Thursday, March 24, 2016

Unashindwa Kwa Sababu Kitu Hiki Kimoja Kimekushinda Kufanya.


Katika maisha tumekuwa tukifanya mambo kadha wa kadha ambayo wakati tukifanya mambo haya huwa tunakuwa na uhakika kuwa mambo hayo ni yenye kutulendea mafanikio makubwa maishani. Lakini kuna wakati huwa tukijikuta tumeshindwa kufanya jambo fulani huwa tunafanya tafakari ya hali ya juu kwa ajili ya kutaka kutambua sababu haswa iliyofanya tusiweze kufanikiwa.  Baada ya kugundua sababu hapa ndipo matatizo huanza na mara nyingi tatizo hili ndilo limekuwa likitufanya tusifanikiwe siku zote.


Unaweza ukashindwa kutekeleza jambo fulani, na baada ya kufanya tathimini ya nini kimekufanya usifanikiwe ukagundua pengine ni kwa sababu uliswhindwa kutumia muda vizuri yaani kuna vitu ambavyo ulivifanya na hatimaye vikawa chanzo cha kukupotezea muda kwa kiasi kikubwa sana na hatimaye ukajikuta umeshindwa  kulitekeleza hilo jambo. Swala la kuwa umeshindwa kutekeleza jambo ulilolipanga kutokana na kufanya mambo ambayo ni kinyume na uliyotakiwa kufanya ili kulitekeleza jambo fulani, umekuja kuligundua baada ya kufanya tathimini ya kina ya nini kimekufanya usifanikishe jambo husikia. Sasa hapa suluhu ya yote haya ni kuyaacha yaende yale mambo yote yanayokupotezea muda lakini hapa ndipo huwa tunafanya makosa makubwa sana maana huwa hatukubali kuyaacha yaende badala yake tunayashikilia tu na hatimaye tunajikuta tumeshindwa zaidi na zaidi. Hivyo basi makala hii inasema unashindwa kwa sababu umeshindwa kuyaacha yaende, hiki ndicho kitu kimoja kinachokufanya usifanikiwe.

Ni vyema ukatambua kuwa maishani usiwe kinganganizi wa mambo yasiyo ya msingi wala maana yoyote kwako badala yake fanya jambo moja tu kwa yale ambayo unahisi kuwa yanakupotezea muda wako kwa kiasi kikubwa au hayana maana maishani mwako basi yaache yaende tu hakuna namna nyingine bali ni kuyaacha yaende tu. Usiwe mtu wa kuhaha huku na huku kuyakumbatia mambo ambayo kimsingi hayana maana. Tumekuwa ni watu wa kushikilia mambo ambayo hayana tija kwetu na mbaya zaidi ni kuwa huwa tunakuwa tunafahamu kabisa kuwa jambo fulani halina tija wala maana kwangu lakini huwa tunaendelea kukomaa nayo tu au zaidi na zaidi yaani tunakomaa nayo tu. Sasa jambo hili ndilo linatufanya tuzidi kushindwa kila mara maishani.

Nyani ni kiumbe ambaye kwa wakati mwingine huonekana ni mjanja sana na ni msumbufu kwa wanadamu, hili kwa wale ambao wanafanya shughuli za kilimo katika maeneo ambayo nyani ni wengi watakuwa wananielewa kirahisi sana, lakini nyani huyu huyu ambaye huonekana mjanja huwa anaponzwa na tabia moja tu nayo ni ile ya kuto kuacha yaende. Kule nchini Brazili wanaowinda nyani hutumia njia rahisi sana ya kumtega nyani, wao huchukua mtego ambao huwa na uwazi sehemu moja ambapo nyani anaweza kupitisha mkono wake, kisha katika lile tundu huwa wanatumbukiza ndizi na kisha kuweka ule mtego pahali fulani. Sasa nyani akija huwa anataka kuchukua ile ndizi, lakini kwa jinsi ambavyo mtego ule ulivyo ni kuwa nyani akishaingiza mkono wake hawezi kutoka akiwa ameshikilia ndizi, nyani hulitambua hilo kuwa hawezi kutoa mkono akiwa na ndizi hivyo aidha aiachie ndizi ili asikamatwe au la. Lakini cha ajabu ni kuwa nyani huyu huendelea kung’ang’ania ndizi husika mpaka wenye mtego hufikia na kuweza kumkamata. Hivyo kinachomponza nyani siku zote ni ile tabia ya kuto acha yaende.
Sasa tabia hii ya nyani ndio hata binadamu tumekuwa nayo mtu utakuta anayafahamu fika madhara ya utumiaji wa pombe kupita kiasi lakini anaendelea, madhara ya uvivu lakini anaendelea, madhara ya kutokuweka malengo lakini anaendelea tu kufanya mambo ambayo yanamfanya asiweke malengo n.k.

Tambua kuwa uwezo wa kushindwa au kushindwa upo mikononi mwako chagua leo kushinda na utashinda tu na chagua leo kutokushinda na hutoshinda kamwe vilevile.

Mwandishi: Baraka Maganga.
Mawasiliano:-simu-0754612413/0652612410.

                    :-barua pepe -Bmaganga22@gmail.com

No comments:

Post a Comment