Thursday, November 12, 2015

Hiki Sio Kipimo Halisi Cha Mafanikio Yako.


Habari za wakati huu ndugu msomaji wa mtandao huu. Ni matumaini yangu unaendelea vizuri katika harakati zako za kupambana katika kuyatimiza yale uliyokwisha kujiwekea kama malengo yako. Tumekutana tena katika kutaka kuelimishana na kujengana yote haya ni katika kuhakikisha kuwa safari yetu ya kuyaelekea mafanikio inakuwa bora zaidi na zaidi.

 Leo ndugu msomajia nataka kukushirikisha jambo moja ambalo binafsi naliona ni kama imani potofu ambayo inaendelea kupandikizwa miongoni mwetu. Imani hii in ile yenye kutufanya tuamini kuwa mafanikio yako mjini tu na hivyo basi kijijini hakuna mafanikio.

 Tumekuwa ni watu wenye kuamini kuwa watu wanaoishi mjini ndio wenye mafanikio tofauti na wale wanaoishi vijijini, sidhani kama jambo hili lina ukweli wowote japo kuwa kiukweli ni kwamba ukilinganisha mafanikio ya mjini na mafanikio ya kijijini ni dhahiri mjini.

 kunaonekana kuna mafanikio lakini hapa tunazungumzia mafanikio ya mtu mmoja mmoja. Ukiangalia leo hii utagundua kuna Lindi kubwa sana la watu (haswa vijana).ambao wanahama kijijini kuelekea mjini wakiamini kuwa mjini ndiko kwenye mafanikio tofauti na kijijini. Lakini wengi wao wakifika mjini hukuta mambo yamekuwa magumu sana kiasi kwamba hutamani kurudi tena kijijini.

 Kimsingi mafanikio yana husisha fursa jambo la msingi ni kutafuta fursa na kutumia fursa hizo, leo hii utamkuta mtu akikimbia kijijini huku akitelekeza mashamba mengi sana na kuamua kwenda mjini kutafuta kazi, mtu huyu ameamua kwenda mjini kwa kuwa ameaminishwa kuwa mjini ndiko kwenye mafanikio lakini mafanikio sio wingi wa watu, magorofa, magari n.k. mafanikio ni pale ambapo umeweza kuyatekeleza malengo yako binafsi na uwezo wa kutekeleza malengo hauna uhusiano na niwapi haswa ulipo. Yaaani hakuna sheria ya kwamba ukitekeleza mafanikio yako ili hali uko mjini ndipo watakuita mwenye mafanikio na kama ukitekeleza malengo yako ili hali ukiwa kijijini hautaitwa mwenye mafanikio.

 Jifunze kuchunguza fursa mahali ulipo na uzitumie usiwe mtu wa kukurupuka na kukimbilia sehemu zingine huku ukiamini sehemu hizo ndizo zenye mafanikio kuliko zingine pasipo kufanya tathimini yoyote ya msingi.

Ni Mimi rafiki yako
Baraka Maganga.
Bmaganga22@gmail.com.
0754612413/0652612410.


No comments:

Post a Comment