Habari za wakati huu ndugu msomaji wa mtandao huu wa kona
ya maarifa ni matumaini yangu kuwa hu mzima wa afya na unaendelea vizuri katika
harakati zako za kutekeleza majukumu yako na hatimaye kuzifikia ndoto zako.
Wengi tumekuwa tukiimba wimbo mafanikio mara kwa mara,
lakini jiulize ni wangapi waimbao wimbo huu wanafanikiwa? Nadhani jibu ni
wachache kati ya wengia ambao wanaimba wimbo huu wa mafanikio ambao
wanafanikiwa kweli. Sababu za kutokufanikiwa zinaweza kuwa nyingi sana miongoni
mwetu. Hapa nina kuletea sumu nne za mafanikio, yaani vitu vinne ambavyo
vinaweza kuhatarisha mafanikio iwe umeyapata tayari, au ndio unaelekea
kuyapata.
1 .lawama,
hii ni sumu nambari moja ya mafanikio, ukijiona wewe ni mtu wa kulaumu mara kwa
mara jua kuwa huwezi kufanuikiwa au kwa lugha rahisi ni kuwa jua kuwa mafanikio
yatakukimbia. Ukiwa wewe ni mtu wa kuilaumu serikali, wazazi, waalimu,
wanafunzi wenzako, mpenzi wako au mkeo/mumeo, tambua kuwa hutoweza kufanikiwa.
Lawama hukuondoa katika mafanikio au katika mstari wa kuyapata mafanikio kwa
kuwa lawama inakufanya uyakimbie
majukumu. Yaani tabia ya mtu anayelaumu ni kuwa huwa anawalaumu watu hata kwa
yale ambayo yanamhusu yeye moja kwa moja. Mfano mwanafunzi hajasoma vizuri kwa
ajili ya mtihani wake wa mwisho lakini akilini mwake anawazo la kufaulu,
inapotokea amefeli huanza kuwalaumu waalimu kuwa hawakufundisha ipasavyo.
2. visingizio, huyu ni pacha wa
lawama, kwanini nimesema hivyo ni kwa kuwa lawama na visingizio vinaendana
kimatendo na kitabia. Yaani wakati mwingine huwa ni vigumu sana kutofautisha
mtu mwenye kulaumu na mtu mwenye visingizio. Wakati yule wa kulaumu anawalaumu
watu basi yule wa visingizio huwasingizia watu. Yaani mfano katika mfano wetu
hapo juu wa mwanafunzi aliyefeli kuwalaumu waalimu, basi hapa atawasingizia
waalimu kuwa hawakufundisha vizuri ndio maana akafeli wakati sio. Watu wengi
wamekuwa wakiwasingizia watu wengi sana juu ya kutokufanikiwa kwao wapo
wanaowasingizia wazazi, waalimu, madaktari, serikali n.k. lakini ukiwachunguza
watu hawa utagundua kuwa kadri wanavyosingizia ndivyo wanavyojiweka mbali na
mafanikio. Hivyo basi achana na habari za kusingizia singizia. Kama ulikuwa
hujui basi faha,u kuwa visingizio pia hutuondelea uwezo wa kufikiri na
kutufanya tushindwe hata kutatua matatizo madogo na badala yake tusingizie tu
watu wengine. Hivyo acha kabisa tabia hii.
3.
hofu, sumu nyingine ya mafanikio ni hofu, mara nyingi watu
wamekuwa na mipango na mawazo makubwa sana ambayo yanaweza kuwafanya
wakafanikiwa kwa kiasi kikubwa lakini punde tu watakapo kujalibu kutekeleza
mipango yao na malengo yao, hofu huja na kupeperusha mipango na malengo yao na
huo ndio huwa mwisho wao. Anza kwa kupinga hofu mara moja kama kweli unataka
kufanikiwa. Utakapoweza kujikwamua katika mtego huu wa hofu basi mafanikio
yatakuwa halali yako. Hofu itakukosesha mambo mengi kama ukiiruhusu ikutawale,
na njia moja wapo ya kukabiliana na hofu ni kufanya kile ambacho unakiuogopa
zaidi kuliko vingine.
4.Kuhairisha
mambo,jiulize leo hii ni mara ngapi umekuwa ukitaka kujihusiha
na jambo fulani, tena la msingi na ambalo lina tija kwako, lakini ghafla
ukatishwa tu kidogo au ukaingiwa na hofu kidogo na matokeo yake unaacha
kulifanya jambo hilo husika. Leo hii watu wengi wamekuwa wakibaki pale pale
walipo kwa kuwa wametawaliwa na tabia ya kuhairisha mambo. Kama kweli unataka
kufanikiwa hakikisha unaipinga vikali tabia hii kwani kuhairisha mambo ni
hatari sana kwa maendeleo yako. Wapo watu wengi ambao wamekuwa wakiona ufahari
kuhairisha mambo yao ya msingi, na wasijue kuwa wanajiua wenyewe alafu baadae
huanza kuwalaumu na kuwasingizia watu wengine kumbe sababu ni kuwa watu hawa
wametawaliwa na roho ya kuhairisha mambo. Ndio maana siku hizi kuna msemo maarufu
huko mtaani kuwa “watu wengi wanakufa na ndoto zao, hivyo ndoto nyingi zipo makaburini”,
ni kwasababu ya tabia ya kuhairisha mambo.
Kwa ujumla sumu hizi nne za mafanikio, zinaweza kutokana
na sisi wenyewe au kutokana na wale wanatuzunguka. Hilo lisikupe shida bali
jambo la msingi ni kuwa wewe pingana nazo kwa kuwa umeshazifahamu vizuri na
madhara yake pia umeyafahamu.
Ni mimi rafiki yako,
Baraka Maganga.
0754612413/0652612410.
No comments:
Post a Comment