Habari za wakati huu ndugu msomaji wa
mtandao huu wa kona ya maarifa ni matumani yangu kuwa hu mzima na unaendelea
vizuri katika kupambana
ili kuhakikisha kuwa unapata kile unachokitafuta katika maisha. Kwa kuwa lengo la mtandao huu ni kuhakikisha kuwa unapata vitu vya kukusukuma mbele zaidi katika kuelekea safari yako hiyo ya mafanikio, basi nasema pambana endelea kupambana bila kuchoka hata pale unapohisi umechoka jilazimishe maana kuridhika baaada ya hatua chache huleta anguko.
ili kuhakikisha kuwa unapata kile unachokitafuta katika maisha. Kwa kuwa lengo la mtandao huu ni kuhakikisha kuwa unapata vitu vya kukusukuma mbele zaidi katika kuelekea safari yako hiyo ya mafanikio, basi nasema pambana endelea kupambana bila kuchoka hata pale unapohisi umechoka jilazimishe maana kuridhika baaada ya hatua chache huleta anguko.
Mara nyingi sana watu wamekuwa na
utamaduni wa kuwapinga watu kwa kutumia vigezo kadha wa kadha na watu hawa ndio
wale wajulikanao kama wakatisha tama. Sasa wanaweza kutumia vigezo vingi lakini
hapa mimi leo nakupatia kigezo kimoja ambacho ni kabila. Yaani wapo watu watakao kupinga kwa kutumia kabila lao.
wapo watakao
kupinga kwa kigezo cha kabila. Yaani watu hawa huwa wanatumia kabila lako kama
dhana au kigezo cha kukukwamisha katika safari yako ya kuelekea mafanikio. Kila
kabila kwa hapa kwetu limekuwa likipewa sifa zake, ambazo hutumika kama
kitambulisho cha kabila hilo wakati mwingine. Ndio maana tunamakabila ambayo
yanafahamika kama makabila ya wafugaji, wafanyabiashara, wakulima n.k. Kuna wakati sifa hizi huwa na ukweli ndani
yake na kuna wakati huwa zinakuwa hazina ukweli ndani yake. Lakini kwa mtazamo
wangu mimi ni kuwa sifa hizi zitakuwa ukweli pindi utakapo ziamini na
kuzikubali kuwa ni za kweli. Itafika wakati utapingwa kwa kigezo hiki cha
kabila lako, mfano kwa hapa kwetu Tanzania inaaminika kuwa wafanyabiashara
maarufu ni wachanga na waha kutoka kigoma. Kwa kiasi kikubwa hapa kwetu makabila
haya ni maarufu sana kwa shughuli hizi ikiwa ni pamoja na ndugu zangu wakinga.
Hivyo
kutokana na mtazamo na imani juu ya makabila haya sio ajabu kuwa leo hii wewe
ukitaka kuanzisha biashara anaweza kutokea mtu akakupinga vikali kwa kigezo
kuwa kwa jinsi ulivyo wewe na kabila lako hilo huwezi kuwa mfanyabiashara maana
wewe sio mkinga, mchaga, au mha.
Utapingwa
kutokana na kabila lako kwa kuwa hizo ni imani ambazo watu wamejiwekea juu ya
makabila mbalimbali lakini jiulize swali je hapa Tanzania mfano kama biashara
wanaweza wachaga, waha, na wakinga pekee?, je makabila mengine ni kweli
hawafanyi biashara?,tafuta, chunguza na mwishoni uone kama utapata kubaini kama
hapa Tanzania hakuna wafanyabiashara wakubwa na maarufu ambao wanatoka katika
kabila lako. Kama hakuna basi anza wewe ili uvunje mwiko, na kama wapo basi nawe
unaweza kuwa miongoni mwao.
Ni
kweli kila kabila huwa na shughuli yake ya kiasili ambayo muda mwingine huwa
kitambulisho kwao. Mfano leo hii wamasai na wasukuma hutambulika kama jamii za
wafugaji lakini sio sababu ya wewe kupingwa kwamba huwezi kuwa mfugaji kisa
wewe sio mmasai wala msukuma. Pia ikumbukwe kuwa dunia inabadilika leo hii sio
wamasai wote wanafuga jamii hii, leo hii wamekuwa walinzi na wasusi maarufu
sana mjini sasa sijui tuwapinge maana wao asili yao ni kuchunga ng`ombe?.
Kumbuka
kuwa kadili ujionavyo nafsini mwako ndivyo unavyokua kumbuka hilo siku zote.
Hivyo basi kama unajiona huwezi kufanikiwa kutokana na kabila lako na itakuwa
hivyo. TWENDE SOTE
Ni mimi rafiki yako Baraka Maganga,. Wasiliana nami kwa nambari za simu
0754612413/0652612410. Au kwa barua pepe ambayo ni Bmaganga22@gmail.com
No comments:
Post a Comment