Habari za wakati huu ndugu msomaji wa
makala za mtandao huu, ni matumaini yangu kuwa hu mzima na unaendelea vyema
katika kubambana ili kuhakikisha kuwa unajiboresha zaidi na zaidi na baadae
unaweza kukamilisha yale ambayo umekwisha kujiwekea kama malengo katika maisha
yako. Nami nikusihi kuwa endelea kupambana pasipo kuchoka kwani harakati na
mapambano yanaendelea kila siku.
Wakati unaendelea kupambana leo kuna
jambo ambalo nataka kukushirikisha hapa, mambo yenyewe ni juu ya ile kauli
ambayo tumekuwa wengi wetu tukiitumia ama kwa kupenda kuiga au hata kwa kutumia
tu kwa sababu tumejizowesha kufanya hivyo. Kauli hii ni ya kusema sina muda. Hebu
hapo hapo ulipo jiulize ni mara ngapi umekuwa ukijiambia kuwa sina muda pindi
unaposhirikishwa jambo fulani iwe biashara, iwe semina, iwe kusoma kitabu n.k
Sasa kama unakumbwa na kauli hii basi
leo nipo hapa ili kukupa sababu na namna ya kufanya ili uweze kuondokana na
kauli hii maana imekuwa ikituferisha wengi wetu siku hadi siku.
1. Kukosa ratiba,ratiba ni mpangilio wako wa
namna utakavyoianza siku na kuimaliza siku yako. Kila mtu huianza ratiba yake kwa namna yake
ya kipekee na kila mtu huianza ratiba yake pindi tu anapoamka kutoka kitandani.
Ratiba huwa ni mpangilio wa mambo na shughuli ambazo utazitenda kuanzia unaanza
siku mpaka unaimaliza, na hii huwa inakwenda sambamba na malengo yako. Sasa
swali la kujiuliza ni kuwa wewe unaratiba?, kumbuka waswahili husema “mazoea
hujenga tabia” nami nakuambia ratiba hujenga mazoea na ni kitu muhimu sana
kwako wewe mwanamafanikio. Mfano nikuulize una muda maalumu wa kulala au huwa
unalala tu pale unapohisi kulala. Ni muhimu ukajiwekea ratiba, hii itakusaidia
wewe kupata muda wa ziada ambao huo unaweza kuutumia katika shughuli au mambo
mengine unayoshirikishwa na unasema hauna muda. Anza na ratiba rahisi sana leo
jiwekee muda maalumu wa kulala na muda maalumu wa kuamka alafu ndio zifuate
ratiba zingine. Fanya hivyo kwa muda wa wiki mbili kwa nidhamu ya hali ya juu
ndipo uanze kuongeza ratiba zingine.
2. Umeshindwa kutenga muda wa uzalishaji na
muda wa kupumzika, muda mwingine kutokana na kukosa ratiba
tumekuwa tukijikuta kuwa tunashindwa kutenga muda wa kuzalisha na muda wa
kupumzika. Hii ni hatari maana binadamu hutakiwa kupumzika maana yeye sio
mtambo ambao umesetiwa ili kufanya kazi kila muda, kila dakika, kila sekunde
hapana. Leo hii anza kwa kutenga muda wa kazi na muda wa kupumzika na katika
muda wa kupumziki ndipo unaweza kuweka mambo mengine au shughuli ambayo ni
rahisi ambayo haihitaji nguvu nyingi wala kutumia akili nyingi mfano mazoezi ya
mwili. Kumbuka muda wa kupumzika uwe mchache kuliko muda wa kufanya kazi.
3. Haujafanya maamuzi,
wakati mwingine shida sio kuwa hauna muda ila shida ni kuwa haujafanya maamuzi
ya kufanya kile unachoambiwa kufanya. Na kwa kuwa haujafanya maamuzi juu ya
lile yaani wewe ulishaipanga akili yako kuwa kwa kila jipya ntakalo ambiwa mimi
jibu langu liwe sina muda. Hii ni kukosa maamuzi na pia vile vile kukosa
maamuzi hutokana na sababu kuwa hauna maamuzi yako binafsi bali unaishi kwa
kufuata maamuzi ya wenzio tu jambo hili ni hatari sana. Sasa leo hii fanya
maamuzi mapya ya kutafuta muda kwa kila unaloshirikishwa leo hii utenge muda wa
kulifanya.
Ni jambo la ajabu leo hii kusema kuwa hauna muda wa
kufanya jambo fulani tena lenye tija katika maisha yako mfano kwenda kwenye
semina, kwenye mazoezi, kwenye makongamano ya kidini, kwenye mikutano ya
kijasiriamali, au hata kusoma kitabu. Lakini una muda wa kuangalia TV kuanzai asubuhi
hadi jioni. Au una muda wa kuingia na facebook na instgram kulike picha za
wenzio tu.
Mwandishi:
Baraka Maganga.
Mawasiliano:-simu-0754612413/0652612410.
:-barua pepe
-Bmaganga22@gmail.com
No comments:
Post a Comment