Sunday, November 22, 2015

Ni Wao Sio Wewe, Ni Wewe Sio Wao

.
Kama wameshindwa ni wao sio wewe. Kushindwa kwa watu kusikufanye nawe ushindwe. Binadamu tumeubwa sawa haya ni maneno ya watu wengi lakini unaposema binadamu tumeubwa sawa ni neno pana kidogo maana huo usawa unaouzungumzia wewe ni katika mawanda yapi. Mfano leo hii ukisema binadamu ni sawa kiakili huoni kama unakosea, maana binadamu tunatofautiana sana tena sana ndio maana kuna warefu, wafupi, weupe, weusi, wenye ulemavu na wasio n.k. wale ambao wanaamini kuwa binadamu ni sawa ndio hutumia watu wengine kama marejeleo yao kwa kiasi kikubwa tena sana ndio maana wao huamini kuwa kama mtu fulani alishindwa basi nao watashindwa kwa kuwa binadamu wote ni sawa. Mara nyingi watu hawa huwa ni wenye mtazamo hasi kwa kuwa wao huamini kuwa binadamu ni sawa na inapotokea mtu fulani anataka kufanya jambo Fulani sawa na mtu au watu Fulani kwa kuwa wao wanamtazamo hasi basi hukimbilia haraka kwenye marejeleo ya watu walioshindwa na sio waliofanikiwa. Hii ni kutokana na mtazamo wao hasi.
Nimekueleza kuwa kauli ya kusema kwamba  binadamu wote ni sawa ni kauli pana sana( it is a general term) maana inabidi ueleze huo usawa wako upo katika mawanda yapi? Nafikiri tuseme binadamu ni sawa kwa namna ya uumbaji wao na ukuaji mfano tunaweza kusema binadamu aliubwa na mwenyezi mungu kama vile washikadini wa dini zote tunavyoamini, pia binadamu wote ni sawa kwa kuwa wote huzaliwa na mwanamke hapo pana usawa, binadamu ni sawa katika makuzi yao maana wote huzaliwa na wakiwa hawana uwezo wa kuongea, huanza kutambaa, kutembea hatimaye kuongea. Huwa watoto, wakawa vijana, wakazeeka na hatimaye wakafa. Hivyo ni sawa kwa binadamu wote maana hakuna binadamu ambaye aliwahi kuwa mzee kisha akarudi ujana kisha utoto hapajawahi kutokea kitu kama hicho hapa duniani. Sasa unaposema binadamu wote ni sawa lazima utueleze usawa huo upo katika mawanda yapi?
Binadamu ni sawa katika mawanda ambayo nimekuonyesha hapo juu, lakini nini kimeniasukuma sasa mpaka nikuambie ni wao sio wewe na ni wewe sio wao, hapa namaanisha kuwa kama wameshindwa au walishindwa niwao na sio wewe na kama umeshindwa ni wewe sio wao. Nachotaka kusema hapa ndugu msomaji ni kuwa tambua kuwa binadamu tunatofautiana katika mawanda mbalimbali kama ilivyo katika kufanana, mawanda hayo ndio huleta utofauti miongoni mwetu na ndio maana nimesema ni wao sio wewe na ni wewe sio wao. Nakuletea mawanda hayo ili unielewe zaidi,
1. Utendaji, tunaweza kuwa tunafanya kazi sawa lakini utendaji wetu wa kazi ukawa tofauti kabisa ndio maana waalimu wawili mfano wanaofundisha somo moja wanaweza kutofautiana ambapo itatokea mmoja akaeleweka zaidi kuliko mwingine. Hii ni kutokana na utendaji wao kutofautiana hivyo kutokana na mawanda ya utendaji tunaweza kusema ni wao sio wewe na ni wewe sio wao. Yaani kama wameshindwa/wameweza ni wao, na kama umeshindwa/umeweza au kufanikiwa ni wewe sio wao.
2. Uwajibikaji, binadamu tunatofautia kiuwajibikaji hivyo uwajibikaji wa mtu mmoja na mwingine ni tofauti sana kutokana na utofauti huu wa kiuwajibikaji utakutana na makundi matatu ya watu ambapo la kwanza ni wanawowajibika sana, pili wanawowajibika wastani na tatu na mwisho ni wale wenye uwajibikaji mbovu. Hivyo ndivyo tunavyotofautiana kiuwajibikaji.
3. Fikira, binadamu tunatofautiana kifikira sana tena sana, kuna wengine wana fikira potovu na wengie hawana fikira potofu hivyo kama wanafikira potovu/sahihi ni wao sio wewe na kama unafikira potovu/sahihi ni wewe sio wao.
4. Mtazamo,binadamu tunatofautiana kimtazamo tena kwa kiasi kikubwa sana. Kuna wale wenye mtazamo hasi na wale wenye mtazamo chanya tofauti hizi za kimtazamo huamua tofauti za matendo yetu. Yaani mtu mwenye mtazamo hasi huwa na matendo yenye kuendana na mtazamo wake na yule mwenye mtazamo chanya pia huwa na mtazamo wenye kuendana na mtazamo wake. Hivyo kama wanamtazamo hasi/chanya ni wao sio wewe na kama unamtazamo hasi/chanya ni wewe sio wao.
5. Kiwango cha uvumilivu, hapa pia tunatofautiana sana. Tunaweza kuugawa uvumilivu wa binadamu katika makundi makuu matatu ambapo tutapata uvumilivu mkubwa, wastani na mdogo. Kila aina ya uvumilivu una watu wake hivyo basi kama upo kwenye aina Fulani ni wewe na sio wao na kama yupo kwenye aina Fulani ya uvumilivu ni yeye sio wewe.
6. Umakini, binadamu tunatofautiana katika kiwango cha umakini ambapo wengine ni makini sana na wengine sio makini sana. Ndio maana utawasikia watu wakisema yule jamaa ni mtu makini katika utendaji kazi wake wakati utasikia mwingine akisema yule jamaa hayupo makini kabisa katika utendaji kazi wake.
Sikuandika makala hii ili kukutofautishia tabia za binadamu bali nimeandika makala hii ili kukufungua na kubwa zaidi kukusihi uache kutumia watu kama marejeleo tena watu walioshindwa badala yake jijengee mazoea ya kujiamini na amini kuwa binadamu tunatofautiana sana hivyo basi kama umeshindwa ni wewe na kama wameshindwa ni wao. Pia wewe ulieshindwa usitake kujitumia kama mfano na uwafanye watu waamini kuwa watashindwa kama wewe. Kumbuka ni wao sio wewe na ni wewe sio wao. Zaidi usiruhusu historia ya mtu ikukatishe tamaa maana sio yako ni yake.
Ni Mimi rafiki yako,
Baraka Maganga.
Bmaganga22@gmail.com.
0754612413/0652612410.


No comments:

Post a Comment