Umekuwa ukitaka kufanya jambo au mambo mbalimbali maishani au umekuwa ukitaka kufanya mambo mbalimbali. Lakini wakati
hujafanya jambo husika ni muhimu ukajiuliza kwa nini unafanya au unataka kufanya. Mara nyingi sana watu wamekuwa wakifanya vitu kwa kukurupuka sana yaani wao hufanya tu kwa sababu wameona mtu fulani anafanya kile kitu. Maisha hayahitaji maswala ya kukurupuka. Yaani usiwe mtu wa kukurupuka na kuona kuwa hili linawezekana bali kuwa na mipango katika mambo yako.
Leo hii ukizungumzia biashara, biashara nyingi sana
zinakufa kwa sababu watu wanakurupuka yaani mtu anatoka huko bila hata kufanya
uchunguzi wa biashara husika na kujilizisha ndipo aianze ila yeye anakurupuka
na kuanza tu biashara. Huko nyuma nilishawahi kuonya juu ya kufanya biashara
sababu inalipa nikasisitiza kuwa kabla hujafanya biashara fanya uchuguzi juu ya
upatikianaji wa bidhaa, usafirishaji wake, pamoja na gharama za usafirishaji na
vile vile swala la soko yaani ni vipi bidhaa yako inauzika na ni wapi zaidi
bidhaa yako inaweza kuuzika kiurahisi kuliko sehemu nyingine. Hayo ndio baadhi
ya mambo ambayo biashara inahitaji, usiwe mtu wa kukurupuka na kuingia katika
biashara bila hata uchunguzi wowote ule.
Leo hii kila mtu utasikia nataka kuwa mjasiriamali lakini
chunguza kati ya hao wanaosema wanataka kuwa wajasiriamali ni wangapi
wanafanikiwa. Leo hii mtu akimwendea mjasiriamali aliyefanikiwa kuwa ulianzaje
anzaje mpaka ukafika hapo, labda akajibiwa kuwa nilikuwa mwajiriwa na baadae
niliacha kazi na kujiiingiza katika ujasiriamali rasmi. Kwa kuwa amejibiwa
hivyo aendelei kuuliza zaidi ili apate taarifa zaidi na zaidi lakini kwa kuwa yeye
ni mkurupukaji basi anabeba wazo kuwa ili niwe mjasiriamali lazima niache kazi,
ndugu yangu, ndugu yangu kuwa makini sana tena sana maana ujasiriamali sio
kuacha kazi tu na hapo hapo unakuwa mjasiriamali. Unapotaka kuwa mjasiriamali
fanya uchunguzi wa kutosha maana taarifa moja haikutoshi kuna mambo unahitaji
kuwa nayo ili kuwa mjasiriamali bora na sio vinginevyo hivyo basi kuwa makini
usiwe mkurupukaji wa mambo na kuanza tu pasipo uchunguzi
.
Njoo katika ndoa za siku hizi, leo hii kuna ndoa nyingi
sana zinafungwa kweli kweli, tena kwa bwebwe nyingi sana tena sana lakini
chunguza katika ndoa hizo zinazofungwa leo hii au siku hizi ni ngapi zinadumu?.
Utagundua kuwa ni chache sana na kama ukitaka kwenda mbele zaidi kuwa kwanini
hazidumu ni kwasababu wanaofunga ndoa hizi wengi wanakurupuka tu na kufunga ndoa hizo. Leo hii watu wanaoa
au kuolewa tu kwa sababu wameona wengine wanafanya hivyo au kwa sababu baba
alioa na mama nae aliolewa na baba basi nami lazima nioe au niolewe, watu hawa
huwa wanafanya hivyo bila hata kuangalia ndoa hizi zilifungwa katika mazingira
gani na waliofunga ndoa hizo walijipanga vipi mpaka kuzikamilisha hakuna hilo
wao huamua tu kufunga ndoa husika bila hata kufanya tathimini ya kutosha sasa
huku ni kukurupuka kwa kiwango cha juu.
Kimsingi maishani huitaji kukurupuka na kufanya mambo ya
ajabu ajabu au maamuzi ya ajabu ajabu bali inatakiwa ufanye uchunguzi wa hali
ya juu ukijiridhisha na hapo ndipo ufanye hilo unalotaka kulifanya na sio unatoka
tu huko kisa umeona jambo fulani linafanyika basi nawe unalifanya bila
uchunguzi.
Ni mimi rafiki yako,
Baraka Maganga.
Wasiliana nami kwa nambari za simu 0754612413/0654612410 au kwa barua pepe:- Bmaganga22@gmail.com.
No comments:
Post a Comment