Ni wengi sana tumekuwa tukitaka kushinda maishani yaani
kufanikiwa kwa kiasi kikubwa. Ni kweli kila mpambanaji huwa anataka kushinda
katika kila pambano analoshiriki na ndio maana kiuhalisia kila binadamu
anapenda kufanikiwa na ndio maana kichwa cha makala nimeamua kukiita siri ya
kushinda maishani nikiwa nataka kulenga siri ya kufanikiwa maishani.
Tumekuwa ni watu wenye kutaka kufanikiwa kwa kiasi
kikubwa kila mtu anapenda apate mafanikio makubwa, mimi nataka mafanikio, wewe
unataka mafanikio na yule anataka mafanikio. Lakini kwanini tumekuwa tukijikuta
kila mara tuko pale pale tulipokuwa jana yaani hatuendi mbele hata hatua moja
kimaisha. Kila mara tumekuwa watu wa kushindwa hata kama tukijitahidi kupanga
mipango muhimu na mizuri lakini wapi huwa tunajikuta tumeshindwa tena na tena.
Je unakumbwa na tatizo hili la kushindwa mara kwa mara
pamoja na kwamba umejiwekea malengo, umepanga mikakati ya kutekeleza malengo
yako na mengine mengi? Kama jibu ndio karibu nikupe njia rahisi ya kuweza
kuepukana na hiyo hali.
Siri ya kushinda ni vitendo.
Hii ndio siri kubwa na ambayo ninata uifahamu kwanzia leo kuwa siri ya kushinda
ni vitendo. Kwanini nimesema hivyo, nimesema hivyo ni kwa kuwa takwimu
zinaonyesha kuwa watu wengi sana wamekuwa au tumekuwa ni mabingwa wa kupanga
mipango mizuri, kuweka mikakati kabambe, kuweka malengo mazuri sana ambayo
ukiyasoma kwa kiasi kikubwa ni yanavutia sana tena sana, kiasi kwamba kila
ukiyasoma yanakuvutia na unayafurahia lakini wakati unafanya hivyo unasahau
kitu kimoja kwamba mipango tunayoiweka sio kwa ajili ya kuiweka kwenye
makaratasi au kwenye karatasi tu bali tunatakiwa kuifanyia kazi yaani tuweke
katika vitendo.
Kila kitu huanza kwa mpango, malengo na mikakati ambayo
mara nyingi sana huwa inakuwa imeandikwa kwenye karatasi, wengi tunaweza
kufanya hili jambo lakini jambo ambalo linatushinda ni kuhamisha yale yaliyomo
katika makaratasi au karatasi na kuyapeleka katika vitendo, hili ndio jambo
ambalo linatushinda kwa kiasi kikubwa sana na ndio maana tunashindwa kushinda (kufanikiwa).
Kama sio mtu wa kuchukua hatua ya kutenda kamwe sahau
kuhusu kushinda maana huto weza kushinda kamwe maishani, kushinda huja kutokana
na kuamua kuweka ile mipango tuliyojiwekea katika vindeo hivyo basi siri ya kushinda
ni vitendo. Unatakiwa kutenda na uendelee kutenda bila kuchoka, kuhairisha wala
kukata tamaa maana katika matendo ndimo huwa tunapata ushindi.
Mara nyingi tumekuwa tunashindwa kuchukua hatua ya
kutenda kutokana na sababu mbalimbali kama vile:-
1. Kuhisi
uvivu pale tunapotaka kutenda, kama unakabiliwa na hii
hali basi jua kabisa hiyo hali sio nzuri kwako na inaweza kukuzuia wewe kutenda
jambo. Hivyo tambua kuwa hakuna matunda mazuri katika uvivu, yaani uvivu hauzai
matunda mazuri hata siku bali huzaa matunda mabovu hivyo uogope uvivu.
2. Uoga, wakati mwingine
pale unapotaka kuchukua hatua ya kutenda unakabiriwa na hali ya kuogopa kuwa
watanichukuliaje au ntaonekanaje hali hii inaweza kukufanya usichukue hatua
yoyote na hivyo kujikuta umeshindwa kutenda na hatimaye unabaki pale pale.
3. Hofu, wakati mwingine huwa
unakumbwa na hofu pale unapotaka kutenda jambo fulani. Hofu ya kushindwa, hofu
ya kuto kujulikana ni mifano wa hofu ambazo zinaweza kukuzuia wewe kuto tenda
jambo fulani. Kabiliana na hofu hizi mara moja.
Hakika siri ya mafanikio/ kushinda ni
vitendo, kuweka malengo sio mafanikio ila kuyaweka malengo yako katika matendo
ndiko huleta mafanikio, kupanga mikakati, na mipango pia hakuleti mafanikio ila
kutenda. Hiyo ndio siri niliyopanga kukushirikisha leo hii, natumaini utakwenda
kushinda sasa.
Mwandishi: Baraka Maganga.
Mawasiliano:-simu-0754612413/0652612410.
:-barua pepe -Bmaganga22@gmail.com.
No comments:
Post a Comment