Habari za wakati huu ndugu mpenzi msomaji wa makala za
mtandao huu, mtandao ambao umelenga kukupatia maarifa ambayo ukiyatumia huta
kaa ujute kwanini uliamua kujiunga na mtandao huu ili uwe unasoma makala zake.
Ni matumaini yangu kuwa unaendelea vizuri sana katika mapambano nami nasema
mapambano yanaendelea na yataendelea.
Ukipanda mahindi utavuna
mahindi.
Ukipanda mtama utavuna mtama
Ukipanda matikiti utavuna
matikiti.
Usipopanda maharage hutovuna
vuna maharage.
Usipopanda mti hutovuna mti.
Usipopanda alizeti hutovuna
alizeti.
Nimeweka kauli hizo hapo juu lengo sio kukuchosha au
kukutaka uzisome tu na kuishia kuzishangaa hapana lengo la kuziweka kauli hizo
hapo juu ni kutaka uweze kunielewa toka mwako ambacho nakimaanisha maana hapa
nataka tuelewane kiurahisi zaidi pengine kuliko siku zote ndugu msomaji wa
makala hii. Kama kichwa kisemavyo kuwa utavuna ulichopanda na hutovuna
usichokipanda. Hivi nikikuuliza ndugu msomaji wa makala hii kuwa uonapo kauli
hii unajifikiria nini juu ya maisha yako. Yaani unaonaje juu ya matokeo
uyapatayo kutokana na shughuli zako?. Na uionapo kauli hii unahusianisha vipi
na ulalamishi au ulalamikaji wa watanzania wa leo. Binafsi naamini kuwa kama
watanzania tungekuwa wenye kuielewa kauli hii vizuri basi leo hii kusingalikuwa
na mtanzania anayekaa na kuanza kuilaumu serikali, wazazi, ndugu au walezi wake
kuwa wao ndio chanzo cha yeye kuto kufanikiwa. Kwanini nasema hivyo mimi nasema
hivyo kutokana na kauli ilivyo.
Kauli inasema utavuna ulichopanda. Kwahiyo ukipanda
ulalamishi utavuna ulalamishi kwahiyo ni kuwa ukimlaumu mtu nae atakulaumu au
nawewe utalaumiwa na wengine. Kauli inasema utavuna ulichopanda na hautovuna
usichopanda hakuna sehemu ambayo imesema utavuna ulichopandiwa na hautovuna
ulichopandiwa hapa naweza kusema kauli hii haitambui jambo linaloitwa utegemezi
hivyo basi kama vijana wangekuwa wanaielewa vyema kauli hii wangeacha maswala
ya kuwategemea wazazi wao kwa kila kitu badala yake wangeanza kupanda mbegu Fulani
ambazo zingeweza kuwazalia matunda Fulani ambayo kwa siku za baadae
zingewaletea matokeo mazuri.
Kauli hii pia inatukumbusha juu ya uwajibikaji nikiisoma
kauli hii nakumbuka juu ya uwajibikaji kuwa kila mtu anapaswa kuwajibika kwa
mafanikio yake na sio kumtegemea mtu akuletee mafanikio. Huwa tunakwepa
majukumu yetu kwa kiasi kikubwa sana, sasa kauli hii inatukumbusha juu ya
uwajibikaji juu ya maisha yetu. Utavuna ulichopanda maana yake unahusikia moja
kwa moja juu ya matokeo uyapatayo maishani. Kama wewe ni masikini mpaka sasa
tambua kuwa umepanda mbegu za umasikini na ndio maana uko masikini mpaka leo.
Hakuna mtu anayehusika na umasikini wako bali ni wewe mwenyewe ndiye
unayehusika nao maana ni mbegu ambazo umepanda wewe mwenyewe bila kumhusisha
mtu mwingine hivyo basi unawajibika kwa umasikini wako na sio vinginevyo.
Kauli hii inanikumbusha juu ya ubora wa mbegu zetu yaani
kama unataka kupata matokeo bora ni
wakati sasa wa kupanda mbegu bora, maana si utavuna ulichopanda maana yake ni
kuwa mbegu bora huzaa mbegu bora na
mbaya huzaa mbaya nyenziye. Hivyo basi panda mbegu bora maana ndiyo ikufahayo.
Maishani tumekuwa tukikumbwa na mambo mengi sana na
tumekuwa watu wa kuwasakizia wengine kuwa ndio wahusika wa mambo hayo
yanayotutokea hata kama ni kwa kuwasingizia lakini huwa tunataka kuuaminisha
umma kuwa hali zetu mbaya ni matokeo ya watu au vitu fulani kumbe tunakuwa
tunajidanganya sasa jambo la msingi hapa ni kuwa kwa kuwa umegundua kuwa
utavuna ulichopanda hata ikitokea watu wanakushawishi uanze kulalamika juu ya jambo
fulani we achana nao maana ukweli wa mambo ushaujua.
Uvivu huzaa uvivu.
Lawama huzaa lawama.
Visingizio huzaa vizingizio.
Tamaa huzaa tamaa.n.k
Ni mimi rafiki yako,
Baraka Maganga.
Wasiliana nami kwa nambari za simu 0754612413/0654612410 au kwa barua pepe:- Bmaganga22@gmail.com.
No comments:
Post a Comment