Tuesday, November 17, 2015

Je Waijua Picha Unayojijengea Akilini Mwako?


Habari za wakati huu ndugu msomaji wa mtandao huu wa kona ya maarifa mtandao ambao upo ili kuhakikisha kuwa unapata mambo mazuri ya kukujenga na kukuhamasisha. Leo nataka kukushirikisha jambo lifuatalo:-
Kwa kawaida binadamu amekuwa ni mtu wa kufikiria mambo mengi juu ya maisha yake. Kutokana na fikira hizo hapo ndipo binadamu huwa anajijengea picha mbalimbali juu ya maisha yake. Picha hizi huendana na fikira za mwanadamu kwa kiasi kikubwa sana. Yaani kama mtu anawaza fikira hasi na kuyaona maisha kwa mtazamo hasi basi picha zote atakazojijengea akilini mwake zitakuwa ni picha hasi ambazo zimejaa kushindwa, visingizio, woga na vipingamizi kadha wa kadha. Wakati kama mtu anawaza fikira chanya atakuwa na mtazamo chanya na hivyo atajijengea picha za ushindi, na mafanikio kwa kila anachokifanya n.k.
Je picha hasi zinatoka wapi?
Picha hasi hutokana na fikira hasi ambazo chanzo chake kikubwa chaweza kuwa kauli za wazazi wetu, ndugu wa jirani au marafiki wa karibu nasi. Mara nyingi watu wanaotuzunguka huwa wana madhara makubwa sana kwetu, madhara haya yaweza kuwa hasi kama nao ni hasi au chanya kama wao wanakauli chanya. Mara nyingi tumekuwa ni watu wa kuamini sana kwa yale ambayo tumekuwa tukiambiwa na watu wa karibu nasi jambo ambalo muda mwingine huweza kutuletea madhara makubwa sana. Katika hali ya kawaida mtoto ambaye amekuwa katika hali ya kusemwa kuwa huna akili, wewe ni mbumbumbu, huwezi lolote pindi anapokuwa amekuwa mtu mzima huwa anachukulia kauli hizi kama ukweli wa maisha yake halisi na hivyo kujijengea picha hasi kichwani mwake ambazo humfanya ajione hawezi lolote na nimbumbumbu haswa.
  Ndugu msomaji ni muhimu uelewe vizuri aina ya picha ambazo unajijengea. Kwa kuwa wote tunahitaji mafanikio makubwa maishani basi tusiende kinyume na kanuni za mafanikio kama kanuni hii rahisi ambayo inaseama huwezi kujijengea picha hasi na ukapata matokeo chanya au picha chanya na ukapata matokeo hasi. Yaani ni sawa na mkulima alimaye mtama hutegemea kuvuna mtama na sio ulezi. Kama akipanda mtama akitegemea kupata ulezi basi mkulima huyu atakuwa na matatizo makubwa.
  Kimsingi kama unataka kuendelea na kupata mafanikio makubwa jijengee picha chanya ili zikuletee matokeo chanya lakini kumbuka picha chanya inatokana na fikira chanya. Na picha chanya ni ile hali ya kujitabilia au kujionea maisha yako katika hali yakushinda wakati picha hasi ni ile Hali ya kujionea maisha katika kushindwa.
Ni mimi rafiki yako.
Baraka Maganga.
Bmaganga22@gmail.com.
0754612413/0652612410.


No comments:

Post a Comment