Habari za wakati huu ndugu msomaji wa mtandao
huu wa kona ya maarifa ni matumaini yangu kuwa hu mzima wa afya na mwenye kiu
ya kuendeleza harakati za kuyasaka mafanikio. Nami nakusihi endelea na hali
hiyo wala usikate tamaa, maana yote yanawezekana tu swala ni imani na juhudi tu
ndio zitatufanya tuweze kuyatekeleza yale tuliyojiwekea kama malengo kwetu.
Ni wasaa mwingine tena ambapotumekutana tena
ilikuweza kupeana maarifa mapya ambayo yatatufanya tuwe bora na hatimaye kuweza
kuyafanikisha yale tuliyojiwekea. Leo kuna swali moja ambalo nataka ujiulize
ndugu msomaji wa makala hii, swali lenyewe ni kuwa ni lini haswa itakuwa zamu
yako?. Nataka ufanye hivyo kwa kuwa naamini kuwa akili ya binadamu huanza
kufanya kazi pale inapochochewa kufikiri juu ya jambo fulani tofauti na pale
inapokuwa imekaa tu bila kuchochewa kufanya jambo lolote.
Umekuwa ukiona wenzio wakifanikiwa katika
biashara zao, miradi yao, kazi zao, elimu zao n.k. nachotaka kumaanisha hapa ni
kuwa katika kila ngazi ambayo upo wewe sio wa kwanza yaani kuna watu ambao
wamekutangulia katika kufanya jambo fulani. Kama wewe ni mfanyabiashara kuna
wafanyabiashara maarufu na wakubwa zaidi yako, mchezaji, mwanafunzi, mfanyakazi
n.k. wapo walio juu yako sasa tunaelewa kuwa mtu anapokuwa amefanya mambo
makubwa naya msingi huwa anakuwa anasifika, anapewa heshima kubwa, anachukuliwa
kama mfano wa kuigwa n.k. najua vitu hivyo huwa unakutana navyo katika maisha
yako. Sasa ulishawahi kujiuliza kuwa ni lini nawe itakuwa zamu yako kusifika au
kusifiwa kwa jambo fulani,au kutumiwa kama mfano wa kuigwa?.
Kila mtu maishani huwa kunakuwa mtu mwenye
mafanikio ambaye yeye huvutiwa nae mfano mchezaji chipukizi wa Tanzania anaweza
kuvutiwa na kiwango cha Mbwana Samtta na akatamanikuwa kama yeye sasa jambo la
msingi la kujiuliza ni kuwa ni lini unataka kuwa kama huyo Mbwana Samatta.
Pengine unatamani kuwa mfanyabiashara mkubwa na mwekezaji mkubwa na mashuhuri
kama Reginald Mengi, lakini hujui ni lini na nivipi utakuwa kama yeye, sasa
jambo unalotakiwa kujiuliza nikuwa ni lini utakuwa kama mengi?. Pengine
unatamani kuwa mchekeshaji maarufu kama Masanja Mkandamizaji wa orijino komedi,
unachotakiwa kufanya ni kujiuliza tu ni lini haswa unataka kuwa hivyo?
Nimeshakwisha kutangulia kusema hapo awali
kuwa akili ya binadamu hufanya kazi pale inapoulizwa maswali kama vile kivipi?,
kwanini?, wapi?, saa ngapi? Na memgine mengi kulikopale inapokuwa imeachiwa tu
na kukaa tu huru, bila kufanya kazi yoyote. Kwa kuwa akili ya binadamu hufanya
kazi au huwa katika hali ya kufanya kazi pale inapokuwa inaulizwa maswali
mbalimbali kuliko pale ambapo haiulizwi maswli hivyo basi jijengee mazoea ya
kujiuliza maswali mbalimbali kila wakatiili tu kuhakikisha unapata majibu
ambayo yatakuwa msaada mkubwa kwako na kukupa uvumbuzi wa majibu ya changamoto
zako.
Pili nataka ujiulize swali la ni lini haswa
itakuwa zamu yako ili majibu ya maswali yako uyatumie katika kupanga malengo
yako. Watu wengi wamekuwa hawapangi malengo yao kwa kuwa wamekuwa hawajiulizi
maswali mbalimbali ukijiuliza swali mfano ni lini unataka kuwa mfanyabiashara
maarufu na ukajijibu kuwa mwezi mei
2017, hili litakuwa tayari kama lengo lako ambapo utaifanya akili yako ifanye
kazi ili kuhakikisha jambo hili linakuwa ukweli kwako na hatimaye kulitekeleza.
Ni muhimu kujiuliza maswali mbalimbali juu ya
ni lini unataka kupata kitu Fulani na ni lini utakuwa mtu Fulani. Jingine
kujiuliza swali ni lini haswa itakuwa zamu yako, kujulikana, kusifiwa na
kutumika kamamfano wa kuigwa?, kutaiamusha akili yako na kuifanya ifanye kazi
ya kukupatia majibu.
Ni mimi rafiki yako,
Baraka maganga,
0754612413/0654612410
No comments:
Post a Comment