Habari ya wakati huu ndugu msomaji wa mtandao huu wa kona
ya maarifa mtandao ambao umejidhatiti katika kuhakikisaha unakupatia maarifa
mapya, maarifa ambayo yatakufanya uwe bora na kuweza kuyafikia mafanikio
makubwa sana maishani. Tumekutana tena katika kutaka kuelimishana juu ya mambo
mbalimbali ambatana name ili ujue leo nimekuletea nini………
Ukizunguka mitaani ukawauliza vijana wengi wanaoshinda
vijiweni wakipiga soga badala ya kufanya kazi kuwa kwanini wanafanya hivyo
watakuambia hatuna kazi ya kufanya, ukiendelea
kuwauliza kuwa ,mbona kuna biashara nyingi, nanyi hamtaki kuzifanya?
utasikia eeh! bwana eeh! hatuna mitaji. Hii ndio imekuwa kauli kubwa sana
miongoni mwetu vijana,na hili ndilo lililonisukuma kuandaa makala hii pengine ulishawahi
kukutana na kauli kama hii ya tatizo ni mtaji miongoni mwa vijana wengi au
pengine nawe ni mojawapo ya watu wanaoitumia na kuiendekeza kauli hii ya tatizo
ni mtaji.
Watanzania tumekuwa bendera fuata upepo, usinielewe
vibaya kwa kusema au kutumia kauli hii lakini
haina budi kusema maana lazima tuwekane wazi maana ongezeko la kauli kuwa
tatizo mtaji ni dhahiri kuwa ni jinsi gani vijana tumekosa fikira za
kimapinduzi na badala yake tumekuwa vibendera fuata upepo ambapo ukisikia
mwenzio kasema kuwa hajaanzisha jambo Fulani kwa sababu hana mtaji basi nawe
unachukulia hivyo hivyo na kujivika sababu hiyo na kuifanya kuwa kama ngao
kubwa ya kushindwa kwako katika biashara.
Kwanza jambo ambalo ni baya sana ambalo tumekuwan nalo na
kwa kiasi kikubwa tumekuwa nalo ni kuamini kuwa pesa ndio mtaji muhimu katika
biashara zetu, jambo hili ni imani potofu sana pamoja na kuwa tumeamini kuwa
pesa ndio mtaji wa kwanza ambayo tayari ni imani potofu tuliyo nayo bado
tumeendelea kujenga imani potofu juu ya imani potofu ambayo ni kuwa pamoja na
kuamini kuwa pesa ndio mtaji nambari moja kwetu bado tumekuwa tukiamini kuwa
ili kuanzisha biashara, ufugaji au shughuli za uwekezaji ama kilimo lazima tuwe
na mitaji mikubwa yaani pesa nyingi. Leo hii sio ajabu kumkuta kijana akitaka kuanzisha biashara fulani
utakuta anapiga hesabu za mamilioni kama mtaji wakati anaweza kuanzisha biashara
husika kwa mtaji hata wa laki moja.
Tabia ya kufikiria pesa nyingi katika uanzishaji wa
biashara, kilimo au uwekezaji ndio kimekuwa chanzo kikubwa cha kuanza kwa kauli
ya tatizo mtaji. Tumesahau kuwa hatua moja ndio huanzisha safari na ni hatua
hiyo hiyo ndiyo umaliza safari ya umbali mrefu. Sio lazima uanze na pesa nyingi
sana katika biashara yako au pesa nyingi katika uwekezaji wako. Nina mfano hai
wa ndugu yangu ambaye alianza uwekezaji kwa mtaji wa shilingi 25,000, lakini
leo hii anamiliki ekari za kutosha za mashamba ya miti ikiwa ni pamoja na
usafiri wake binafsi( gari ya kutembelea). Yaani hapa ni rahisi sana kuuelezea
mfano huu ni kuwa shilingi elfu 25 ndio iliyo zaa mamilioni. Kwahiyo ndio maana
tunasema hatua moja ni muhimu kuliko hatua nyingi ulizotembea au utakazotembea.
Kama mtu huyu angeogopa kutumia shilingi elfu 25 leo hii angebaki kulalamika
kama wewe kuwa tatizo mtaji na wala leo nisingalimtumia kama mfano katika
makala hii.
Ni kweli pesa kwa kiasi kikubwa ndio kila kitu
katikashughuli za kilimo, biashara, uwekezaji na maeneo mengine ya kibiashara
na kiuzalishaji lakini pesa pekee haitoshi. Je kama pesa pekee haitoshi nini
basi kinatakiwa kitangulie kabla ya pesa?.
Kabla ya mtaji wa pesa kuanza mtaji nambari moja ni
fikira au wazo/mawazo. Yaani huu ndio mtaji nambari moja ambao kila mtu anao
leo hii huwezi kusema eti mtu fulani huwa hafikirii, yaani huo ni upotoshaji
maana hakuna mtu ambaye huwa hafikirii. Kila mtu aliumbwa na uwezo huu wa kufikiri,
na uwezo wa kufikiri unatofautiana toka kwa mtu hadi mtu na kinachofanya
utofautiane ni namna ambayo kila mtu hutumia fikira zake katika kupambana na
chagamoto zinazomkabili. Wale ambao hawataki kumiza bongo zao juu ya ni jinsi
gani watakabiliana na changamoto za kimaisha ndio hukimbilia kusema pesa ndio
mtaji na pamoja na kutambua kuwa pesa ni mtaji bado hao hao hurudi na kusema
mtaji ambao ni pesa ni tatizo. Kila kitu huanza kama wazo kisha wazo hilo ndio
hugeuzwa na kufanywa au kuleta pesa. Kuna
historia ya dada mmoja ambayo niliisoma katika kitabu fulani yeye alieleza kuwa
hakuwa na pesa ya kuanzisha biashara aliyokuwa akiifikiria lakini alikuwa na
wazo ambalo ndio mtaji wake, hivyo akashirikisha watu na baadae akapata pesa
kwa ajili ya kuanzisha biashara yake hiyo. Mfano huu unatuonesha kuwa tatizo
sio mtaji ambao unatufanya tushindwe kuanzisha biashara au shughuli za kilimo,
au za uwekezaji bali mawazo yetu mabovu ndio hupelekea hali hiyo. Hivyo kwa
kuwa wazo ndio mtaji mkubwa na mtaji huu ukiwa mbovu basi hatutaweza kufanya
chochote zaidi ya kulaumu kuwa tatizo ni mtaji.
Usikae na kupiga piga makelele kijiweni kuwa tatizo ni
mtaji bali kaa tulia na ufikiri utajikwamua vipi katika changamoto
zinazokukabili na kumbuka matatizo hayatatuliwi kwa kukaa kijiweni na kupiga
soga badala yake muda unaoutumia kupiga soga utumie katika kusoma vitabu au
kufuatilia hadithi za watu waliofanikiwa wa ndani na nje ya nchi.
Ni mimi rafiki yako
Baraka Maganga
0754612413/0652612410.
No comments:
Post a Comment