Habari ndugu msomaji wa mtandao huu. Ni matumaini
yangu kuwa unaendelea vizuri na harakati za hapa na pale huku ukiwa na hamasa
kubwa sana ya kuyapata mafanikio nami nasema vizuri na endelea kupambana.
Leo nataka
nikushirikishe jambo nalo ni kuhusu jinsi ya kuyatumia mafanikio ya wengine.
Kuna namna mbili ambazo binafsi nimeziona watu wakiyatumia mafanikio ya watu.
1. Mafanikio ya watu kama chanzo cha
mgogoro,
kuna watu wanatumia mafanikio ya watu kama chanzo cha mgogoro baina yao na ya
watu wenye mafanikio. Yaani hapa namaanisha kuwa kuna watu ambao hawapendi
mafanikio ya watu hawa ni watu ambao hawapendi kuona watu/ mtu Fulani
kafanikiwa hivyo basi watu hawa huanza kuwashutumu watu wenye mafanikio kwa
maneno na vitibwi kemukemu. Watu hawa huwa ni wenye kutawaliwa na wivu na roho
mbaya sana, hivyo huona kufanikiwa kwa wengine sio haki. watu hawa huwa ni wenye mtazamo hasi mara zote juu ya mafanikio ya wenzao na pengine huona ni kama watu wenye mafanikio husika hawasitahiri kuyapata mafanikio hayo.
2. Mafanikio ya watu kama somo, aina ya pili ya watu ni
wale ambao huchukulia mafanikio ya wenzao kama somo, hawa ni wenye kufurahia
mafanikio ya wenzao na kuwaona watu waliofanikiwa kama watu wenye kuwa darasa
kwao, msaada na kimbilio kwao. Aina hii ya watu ni wale ambao hudiriki kuwafata
watu wenye mafanikio na kutaka kujifunza kwao kuwa wamefanyafanya vipi au
wamepitapita vipi mpaka kuyafikia mafanikio. Hawa ni ambao hutaka kujifunza
zaidi kupitia waliofanikiwa na hutaka kuwa kama waliofanikiwa.
Nimekupatia
njia mbili za kujifunza kupitia watu walifanikiwa lakini nakushauri utumie njia
ya pili kwa kuwa ndio bora na yenye msaada kwako kama kweli unataka kufanikiwa.
Ni Mimi rafiki
yako
Baraka Maganga.
Bmaganga22@gmail.com.
0754612413/0652612410
No comments:
Post a Comment