Wednesday, April 6, 2016

Njia Hizi Zitakusaidia Kupambana Pindi Unapokabiliwa Na Changamoto.


Maisha yamejaa changamoto za namna mbalimbali, wakati unapambana ili kujihakikishia kuwa unapata mafanikio au matokeo mazuri juu ya mambo fulani swala la changamoto huwa linakuwa ni jambo ambalo halihepukiki wakati mwingine. Ni muhimu tupitie katika changamoto kwani changamoto hizi huwa zinatujenga na kutufanya tuwe imara zaidi na zaidi maishani,
Ni muhimu kusimama imara pindi tunapokuwa tunakabiliwa na changamoto hizo. Hii ni kutokana na sababu kuwa uwezo wa kupambana na changamoto hizi huwa upo mikononi mwetu. Ni muhimu kutambua kuwa kwa kila changamoto inayokukabili ni muhimu uanze kujihoji kwanza na kujiuliza wewe mwenyewe ufanye nini juu ya changamoto husika. Kwa kufanya hivyo utajikuta unapata majibu ambayo yanakuwa msaada mkubwa sana kwako. Pamoja na hayo zifuatazo ni baadhi ya njia ambazo zaweza kukusaidia wewe katika utatuzi wa changamoto inayokukabili:-






Kuwa mkweli, hapa nazungumzia ukweli baina ya pande mbili. Ukweli wa nafsi yako na ukweli kwa wengine. Unapokabiliwa na changamoto na unapotaka kuitatua changamoto husika basi hakikisha kuwa hu mkweli wa nafsi yako na kwa wengine. Ukweli wa nafsi yako ni muhimu pale ambapo utakuwa unajihoji mwenyewe ili kutaka kujua nini haswa chanzo cha changamoto ile, na ufanye nini wewe kama wewe ili kuitatua changamoto hiyo. Ukweli wa nafsi yako mwenyewe ni muhimu kwa kuwa huu utakuondolea ile hali ya kutaka kuwasingizia watu wengine kuwa wao ndio chanzo cha changamoto husika wakati sio kweli, pengine wewe mwenyewe ndio chanzo cha changamoto husika.
Ukweli kwa watu wengine huu utakuwa na msada pale ambapo unataka kumshirikisha mtu fulani ili aweze kukupa msaada wa mawazo juu ya nini ufanye kuhusiana na changamoto hiyo. Ni muhimu kuwa mkweli pale unapotaka kupata msada wa mawazo kutoka kwa wengine, hii itawasaidia wao kuelewa changamoto inayokukabili kinagaubaga na hatimaye wakaweza kutoa mchango wao kwa usahihi kwa kuwa umeiweka wazi changamoto na wameielewa kuliko ungeficha ficha mambo.

2.    Omba ushauri kwa mtu sahihi, hapa nachomaanisha ni kuwa unapokabiliwa na changamoto ni muhimu ukaelewa kuwa sio kila mtu anaweza kukupa ushauri wa ni nini haswa unapaswa kufanya ili kuweza kukabiliana na changamoto husika. Ndio maana ninakuambia omba ushauri kwa mtu sahihi.  Mfano unakabiliwa na changamoto katika kilimo cha nyanya ni muhimu ukaomba ushauri kwa mkulima au mtaalamu wa kilimo hicho cha nyanya na sio unachangamoto katika kilimo cha nyanya wewe unaenda kuomba ushauri kwa mkulima yoyote yule au mtaalamu yoyote yule wa maswala ya kilimo. Ni muhimu utambuwe kuwa kuna kitu kinaitwa ubinafsi katika maisha, yaani kutokana na upana wa jambo fulani kila mtu leo hii anafanya ubinafsi  katika taaluma fulani ndio maana leo hii unaweza kukuta kuna daktari wa macho pekee mengine hajui hii ni kutokana na ubinafsi alioamua kuufanya katika taaluma husika, hivyo ni muhimu ukaelewa mtu unaemfata kutaka ushauri yuko katika jambo hilo kiusahihi.

Nimekupatia njia mbili rahisi sana za kuzifuata pindi unapokabiliwa na changamoto, nina imani kuwa njia hizi hazina ugumu wowote katika kuzitekeleza ndio maana nikasema ni rahisi. pia nina imani kuwa ukizifuata njia hizi utapata matokeo mazuri na utaweza kuitatua aina yoyote ile ya changamoto inayokukabili. Kumbuka changamoto ni kitu ambacho mwanadamu hawezi kukiepuka ila anao uwezo wa kukabiliana nazo.

 Mwandishi: Baraka Maganga.
Mawasiliano:-simu-0754612413/0652612410.

KARIBU KATIKA DARASA HURU.
Je? unataka kujifunza na kuwa bora zaidi?,Je? unataka usihangamie kwa kukosa maarifa?,Je? unataka kujua namna ya kutatua matatizo na changamoto mbalimbali zinazokukabili?,Je? unakumbana na hali ya kukata tama mara kwa mara?,Je? unashindwa kujiwekea malengo n.k.Kama jibu ndio basi karibu katika darasa huru. Namna ya kujiunga na darasa huru tuma kiasi cha pesa cha shilingi 5000/= kwa namba 0754612413 kwa mpesa (jina. Baraka magama) au 0652612410 kwa tigo pesa. (jina: Baraka maganga). Kisha, tuma namba yako ya simu kwenda namba moja kati ya hizo huku ukiwa umeambatanisha na jina lako kamili kama linavyojitokeza katika m-pesa au tigo pesa. Kumbuka kufanya hivyo huku ukiwa na uhakika kuwa pesa yako imepokelewa na hapo utaunganishwa kwenye kundi la whatsapp ambalo litakuwa na jina la DARASA HURU.
N.B, huduma hii itatolewa kwa njia ya whatsapp, hivyo hakikisha simu yako ina uwezo wa whatsapp ndipo ujiunge ili kuepuka usumbufu.
Barikiwa.
Karibu sana.


No comments:

Post a Comment