Habari za wakati huu ndugu mpenzi msomaji wa makala za mtandao
huu, ni matumaini yangu kuwa hu mzima na unaendelea vyema katika kuhakikisha
kuwa unapambana ilivyo ili kuweza kujiletea mafanikio, nami nasema mapambano
yanaendelea kamwe usikate tamaa hata siku moja. Maana mpambanaji huwa hakubali
kukata tamaa kirahisi.
Wakati unaendelea kupambana ili kuhakikisha kuwa
unajiletea mafanikio ni vyema ukatambua jambo hili,kwa kuwaa ninaaini kuwa wewe
hiki kitu unakifanya ndio maana nikakuuliza je? Mtu huyu unamfahamu vizuri? Najua
kila mtu anasehemu au ana mtu ambaye huwa anakuwa anamwomba ushauri sasa
kutokana na kitendo hiki ndio maana kichwa cha makala hii kinauliza mtu huyu
unamfahamu vizuri?
Najua unamshauri wako, tena huyu ni mtu unaemwamini na
kumtegemea kwa kiasi kikubwa sana tena sana, kwanini nimekuuuliza basi kuwa mtu
huyu unamfahamu vizuri? Hapa nimekuuuliza kwa sababu ndani ya washauri wetu
kuna mambo makuu mawili au kuna washhauri wa aina mbili, yaani kuna mtu anaetoa
ushauri kwa kutumia uzoefu na kuna mtu anaetoa ushauri kama sehemu ya taaluma
yake. Lakini ukiachilia mbali hizi tofauti wote wanafanya kazi moja mabayo ni
ushauri. Sasa jambo nalo kuuliza unamfahamu mshauri wako, yaani unaufahamu kama
yeye anatoa ushauri kutokana na uzoefu au anafanya kama taaluma?.
Mshauri anaefanya ushauri kwa kutumia uzoefu sio kuwa ni
mbaya hapana lakini amekosa kitu kimoja ambacho ni taaluma, pia tatizo moja la
mshauri wa namna hii ni kuwa anaendeshwa na matukio yaliyokwisha kutokea nyuma
hivyo basi endapo litatokea jambo jipya au changamoto ambayo ni nje na uzoefu
wake inakuwa ni ngumu sana kwake yeye kuweza kutatua changamoto husika. Pia mshauri
huyu huwa anakuwa akitawaliwa na hisia zake zaidi kuliko za wengine hivyo basi
hata kama wewe ukiwa na wazo zuri ila ni kinyume na uzoefu wake pamoja na hisia zake basi hutoweza kupata ushauri
sahihi.
Pia mshauri mwenye taaluma huyu sio kuwa nae ni mbaya ila
tatizo linakuja kuwa mshauri wa namna hii ni kuwa anakosa kitu kimoja ambacho
ni uzoefu. Lazima utambue kuwa maishani uzoefu una nafasi yake katika utatuzi
wa changamoto maana uzoefu huwa unatusaidia kupata hisitoria ya tatizo husika. Hivyo
basi uzoefu ni muhimu lakini mshauri mwenye taaluma anaweza kujikuta akiwa
katika wakati mgumu pindi linapokuja swala la uzoefu. Lakini uzuri wa mshauri
huyu ni kuwa hatawaliwi na hisia bali anafanya kazi yake kutokana na taaluma
yake inavyomwongoza.
Hivyo basi nini ufanye sasa, jambo la kufanya hapa ni kuwa
hakikisha kuwa unamfahamu vyema mshauri wako kwa kuwa huyu ni mtu ambaye
anakuwa na nafasi kubwa sana katika maisha yako, najua ni ngumu kumpata mtu
mwenye taaluma na uzoefu hilo lisikupe shida wewe lakini hakikisha kuwa
unamfahamu mtu huyu anaekushauri, yaani uwe na uwezo wa kutambua kuwa mshauri
huyu je anaongozwa na hisia zake katika kunishauri au anatumia taaluma na je
anayonishauri yanaendana. Maana kuna mtu ukimwomba ushauri juu ya jambo fulani
ambalo yeye aliwahi kufanya akashindwa tambua kuwa hapo hutoweza kupata ushauri
mzuri bali utakuwa ni ushauri wa kukatisha tamaa tena kwa kiwango kikubwa sana,
maana siku zote aliyeshindwa hawezi kukupa wewe ushauri wa kukutia moyo kuwa
utafanikiwa ili hali yeye alishindwa. Hivyo
basi hakikisha kuwa unamfahamu vyema mshauri wako.
]
Mwandishi:
Baraka Maganga.
Mawasiliano:-simu-0754612413/0652612410.
:-barua
pepe -Bmaganga22@gmail.com.
KARIBU KATIKA DARASA HURU.
Je?
unataka kujifunza na kuwa bora zaidi?,Je? unataka usihangamie kwa kukosa
maarifa?,Je? unataka kujua namna ya kutatua matatizo na changamoto mbalimbali
zinazokukabili?,Je? unakumbana na hali ya kukata tama mara kwa mara?,Je?
unashindwa kujiwekea malengo n.k.Kama jibu ndio basi karibu katika darasa huru. Namna ya kujiunga na
darasa huru tuma kiasi cha pesa cha shilingi 5000/= kwa namba 0754612413
kwa mpesa (jina. Baraka magama) au 0652612410 kwa tigo pesa. (jina: Baraka
maganga). Kisha, tuma namba yako ya simu kwenda namba moja kati ya hizo
huku ukiwa umeambatanisha na jina lako kamili kama linavyojitokeza katika
m-pesa au tigo pesa. Kumbuka kufanya hivyo huku ukiwa na uhakika kuwa pesa yako
imepokelewa na hapo utaunganishwa kwenye kundi la whatsapp ambalo litakuwa na
jina la DARASA HURU.
N.B, huduma hii itatolewa kwa njia ya whatsapp, hivyo
hakikisha simu yako ina uwezo wa whatsapp ndipo ujiunge ili kuepuka usumbufu.
Barikiwa.
No comments:
Post a Comment