Najua unaweza kuwa umeshangazwa
kidogo na kichwa cha makala yetu ya leo, lakini usiogope wala kushangaa sana na
kuaanza tayari kusema haiwezekani bwana mimi sio dereva. Punguza presha ndugun
msomaji na uwe mpole maana taratibu utanielewa. Nasema wewe ni dereva ndio wewe
unaesoma makala hii kwa sasa wewe ni dereva, acha kubisha uliza dereva wa
nini?.
Kabla sijakujibu nataka nitoe maana ya dereva kwa uelewa wangu, dereva ni mwongozaji wa chombo Fulani inaweza kuwa gari, meli, ndege lakini mwongozaji huyu ambae anajulikana kama dereva huwa ni Yule anaeongoza magari tu hivyo ndivyo ilivyozoeleka lakini ukweli ni kuwa dereva ni mwongozaji wa chombo cha moto. Kazi kubwa ya mwongozaji huyu ni kukifanya chombo kisiende mlama na hatimae kikaleta madhara. Mfano dereva wa gari huwa na kazi ya kuliongoza gari ili kama kabeba abiria wafike salama na kama kabeba mizigo pia ifike salama. Nadhani umenielewa.
Kabla sijakujibu nataka nitoe maana ya dereva kwa uelewa wangu, dereva ni mwongozaji wa chombo Fulani inaweza kuwa gari, meli, ndege lakini mwongozaji huyu ambae anajulikana kama dereva huwa ni Yule anaeongoza magari tu hivyo ndivyo ilivyozoeleka lakini ukweli ni kuwa dereva ni mwongozaji wa chombo cha moto. Kazi kubwa ya mwongozaji huyu ni kukifanya chombo kisiende mlama na hatimae kikaleta madhara. Mfano dereva wa gari huwa na kazi ya kuliongoza gari ili kama kabeba abiria wafike salama na kama kabeba mizigo pia ifike salama. Nadhani umenielewa.
Nataka nikujibu sasa swali lako
kuwa kwanini nimekuita dereva na ni
dereva wa nini. Wewe ni dereva mzuri na ni dereva mzuri wa maisha yako. Hapo
naona tumeanza kuelewana kwanini nasema wewe ni dereva mzuri wa maisha yako, ni
kwa kuwa hakuna anaekujua zaidi ya wewe unavyojijua. Achana na ile misemo kuwa
namfahamu Yule bwana au bibi fika, hiyo ni misemo ya watu ambao wakati mwingine
hawana maana yoyote wewe ndiye unaejifahamu, yaani unajijua uko vipi, ubora na
udhaifu wako unaujua wewe na sio kaka, dada, mama, baba, mke au mume. Nakuambia
leo sasa kuwa mke wako hawezi kukujua kuliko wewe unavyojijua, na wewe mke
mumeo hawezi kukujua kuliko unavyojijua wewe. Ndio maana nakuambia wewe ni
dereva mzuri sana wa maisha yako.
Sababu iliyonisukuma kuweza
kuandika makala hii ni kutokana na upotoshaji mkubwa sana uliopo miongoni mwa
watu haswa sisi vijana maana mimi ni mtu ambae nimekuwa nikiandika sana kuhusu
vijana, kuwa tumekuwa na tabia moja ya kuhisi kuwa kuna mtu tunamsubiri aje
atuongozee maisha yetu. Yaani sisi tunataka kuwa abiria wa maisha yetu. Yaani
tunataka kila kitu tufanyiwe, kila kitu tuletewe kama vile hatujiwezi sasa
jambo hili huwa ni hatari sana. Kumbuka dereva ni mwendeshaji wa chombo cha
moto hivyo kama ni gari tutasema ni dereva wa gari. Sasa nikisema wewe ni
dereva hata kama unaesoma hii makala ni dereva wa gari, bodaboda, na vingine
jua udereva wa kwanza ni wa kuendesha maisha yako. Watu wengi wamekuwa sio
madereva wa maisha yao na hapa utawakuta aidha wanaendesha maisha ya wenzao au
wanakuwa abiria wa maisha yao. Yani wanasubiri kuendeshwa.
Nachokutaka leo jenga misingi ya maisha yako,
yasimamie maisha yako mwenyewe maana hakuna mtu mwenye kuweza kuyasimamia
maisha yako wakati nae anayo ya kwake. Nataka uwe na utawala wa maisha yako na
sio maisha yako yatawaliwe na mtu fulani au watu fulani, kumbuka nishakuonya
toka mwanzao kuwa baba, mama, shangazi, mjomba sijui mume hawezi kuwa dereva wa
maisha yako. Chukua hatua mwanzoni mwa mwaka huu uanze kujipanga na kusimamia
na kuendesha maisha yako. Huo ndio udereva nao uzungumzia hapa. Usijidanganye
hata siku kutaka kuwa abiria wa maisha yako kwani kwa kufanya hivyo huwezi
kufanikiwa hata siku moja.
Kila kheri katika kuuanza
udereva wako.
Rafiki
Yako
Baraka
Maganga
0754612413
No comments:
Post a Comment