Habari za wakati huu ndugu
msomaji wa mtandao huu wa kona ya maarifa ni matumaini yangu kuwa hu mzima wa
afya na unaendelea vyema katika harakati zako za kuhakikisha unayatekeleza yale
ambayo umekwisha jiweke na ukizingatia kuwa mwaka ndio huo uko ukingoni.
Leo nataka kukushirikisha
juu ya jambo hili nalo ni kukosekana kwa uhusiano wa moja kwa moja kati ya
elimu ya darasani na mafanikio, hii ni kutokana na sababu kuwa kuna watu ambao
wamekuwa wakiamini kuwa ili wafanikiwe ni lazima wae na elimu ya darasani. Yaani
kwao wao ni kuwa ili mtu aweze kufanikiwa ni lazima awe amesoma sana na angalau
awe na elimu ya degree au masters hapo ndipo atafanikiwa.
Jambo hili limeshamili sana
miongoni mwa jamii nyingi sana hapa kwetu Tanzania ndio maana leo hii msisitizo
kwa wazazi kwa watoto wao ni kuwa soma sana mwanangu ili uje kuwa na maisha
mazuri na yenye mafanikio. Kwa wazazi wengi hapa nchini kwetu ni kuwa mafanikio
hutokana na kusoma na kuwa na degree au masters. Yaani msisitizo wao mkubwa ni
katika elimu ya darasani ambayo itakufanya uajilliwe na katika ajira, ajira
hutolewa kutokana na elimu ya mtu, yaani mwenye elimu ya juu ndiye hupewa ajira
yenye mshara mkubwa na kwa kuwa tunaamini kuwa mshara mkubwa ndio hukufanya uwe
na pesa na kwa kuwa wengi wetu hupima mafanikio kwawingi wa pesa basi huwa
tunaamini katika ajira na ajira huja kutokana na elimu yako ndio maana wazazi
wamekuwa wakitusisitiza juu ya elimu ya darasani.
Lakini ndugu msomaji wa
makala hii nataka ujiulize kama kweli unaamini kuwa mafanikio hutokana na elimu
ya darasani je ni wangapi ambao pamoja na masters zao na degree zao lakini bado
ni masikini?, hawana mafanikio yoyote yaani ila wanaringia elimu zao za
darasani?. Jibu nadhani ni wengi, sasa kama ni wengi huo uhusiano unatoka wapi wa
kukufanya wewe uamini kuwa mafanikio ya kweli hutokana na elimu ya darasani
pekee?. kama elimu ya darasani ndio kigezo cha mafanikio ya watu je nani
angekataa kusoma mpaka kupata hizo degree na masters?, maana hakuna asiyependa
mafanikio.
Na jiulize tena ni wangapi
ambao pamoja na kutokuwa na elimu ya darasani lakini wanamafanikio makubwa sana
na nimatajiri wakubwa duniani?. Mfano ni tajiri Bill gate ambaye aliachana na
habari za shule na kuamua kujifundisha mwenyewe na kisha kugundua program ya
Microsoft katika computer. Matajiri wangapi au wafanyabiashara wangapi
unaowajua hapo mtaani hawana elimu ya darasani lakini ndio matajiri wakubwa.
Utamaduni wa kuwasisitiza
watoto au ndugu zetu kusoma sana ili kupata maksi nzuri darasani na baadae
kupata ufaulu wa juu kisha wapate kulipwa kutokana na elimu zao ni utamaduni wa
zana za kale za mawe sio utamaduni muhimu katika ulimwengu wa sasa wa taarifa.
Ulimwengu wa sasa hausemi kuwa mwenye elimu ndiye atakaye fanikiwa bali unasema
kuwa mwenye taarifa sahihi ndiye atakaye fanikiwa. Yaani utofauti wa taarifa ya kitu fulani kati
yako na mtu mwingine ndio utaamua nani afanikiwe. Utaratibu wa kasome mwanangu
ili uje kuwa na maisha mazuri kutokana na ajira yako ni utaratibu ambao
umepitwa na wakati sasa. Na kwa mujibu wa mwandishi mashuhuru wa marekani bwana
Robert
Kiyosaki huu ni utaratibu mbovu yeye anasema kuwa kitakachomfanya mtu
afanikiwe ni elimu juu ya pesa na elimu hii haifundishwi shuleni badala yake
mtu anatakiwa ajifunze kutoka kwa wazazi wake. Mwandishi huyu anasisitiza
katika umuhimu wa elimu juu ya fedha maana haifundishwi darasani na ndio maana
hata wenye degree na masters zao wanakuwa masikini na waliokosa mafanikio.
Sisemi kuwa elimu ya
darasani sio elimu ya msingi, ni elimu ya msingi sana tena sana kwa ulimwengu
wa leo ambao umejaa ushindani sana ambapo ni muhimu kwa mtu kupata angalau
degree hata moja, nachopinga ni kuwa elimu hii isitumiwe kama tiketi ya
kufanikiwa yaani kwana kwamba mwenye elimu ya darasani ndiye mwenye uhalali wa
kufanikiwa hili ndilo nilipingalo maana kuna watu ambao wana elimu na
wanamafanikio na wakati huo huo kuna wale wenye elimu hiyo na hawana mafanikio,
na kwa upande wa pili wa shilingi kuna wasio na elimu na wanamafanikio na hapo hapo
kuna watu ambao hawana elimu na hawajafanikiwa.
Kinachohitajika katika
mafanikio ni namna ya kujifunza kupitia watu waliofananikiwa na kutumia
mafanikio yao kama somo na sio kitu kingine. Elimu ya darasani ni kichocheo tu
ambacho peke yake hakiwezi kufanya kazi. Hivyo usikae kisa huna elimu ya
darasani na ukasema huwezi kufanikiwa. Pia jifunze kuhusu elimu ya pesa maana
ndio muhimu sana kwa ulimwengu wa sasa.
Ni mimi rafiki yako,
Baraka Maganga.
0754612413/0652612410.
No comments:
Post a Comment