Monday, February 22, 2016

Fanya Kitu Hiki Na Utafanikiwa Tu




Habari za wakati huu ndugu msomaji wa makala za mtandao huu, ni matumaini yangu kuwa hu mzima na unaendelea vizuri katika kupambana
kwakwo ili tu kuhakikisha kuwa unajiletea mafanikio makubwa maishaniNi vyema ukashikiria yale unayoyaona ni mema kuyafanya na ukayafanya bila kuchoka ili tu ujiletee mafanikio makubwa maishani. Maisha ni mapambano, mafanikio ni mchakato unaoandaliwa sio kitu kinachokuja tu bila kuelewa kimetoka wapi. Hivyo basi pambana bila kuchoka.



Ikiwa unaendelea kupambana ndugu msomaji ni bora ukatambua jambo hili moja nalo ni kuwa ulishawahi kuwaza juu ya kitu kinachoitwa
kurudia/marudio. Yaani kama ulikuwa unafanya jambo ukajikuta unarirudia na kurirudia unajisikiaje? je huwa unakuwa na hiyo tabia au huwa unachukulia kurudia kufanya jambo au shughuli fulani ni kupoteza muda na kujichelewesha, kama huwa unawaza hivyo basi acha kufanya hivyo mara moja maana unajidanganya na kama huwa unakuwa na tabia ya kurudia kufanya jambo husika basi endelea kufanya hivyo maana upo sahihi sana.

Kwanini nimekuambia kuwa uwe na tabia ya kutaka kurudia kufanya shughuli fulani au jambo fulani nimekuambia hivyo kwa sababu moja muhimu nayo ni kuwa kurudia kufanya jambo fulani ndiko huleta mafanikio. Marudio ni mbolea ya mafanikio kama hauelewi au ulikuwa haujui. Ndio nakuona umeduwaa ila ukweli ndio huo kuwa marudio ni mbolea ya mafanikio. Tafsri yake ni nini haswa hapa, hapa tafsiri yake ni kuwa yule mwenye tabia ya kufanya jambo fulani kisha akaendelea kurirudia na kurirudia atakuwa na kuwa mwenye mafanikio makubwa sana kuliko yule ambaye huwa hana tabia ya kurudia kufanya jambo. Kama wewe ni mkulima au ulishawahi kujishughulisha na shughuli za kilimo utajua tofauti iliyopo kati ya mmea uliowekewa mbolea na ule ambao haukuwekewa mbolea. Sasa kama unazijua zile tofauti basi hata katika maisha yetu sisi wanadamu inakuwa hivyo.

Chukulia mfano wa mtu anayejifunza kuendesha baiskeli huwa anakuwa na wakati mgumu sana katika kutekeleza zoezi hili la kuendesha baiskeli, lakini pamoja na ugumu huo ikiwemo kuanguka na kuumia lakini huwa tunaendelea kurudia rudia hili zoezi la kujifunza baiskeli mpaka tunajikuta sasa tumeshakuwa mafundi na mabingwa wa kuendesha baiskeli na kwetu inakuwa sio shida tena. Hali sio hivyo tu katika baiskeli bali hata katika vyombo vya moto kama vile gari, pikipiki, ndege na hata meli. Ujifunzaji huu hutawaliwa na marudio kwa kiasi kikubwa sana kiasi kwamba uwingi wa marudio ndio uendana sambamba na ufanikishaji wa jambo husika. Hapa ndio maana tunasema marudio ni mbolea ya mafanikio.

Wewe unayesoma makala hapa, ulijuaje kusoma, hebu jiulize kwa dakika moja au mbili, ulijuaje kusoma au ulianzaje anzaje mpaka ukajua kusoma?. Lazima kuna hatua za ujifunzaji ambazo ulipitia lakini katika hatua hizo lazima marudio huwa muhimu sana, tulipokuwa watoto wadogo tulikuwa wenye kutaka kujua kusoma na hapo ndipo tulipoanza kujifunza taratibu kuzitamka irabu, na konsonati na baadae herufi, katika kujifunza utamkaji huu tulikuwa ni watu wenye kurudia rudia kujifunza huko matokeo yake leo hii mimi na wewe kusoma sio shida tena hii ni kutokana na sababu kuwa tulijijengea mazoea ya kurudia rudia kile tulichojifunza mara kwa mara.

Sasa ajabu  ni kuwa leo hii tumekuwa hatutaki kurudia yale ambayo tumekuwa tukiyafanya na hii ni baada ya kushindwa na matokeo yake ni kuwa tunajikuta kuwa sasa tuko katika wakati mgumu kiasi kwamba sio rahisi kwetu sasa kuweza kufanikiwa kwa kuwa tunapuuzia vitu vidogo kama hivi. Weka marudio kama kanuni yako ya kuelekea mafanikio hata kama umeshindwa jambo fulani rudia rudia jambo husika na mafanikio utayaona tu tena kwa kiasi kikubwa. Waingereza husema “practice makes perfect” wanamafanikio tunasema marudio ni mbolea ya mafanikio. Hivyo basi uamuzi ni wako kurudia tena kufanya jambo hata kama ulishindwa au kuacha kurirudia hilo jambo huo ni uamuzi wako maana nilishakuonyesha kipi ni bora na kipi sio.

 Ni mimi rafiki yako,
Baraka Maganga.
Wasiliana nami kwa nambari za simu 0754612413/0654612410 au kwa barua pepe:- Bmaganga22@gmail.com.


No comments:

Post a Comment