
nunua na utakuwa umegoma kulipia gharama yake. Na kubwa zaidi ni kuwa kitu
hicho utakuwa umekikosa kwa muda huo mpaka pale utakapo kuwa tayari kulipia
gharama yake na kama huta taka hii inamaanisha kuwa maishani mwako hutakuwa na
hicho kitu.
Tukirudi katika safari ya kuelekea mafanikio hapa ni
rahisi sana gharama za safari ya mafanikio lazima uweze kuzilipia na hapo ndipo
utakapo yapata mafanikio. Kama ukishindwa kulipia gharama hizo hiyo inamaanisha
kuwa hauto weza kufanikiwa. Gharama za mafanikio ni kama vile uvumilivu, kuweka malengo,
kuwa na timu sahihi ya kushirikiana nayo, kuto kukata tamaa, kuwa jasiri, kuwa
na hamasa ya kupambanan.k. hizi zote ni gharama ambazo inabidi uzilipe
na hapo ndipo mafanikio utakapoyaona. Kama ukishindwa kufanya mambo hayo
hutoweza kufanikiwa na mafanikio utakuwa unayasikia kwa wenzio.
Wengi wetu sana tumekuwa tukitaka kufanikiwa lakini
hatupo tayari kulipia gharama mfano hatutaki kuwa wavumilivu, yaani mtu anataka
leo aanzishe mradi kesho uwe umemlipa amekuwa na pesa nyingi na kuwa maarufu au
awe ameshatambulika kama mtu tajiri miongoni mwa watu matajiri kumbe hilo ni
jambo ambalo haliwezi kutokea kwa muda mchache kama unavyodhani. Wengi wetu
tumekuwa hatupo tayari kulipa gharama hii ya uaminifu ndio maana tunaamini kuwa
maishani kuna njia ya mkato jambo ambalo ni hakuna kabisa.
Mara ngapi umekuwa ukitaka kufanikiwa lakini unajikatisha
tamaa mwenyewe kuwa dah kitu fulani mimi siwezi sio fani yangu?, ukijisemea
hivyo hii inamaanisha kuwa haupo tayari kulipia gharama ya kuto kata tamaa maishani.
Mara ngapi umekuwa ukishindwa kujiwekea malengo ili hali unajua kuwa lazima
ujiwekee malengo kama kweli unataka kufanikiwa maishani?, lipia gharama ya
kujiwekea mafanikio kama kweli unataka kufanikiwa.
Kimsingi mpaka hapo utakuwa umeshanielewa kuwa gharama za
mafanikio hazihusu kulipia pesa kama gharama za safari bali gharama zake ni
kufuata kile kitu ambacho ukikifanya hakika utafanikiwa tu. Hicho ndicho nacho
maanisha naposema lipia gharama kama kweli unataka kufanikiwa.
Ni mimi rafiki
yako Baraka Maganga,. Wasiliana nami
kwa nambari za simu 0754612413/0652612410. Au kwa barua pepe ambayo ni
Bmaganga22@gmail.com
No comments:
Post a Comment