Wednesday, March 23, 2016

Mambo Matatu Yanayoweza Kukufanya Usitimize Ndoto Yako.


Kila mtu ana ndoto zake maishani hilo ni swala ambalo naliamini maishani kuwa wewe una ndoto, yule anandoto zake na mimi ninazo za kwangu ambazo kwa kiasi kikubwa sana zinatofautiana sana tena sana. Kwa kuwa ndoto zetu zinatofautia hili ni jambo jema maana hili ndilo hupelekea hata sisi kutofautiana kimaisha na kimatendo. Hivyo sio jambo baya kuwa na tofauti ya ndoto kati yangu mimi na wewe na yule.

Leo nataka nikushirikishe mambo matatu ambayo yanaweza kukufanya ushindwe kutimiza ndoto zako mambo hayo ni kama yafuhatayo.


  Hofu, ile hali ya kuwa na wasiwasi mwingi juu ya lile unalotaka kulifanya inaweza kuwa adui mkubwa sana wa ndoto zako. Najua kuwa unazifahamu aina nyingi sana za hofu, lakini mimi nataka kugusia hofu ya aina moja tu ambayo ni hofu ya kuto kujulikana. Mara ngapi umekuwa kila unapotaka kufanya jambo fulani unasikia ndani yako kuna sauti inakuhamaasisha kuwa nani anakujua wewe hapa mjini nani?, ukisikia sauti hiyo usijidanganye kusema ni malaika wa mungu anakusihi uache, hapana jua hiyo ni hofu. Ni kweli hakuna anayekujua lakini hilo halikuzui wewe kuweza kutekeleza jambo fulani. Kweli hawakujui kwa sababu hujajitambulisha kwao wewe ni nani. Sasa  pengine kupitia lile unalotaka kulifanya ndilo linaloweza kukufanya ufanikiwe kwa kiasi kikubwa na hatimaye ukawa umejitambulisha kuwa wewe ni nani na ukawa usha fahamikia tayari. Sasa kabiliana na hii hofu tenda lile unaloliona ni sahihi na utajulikana tu. Hakuna aliyezaliwa akiwa anajulikana.

2.    Kutaka kuanza na makubwa,umekuwa ni mtu wa kutaka kusubiri eti mpaka uwe na kitu kikubwa ndio uweze kutenda jambo fulani. Ndugu msomaji waswahili walisema “haba na haba hujaza kibaba”. Anza na kidogo wala hata usiogope kuanza na kitu kidogo maana kidogo huzaa kikubwa sasa wewe unaposubiri eti upate kikubwa ndipo utende huko ni kujidanganya na kujipotezea muda na kuendelea kudumaza ndoto yako maana hakuna namna ambayo unaweza kupata kitu kikubwa  bila kupitia kitu kidogo hivyo basi njia ya uhakika ya kukufanya wewe uweze kufanikisha ndoto zako ni kuanza na kidogo siku zote. Hata kama ni biashara unataka kuwa na biashara kubwa sana wewe anza na mtaji hata wa milioni mbili hata kama ndoto yako ni kuwa na biashara ya milioni ishirini na hiyo milioni mbili baada ya muda itajizalisha na kufikia hizo milioni ishirini unazozitaka. Hivyo nakusii usiue ndoto yako kwa kutaka eti kuanza na kikubwa maishani bali wewe anza tu pale unapohisi upo tayari na unachakuanzia hata kama ni kidogo.


3.    Kuto kuwa na maono sahihi, kama unataka kufanikiwa lazima uwe na maono. Maaono ni ile hali ambayo unaweza kuwa unajionea mambo ya mbele kifikira zaidi. Mfano unajionaje wewe baada ya miaka mitano toka leo. Kila mtu ana namna ambayo anajiona atakavyokuwa baaada ya miaka mitano mwingine anaweza kujiona kuwa anakuwa mtu maarufu sana, anakuwa mfanyakazi bora, mjasiriamali mkubwa n.k. hayo ndio maono. Sasa ikitokea huna uwezo wa kuona ndani ya miaka mitano utakuaje basi hii ni njia moja wapo ya kuweza kuua ndoto zako. Maono huwa kama tasirwa/picha mabayo unayaona maisha yako kifikira zaidi. Na maono sio malengo hivyo usijichanganye niliposema labda unajiona kuwa mfanyakazi bora baada ya miaka mitano ukajua ni malengo hapana malengo na maono vinatofautiana. Ingawa maono yanategemea malengo yako na malengo yako yanategemea maono yako. Hivyo basi hakikisha una maono sahihi yaani unauwezo wa kujiona ndani ya miaka mitano utakuaje au utakuwa wapi kimaisha.

Mwandishi: Baraka Maganga.
Mawasiliano:-simu-0754612413/0652612410.
                    :-barua pepe -Bmaganga22@gmail.com.



No comments:

Post a Comment