Tuesday, November 17, 2015

Unajiua Kila Siku Kwa Kufanya Jambo Hili Mara Kwa Mara.




Habari za siku ndugu msomaji WA mtandao huu wa kona ya maarifa, ni matumaini yangu kuwa unaendelea vizuri katika harakati zako za kujiletea mafanikio.
Leo nakushirikisha jambo hili ambalo wengi wetu tumekuwa tunalifanya ambapo Nina uhakika wengi wetu hatujui madhara yake ndio maana tumekuwa tukilifanya. Jambo lenyewe ni kutaka kumridhisha kila mtu.
Tabia ya kutaka kumridhisha kila mtu imeshamili sana miongoni mwetu ambapo watu wengi tumekuwa tukifanya mambo mbalimbali ambayo wakati mwingine tunakuwa hatuyataraji, wala kuyapenda lakini tunayafanya,  hii ni kwasababu tu tunataka kuwaridhisha watu. Tumejijengea fikira za kutaka kuwaridhisha wazazi, wadogo zetu, majirani na ndugu mbalimbali. Wakati tukifanya hivi tumejikuta tukisahau hata kufanya mambo yetu ya msingi kisa tu tunataka kuwaridhisha watu.
  Sio jambo la ajabu kumkuta mtu anaacha shughuli yake ya msingi na kwenda kumsaidia mwingine shughuli kisa tu aonekane mwema na mwenye fadhira kwa mtu huyu, huku akilini mwake akiamini kuwa amemuridhisha yule mtu kwa msaada wake, lakini wakati huo huo amesahau kuwa alikuwa na shughuli yake ya msingi ambayo aliiacha kisa tu amsaidie huyu mtu. Lakini nataka ujiuluze kama umeona kuacha shughuli zako na kuwasaidia wengine ndio njia ya kuwaridhisha hao watu, piga hesabu hapo unapoishi kuna watu wangapi?, na kwa kuwa unataka kumridhisha kila mtu na njia uliyochagua kuwaridhisha watu hawa ni kwa wewe kujihusisha na shughuli zao huku ukiacha shughuli zako piga hesabu kama unapoishi kuna watu mia tana (500), utakuwa na siku ngapi za kuwasaidia na nilini haswa utajihusisha na shughuli zako?.
Ki kawaida binadamu ni kiumbe aliye mgumu kuridhika yaani ni ngumu sana kumridhisha binadamu kwa kuwa binadamu amejaa lawama na kama binadamu wengi wa sasa wamejaa lawama basi hutoweza kuwaridhisha wote. Maana hata kwa ile njia ambayo umeichagua kuwa utawaridhisha kwa kuwasaidia shughuli zao wapo ambao hawataridhika maana wanaweza kutumia kigezo cha muda na uzito wa shughuli ambapo watakuhukumu kuwa kunabaadhi ya watu ulitumia muda mwingi kuwasaidia tofauti na wengine hivyo basi hawajaridhika sasa jiulize utafanyaje kuwaridhisha watu hao?. Pengine utataka kurudia kwa wale unaona hawajaridhika utakapo rudia utakuwa ndio umejiloga maana ukirudia kuwasaidia na wengine tena watasema nao pia hawakuridhika. Hapo ndipo utakapo gundua kuwa binadamu ni kiumbe asiye ridhika kiurahisi.
Jiulize mwenyewe ni Mara ngapi wewe uliyeajiriwa umekuwa ukiamua kufanya maamuzi magumu ya kugawana mshahara wako na wazazi,marafiki au wadogo zako. Hivyo basi kila unapopata mshahara unawagawia kiasi cha pesa huku ukiamini kuwa kwa kufanya hivyo umewaridhisha na kuwafurahisha lakini nakuambia ukweli kwa binadamu wa sasa ambao ni wajaa lawama watakulaumu tu, na watadiriki hata kusema kuwa hauwasaidii. Ili hali wewe unawasaidia. Hivyo basi kama unatoa msaada toa kwa sababu umeamua kusaidia na sio kwa lengo la kuwaridhisha watu.

Tambua jambo moja haukuja duniani kumridhisha mtu wala kupendwa na kila mtu hivyo basi jambo la msingi kwako ni kuwa tenda haki siku zote usiwe mtu wa kuyumba yumba bali tenda haki siku zote. Pia weka malengo yako na hakikisha unayatekeleza kwa namna yoyote ile.
Ni Mimi rafiki yako,
Baraka Maganga.
Bmaganga22@gmail.com.
0754612413/0652612410.



Posted via Blogaway


No comments:

Post a Comment