Thursday, January 28, 2016

Fahamu Leo Kuwa Maneno Yana Nguvu Sana Katika Maisha Yako.

Habari za wakati huu ndugu msomaji wa mtandao huu wa kona ya maarifa ni matumani yangu kuwa hu mzima na unaendelea vizuri katika kupambana ili kuhakikisha kuwa unapata kile unachokitafuta katika maisha. Kwa kuwa lengo la mtandao huu ni kuhakikisha kuwa unapata vitu vya kukusukuma mbele zaidi katika kuelekea safari yako hiyo ya mafanikio, basi nasema pambana endelea kupambana bila kuchoka hata pale unapohisi umechoka jilazimishe maana kuridhika baaada ya hatua chache huleta anguko.

Najua umekuwa ukupambana sana katika kuhakikisha kuwa unafanikisha mambo yako lakini kuna wakati ukikaa na kupiga tathimini unajikuta ukitamani kukata tamaa hii ni baada ya kuona au kupata matokeo ya tathimini yako  na hapo ndipo wengi huwa tunapatwa na hofu ya kuacha na mara nyingi sana huwa tunaanza kuona ni kama hatupigi hatua hivyo basi tunatamani kuachana na harakati zetu ambazo tumekuwa tukizianzisha na kuamini kuwa zitakuwa na msaada kwetu. Unatamani kuacha nakuona unasoma hii makala na huku unasema dah yaani sioni matokeo yoyote, niliambiwa hivi na vile, nilisoma hivi na vile lakini sioni matokeo yake, naacha bwana.








Kabla hujafikiria kufanya kitu hicho unachotaka kufanya nataka ujichunguze sehemu hii moja, yachunguze maneno yako. Kabla hujafikiria kufanya uamuzi wa kuacha kufanya jambo fulani kwa kuwa tu hujapata matokeo mazuri yachunguze maneno yako,  narudia tena yachunguze maneno yako. Unajua binadamu tuna namna mbili za kuongea, nakuona unashangaa kusikia namna mbili za kuongea, namaanisha kuwa tunakule kuongea kwa kawaida ambapo tunaongea na wenzetu huku kumezoeleka na ni maarufu lakini aina ya pili ni ile ya kujiongelesha wenyewe, yaani  kuna muda huwa unajikuta uwapo mwenyewe kuna maneno unayojiongelea mwenyewe sasa maneno haya ndio nayo taka uyachunguze.
Jiulize mwenyewe hapo ulipo je kauli unazojisemesha mwenyewe ni hasi au chanya, nakuona unasita kutoa jibu kwa kuwa unajua ni hasi. Wengi tumekuwa hatujui nguvu iliyopo katika maneno yetu ambayo tumekuwa tukijisemesha mara kwa mara na ndio maana tumekuwa tukihangaika kuchunguza mchawi wa maisha yetu kumbe sisi wenyewe ndio tunao jiloga. Unajiloga kwa maneno yako mwenyewe alafu unajikuta unalalama eti nalogwa na ndugu zangu hawataki nifanikiwe kabisa. Dah wewe, nani asiyetaka ufanikiwe wewe au wao?, jibu unalo mwenyewe mpaka hapo.

Pengine unajiuliza sasa mbona mimi sielewi ni kauli gani sasa, sawa mimi nipo kukuletea hizo kauli, mara ngapi umekuwa ukijisemea kuwa wewe unamikosi, nuksi au gundu. Ndio umekuwa ukijiambia ukisema unamikosi, gundu au nuksi maana yake huwezi kufanikiwa sasa kwanini unataka kufanikiwa ikiwa kila siku unajisemesha mwenyewe kuwa hauwezi kufanikiwa. Huoni kuwa unafanya kazi ya kuchanganya maji machafu kwenye maji masafi alafu unategemea maji masafi yaendelee kuwa masafi. Eti unataka kuacha kufanya mambo ya kukusogeza mbele kisa unamikosi, na ukiamini na kujisemesha kuwa unamikosi kweli utakuwa nayo tena mingi haswa. Acha kujisemesha na kujitazama kama mtu mwenye mikosi, gundu, na nuksi. Acha mara tu baada ya kusoma makala hii.

Mara ngapi umekuwa ukisalimiwa asubuhi unaambiwa habari ya asubuhi ndugu unajibu aa bora kumekucha, au dah bora ya jana, hivi unajua maana ya hayo maneno unayoyasema. Unayasema maneno hayo alafu akilini mwako unawaza kuwa biashara yako itakwenda sawa. Nani kakudanganya wewe acha kujidanganya, ukisema bora kumekucha maana yake haukutaka kukuche sasa unaendeleaje na shughuli kama hautamani kukuche?, ukisema dah bora ya jana maana yake siku ya leo ni ya ovyo sasa unategemea vipi kudharisha katika siku mbovu?, anza siku yako na kauli nzuri na mafanikio utayaona
.
Nakuona kila ikifika ijumaa unajifanya mzungu eti “thanks God it is Friday” ukimaanisha asante mungu kwa kuwa leo ni ijumaa. Unajua tafsiri yake hapo tafsiri yake ni kuwa siku zote zilikuwa mbaya kwako ndio maana unafurahia kuiona ijumaa. Sasa kwanini utake kufanikiwa jumatatu wakati kwako ni mbaya? Au alhamisi wakati ilikuwa mbayas?
Kuwa makini na kauli unazojinenea mwenyewe maana mnamo maneno mna nguvu sana, maneno huumba hilo waswahili waliliona na sio kuumba tu, maneno yanaamua maisha yetu ya sasa na baadae.hivyo basi kuwa makini sana tena sana juu ya maneno yako kama kweli unataka kufanikiwa. TWENDE SOTE.


Ni mimi Baraka Maganga, rafiki na mwalimu wako.  Wasiliana nami kwa nambari za simu 0754612413/0652612410. Au kwa barua pepe ambayo ni Bmaganga22@gmail.com.  

No comments:

Post a Comment