Leo hii tanzania kimeibuka kitu ambacho kimeibuliwa na
serikali ya awamu ya tano. Ambacho kinatufanya wengi wetu tuwe mashabiki sana
wa hiki kitu. Wengi wetu leo hii tumekuwa tukishabikia sana sera ya mheshimiwa
raisi ya kutumbua majibu, kweli wengi sana tunashangiulia lakini leo nataka
kukusisitiza na kukuonya kuwa usiishie kuwa shabiki tu wa hii sera ya kutumbua
majipu.
Sera hii ilianzishwa na mheshimiwa raisi kwa lengo moja
tu la kuwawajibisha wasiotaka kuwajibika wenyewe kwa ihali yao. Sasa kama wewe
unaishabikia sera hii ni muhimu utambue kuwa neno kutumbua jibu ni kwa wale wasiotaka
kuwajibika na sio vinginevyo na pindi unaposhabikia kuwa fulani kawajibishwa
anza kujiuliza kuwa wewe unawajibika kwa kiasi gani?. Dhana hii imekuja
kuonekana kuwa ni mwiba mkali sana kwa viongozi na watumishi wa serikali lakini
hapa mimi sipo kuongeana na viongozi naongea na wanamafanikio na wanaotaka
mafanikio.
Kwako wewe mwanamafanikio hutakiwi kushabikia tu dhana
hii pasipo kuelewa maana yake, mimi nishakupa maana yake kuwa mtu yoyote
asiyetaka kutekeleza wajibu wake ni jipu. Sasa kwa kuangalia hilo wewe unahisi
hapa tanzania tuna majipu mangapi?. Kwa watumishi na viongozi wa serikali akiwa
jipu anatumbuliwa maana yake anakosa kazi, je mambo yakoje kwako wewe unayetaka
mafanikio?, kwako wewe unayetaka mafanikio kama ukiwa jipu hii inamaanisha kuwa
hauwezi kuyapata mafanikio kamwe na kwako wewe ulie na mafanikio alafu ni jibu
hapa litakalo tokea ni kuwa utapata anguko kubwa sana.
Nimesema usiishie kuwa shabiki tu wa hili neno la
kutumbua majipu, maana wakati mwingine kuwa shabiki tu kunakufanya ushindwe
kufikiri nje ya boksi. Leo hii kila mtu anafurahi akisikia kiongozi fulani
katumbuliwa jipu lakini turudi kwako wewe baba wa familia ambaye ukiamka tu ni
wewe na mambo yako tu hujui familia itakula nini, watoto wameenda shule au la,
hujui hata kama familia ni wazima au la ila swala ni kuwa wewe ukiamka tu
unakurupuka na kwenda kijiweni kucheza bao na kupiga stori nyingi kweli wakati
hutaki kuwajibika kwa lolote lile linalohusu familia, nataka nikuulize kwa
maana niliyoitoa kuhusu jipu, je hapo wewe sio jipu?.
Wewe mfanyakazi kwanini hutaki kufanya kazi ipasavyo
unafanya kazi ilimradi umefanya nataka nikuulize hiyo kazi uliombewa au uliomba
mwenyewe, hivi kuna aja gani na kufanya kazi ambayo huipendi, nakusikia unasema
aa bhana kazi tunafanya hivyo hivyo tu. Ukiwa unasema hivyo kuwa unafanya kazi
hivyo hivyo tu ndio maana unajikuta ukitumbuliwa jipu maana kitendo cha kusema
kazi unafanya hivyo hivyo hii inamaanisha kuwa huwajibiki ipasavyo, sasa nataka
nikuulize uliajiliwa ili ukafanye kazi au ili ukafanye kazi hivyo hivyo?
Nakuona mkulima unafurahi maana hakuna wa kukutumbua
jibu, ni vizuri lakini nataka nikuambie ukiona kila siku kipata chako cha mazao
ni kile kile miaka nenda miaka rudi jua na wewe mkulima ni jipu, tena jipu
kubwa tu sema hakuna wa kukutumbua tu ndio maana unafurahi furahi tu. Nataka nikusisitize
sana ndugu mkulima kuwa jibidiishe katika kilimo, tafuta mbinu mpya za kilimo,
tafuta taarifa mpya za kilimo ili usiwe mkulima jipu hata kama hakuna wa
kujitumbua.
Katika mafanikio tunasema jipu zuri ni lile la kujitumbua
mwenyewe, yaani njia bora ya kuwajibika ni kujiwajibisha mwenyewe usisuubiri
kujakuwajibishwa kama watumishi wa serikali.
Mwandishi:
Baraka Maganga.
Mawasiliano:-simu-0754612413/0652612410.
:-barua
pepe -Bmaganga22@gmail.com.
KARIBU KATIKA DARASA HURU.
Je?
unataka kujifunza na kuwa bora zaidi?,Je? unataka usihangamie kwa kukosa
maarifa?,Je? unataka kujua namna ya kutatua matatizo na changamoto mbalimbali
zinazokukabili?,Je? unakumbana na hali ya kukata tama mara kwa mara?,Je?
unashindwa kujiwekea malengo n.k.Kama jibu ndio basi karibu katika darasa huru. Namna ya kujiunga na
darasa huru tuma kiasi cha pesa cha shilingi 5000/= kwa namba 0754612413
kwa mpesa (jina. Baraka magama) au 0652612410 kwa tigo pesa. (jina: Baraka
maganga). Kisha, tuma namba yako ya simu kwenda namba moja kati ya hizo
huku ukiwa umeambatanisha na jina lako kamili kama linavyojitokeza katika
m-pesa au tigo pesa. Kumbuka kufanya hivyo huku ukiwa na uhakika kuwa pesa yako
imepokelewa na hapo utaunganishwa kwenye kundi la whatsapp ambalo litakuwa na
jina la DARASA HURU.
N.B, huduma hii itatolewa kwa njia ya whatsapp, hivyo
hakikisha simu yako ina uwezo wa whatsapp ndipo ujiunge ili kuepuka usumbufu.
Barikiwa.
No comments:
Post a Comment